BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, July 29, 2009

HAYA NDIO MAMBO YA TANGA JAMANI- TAZAMA HII NYUMBA!!!

Mambo ya Lushoto, mkoani Tanga ndiyo kama hivi. Nyumba tope lakini ungo juu kwa juu na ndani mtandao dot com. Kashangae feriii!!!! Hivi ndio VIJIMAMBO jamani


Saturday, July 25, 2009

CP KUTOKA NA PWAA III- KAA TAYARI!!!


Unakumbuka toka Pwaa ya kwanza kabisa iliyobamba ipasavyo katika anga za Bongo Fleva?
Ikaja Pwaa Part ngoma iliyosimamiwa na Mtu mzima Lucci ambapo ilimpeleka CP katika Level nyingine kabisa, Level za kimataifa, kwani kiukweli ukiangalia au kusikiliza ngoma ya Pwaa Part2 utakubali ya kuwa CP alifanya kazi ya ziada kuanzia utunzi wake mpaka shooting ya Video yake ilikuwa katika “another Level”, ili kuwapa wapenzi na washabiki wake mautamu zaidi na kuonyesha nini amekusudia mchizi muda si mrefu ataachia songi lake la Pwaa Part3.


Bila kuweka kazi ni nani na nani watakaokuwa wamesimama kwenye ngoma hiyo, Cp alisema ya kuwa huo ni mwendelezo wa ngoma yake hiyo ambapo kwa madai yake mwenyewe mchizi amesema anatarajia kuifanya tofauti zaidi, na habari za ndani zinasema kuna Pwaa kibao zinakuja, sasa mpenzi na mshabiki wa CP na muziki wa Bongo Fleva kwa ujumla kaeni mkao wa kula kumsikiliza na kumuona jamaa ubunifu zaidi na zaidi.


THE NGOMA AFRICA BAND WAPATA TENA DILI- SASA KUPIGA SHOW UJERUMANI.

Kundi zima la The Ngoma Band likishambulia jukwaa

Ras Makunja, kiongozi wa bendi hiyo akionyesha makeke yake.


The Ngoma Africa Band aka FFU! Kukiwasha cha moto kingine ndani ya
AFRILU Festival, Ludwigshafen City,Germany siku ya Ijumaa 24.7.



Kamanda Ras Makunja atakiongoza kikosi cha The Ngoma Africa Band aka FFU katika jukwaa lingine la onyesho la AFRILU .Onyesho hilo litakalo fanyika siku ya ijumaa 24.07.2009 jioni katika uwanja wa Ebert Park,mjini Ludwigshafen,huko Ujerumani,ambako washabiki wengi wanasubiri kucheza gwaride na ffu wa Ngoma Africa band.habari za uhakika zinatonya kuwa Karandinga la FFU hao linapiga misele na kwenda kwa kasi kuelekea katika maonyesho hayo!
ambapo washabiki watapata burudani ya aina yake.
Usikose kupata mziki hapa
http://www.myspace.com/thengomaafrica pia unaweza kuwasiliana na ffu at ngoma4u@gmail.com



Monday, July 20, 2009

WAGOSI WA KAYA NA TANGA KUNANI...!! JAMAA WAPO KIMYA SANA JAMANI


Kwa wale ambao wamekuwa wafatiliaji wakubwa wa muziki wa bongo flava nchini Tanzania, hakika watakuwa wanawafahamu WAGOSI WA KAYA- vijana mahiri wa muziki huo kutokea hapa jijini Tanga.


Kwa hakika walibamba sana na staili yao ya ki'lugha....kwa maana ya kisambaa na kidigo, hawa wa Dr John na mwenzake Mkoloni. Unakumbuka ngoma zao kama TANGA KUNANI, WAUGUZI, TRAFIKI HAYAAAA!!, KEROOO, SOKA LA BONGO na nyengine kibao tu!!


Baada ya kukumbuka nyimbo hizo, jiulize ni kiasi gani zilikubamba na je sasa hivi wapo wapi na wanafanyanini...!!??? Ukimya wao umeonekana kuwagusa watu wengi ambao kwa namna moja ama nyenigne walikuwa tayari wameshazama kwenye dimbwi la upendo wa nyimbo zao ambazo zilikuwa zinagusa moja kwa moja jamii ya kitanzania.


Kwa hapa Tanga jamaa walikuwa kama akina P Square wa kule nchini Nigeria, si mtoto wala mkubwa- kila kona utasikia TANGA KUNANI kama vilivyo VIJIMAMBO VYA TANGA kwa sasa. Duh....jamani mmekaa kimya sana wagoshiiiii, tunaomba mrudi tena ili tufurahie tena ladha zenu za kisambaa na kidigo.


HAYA NI MASHAIRI YA WIMBO WA TANGA KUNANI!!
Wagosi wa Kaya - Tanga kunani?


(verse 1)Tanga kwa kweli ni kijimji kidogo, na pia kuna mambo ya uswahili si kidogo. lakini habari zake kwa kweli ni kubwa, na mji ule ukiuvamia kwa papara palee, mengi yatakukumba! Ukifika Tanga utatambuaje kama kweli huu nd'o mkoa wa Tanga?Utaona wanawake wengi palewamejifunika mabaibui na vijikanga. Waume makanzu baraghashia, mkononi tasibihiwanakuhesabia.
Baiskeli ndiyo teleeee, mpaka zawakera wenye magari barabaraniHalafu hali ya sasa sii kama ile yazamani, ukaenda ovyo tu utauza kila kitu chako cha thamani.Matajiri wa enzi zile ukiwaonaleo hii tena hawana thamani Enzi zile bwana mkoa wa Tanga kilakitu mambo yalikuwa swafi. Mijikazi ilikuwa tele, na kulikuwa hakuna mambo yaukorofi, lakini sasa hivi thubutu, twendelea kuchakaa mpaka tutoke ukurutu, hakuna ndimaa, kilo mtuambiwa ajifanya mvuvi ati, na ukamshauri mtu akushushia varangati, astaghafirullai laadhim!Watu waongea peke yao kamavile wendawazimu, labda tutambikemizimu huenda kidogo pale mamboyakany'oka. Palikuwa na viwanda na mashamba ya mkonge telee. Haviwapi sasa? Utafikiri mamiye mwali aliyefunga kizazi bwana, maana havizalishi ati, vyote viko, nyang'anyang'a. Hali hii kutupa vitu njia panda, yaonyesha kabisa tayari maisha yeshatushinda. Watu kilo siku waenda kwa waganga, ukipita pale mara kumevunjwa nazi, mara huku nako kule kumetupwa hirizi, mwatakani basi nyiye wana msiotulia?


KIITIKIO



Tanga, kunani paleee, mbona kila kitu pale kimekufa, Tanga, kunani paleee, mbona maisha pale yanasikitisha.
(verse 2)lshi Tanga lakini kuwa makini,watu wajua mpaka siri zako za ndani, sijui habari hizi huwa waambiwa na nani?
Hospitali ya Bombo ya leo ni vichekesho,ukienda pale hata kama utumbo uko nje, utaambiwa tu matibabu kesho. Tanga, Tanga jamani yarabi toba.Ndege pia kwa mwezi twaona mara moja, basi balaa hili watu tumekuwa twaishi maisha yatumbiri, sijui tusomeane alubadili,ili tumkamate alotu filisi utajiri.Bandari nayo sasa yachungulia shimo, zamani waweza ona miji meli palee wala haina kipimo, lakini! sasa hivi si meli tena, wala hazina uwezo wa kubeba hata kontena. Ukiondoa Wahindi na Waarabu, Waswahili wenye pesa ni wa kuhesabu, halafu wikiendi angalia nyendo zao, kuchukua wake za watu na kutaka mambo nje ya uwezo wao.
Saruji ndo kiwanda arnbachokimebakia, panga pangua makaburu wameingia ubia. watafanyabiashara miaka mitano haifiki nao wale pia watajiondokea
Railway kimyaa, zamani wenyewepale tulishaizoea mijihoni, sasa hivibehewa moja la abiria hatulioni,mwawekani basi mabehewayaloozana pale. Si muondoe jamayaleta mafico wezi yale.


KIITIKIO



(verse 3)Hatijawahi kulalamika sisi hatasiku moja,najuu ya maisha ya Tanga MC natoa hoja, msije mkaona mzaha jamani hivi si vioja, kucheka mtacheka lakini mkoa unadodaViongozi wetu kazi yao hawajui hata moja, vikao vyao n'vingi wanakutana Mkonge Hotei,na agenda za huko hawatiambii ukweli.
Promise zao ni za uongo haziambiiki, sijui wametuona mma'bahau ama m'visiki,Tinapomichagua majukumu yenu mnayatambua? Au mnaona raha dada zetu kuuza vitumbua?
Titabeba zege mpaka lini na kujitutumua? Inaelekea mmetisahau halafu pesa mnazitumbua.Na huu mpango mpango wa Tanga wa vipande vya baiskei,titakuja kutoana roho mchana mchana aisee, tinashikwa na mgambo ili tilipie manispaa, wakati wagosi wa kaya wenyewe ti nakufa na njaa. asalam alekum wallahiNdio maana akili zetu mnasema hazifai, na asubuhi ni mnazi badala ya chai.Pamoja na viwanda na upuuzi huo kufa, elimu tinaichezea halafu kingereza n'cha ugoko. Tisibishane hapoo!Sasa tirudi katika suala ya maendeleo, tinapataje mtaji kwa ajili ya haya maendeeo? Kama si kupakiza magunia kwenye Shengena, tinalipwa hela kidogo haafu tinasengenywa.Chai asubuhi ni kavu hakuna cha kutafuna, watoto wamezoea ubwabwa siku huna hela wananuna,
Wake zetu wamekakamaa utadhani wanafanya diet, haku nacha diet hapo ukapa umepanda chatiNa ukitaka kujua n'balaa kwa haya tinayosema,uwanja wa sabasaba umekufa, hata jumba ya sinema.Msije mkani kumbusha mimi hapa naweza kulia.Oh Tate none wa Tanga tushikamane.Mike Byanaku ni fundi mzuri wa baiskeli, anasaidia sana lazima niseme ukweli. Anapogonga nyundo Wahindi wanasema n'kelele,nntafutieni nyundo yasailensa aondoe hizo kelele.
Na nyie na magari yenu msipige honi wala misele, hapo titaelewana.Tanga tina barabara maarufu na ziko ishirini na moja, na hizi zimejipanga panga na ni hatari kwa vioja, tega sikio usikie ni kitu gani kinakuja.
Tinao akina kaka wanaoshikishwa ukuta, wengine wanajifanya waswalihina wanakula kitimoto, hatiwasemi tinaogopa mkong'oto.Tanga Wahindi wamejazana kwenye maghorofa ya msajii,tunabaki kuhangahanga Kwanjeka sisi waswahii, ukipita chini ya ghorofa wanakutemea mate ya palikiUkiuliza hivi n'kwa nini matusi yake hayaambiiki. Weee Master J!Kuna siku n'tampandia mtu ghorofani nimtoe roho, halafu n'pelekwe kwenye gereza la Maweni n'kanyee ndoo.Timeshachanganyikiwa mnatiletea ubishoo.Juhudi zako zinaonekana sana Kapteni Mkuchika. Afadhali sasa kidogo Tanga tinahema na kucheka.Maneno tinayoongea hapa hatumpigi mtu kamba, Wagosi tinamalizia na salamu kwa Makamba.Baba yetu Makamba, hawa akina matonya hawako tu pekee Daisaama, hata kule Tanga wamejazana ni kiama.


KIITIKIO


PATA NGUO ( PAMBA) ZA UKWELI KUTOKA KINA KLOTHING..!!


Salaam kwa wadau wote.
Kina Klothing ina furaha kuwafahamisha kuwa tumefungua duka letu mtandaoni na unaweza sasa kununua Tshirt moja kwa moja kupitia http://www.kinaklothing.com/

Kina ni kampuni mpya ya nguo ambayo inawakilisha Bongo na Afrika kwa ujumla. Kwa utambulisho tumetoka na kollektion inayoitwa Uhuru St. kwa sababu neno uhuru linabeba sababu nzima ya sisi kuanzisha Kina.

Vilevile hii ni lebo ya mavazi ya kitaa na Uhuru ni mtaa wa kwanza katika mfululizo wa kollektion zitakazobeba majina ya mitaa mbalimbali ya Bongo na Afrika kwa ujumla.

Kama kauli mbiu yetu inavyosema “Vitu vyetu. Kivyetu” basi ndio tunavyotarajia kuendesha lebo yetu, yaani full uhuru wa kutengeneza kazi zinazotuwakilisha, kwa namna tunayoamua wenyewe.

Tshirt hizi zimesanifiwa mahsusi kwa ajili ya wabongo na marafiki zao ili kuonyesha kuwa wabongo nao tumo katika medani hii ya design; lakini si hivyo tu, ujumbe unaobebwa na nguo kina ni mchango wetu katika harakati za kujenga madaraja kati ya waafrika barani na diaspora kwa kusambaza na kusheherekea yale yanayotuunga pamoja kama waafrika.

Hata hivyo, katika kollektion hii ya kwanza tumeamua “kucheza kwetu” zaidi, tunatumai utatutunza.
Tutembelee www.kinaklothing.com na tuambie mawazo yako.
Pia usisahau kujiunga nasi katika ukurasa wetu ya facebook (http://www.facebook.com/pages/Kina-Klothing/101720604819) na kutufuatia katika http://www.twitter.com/kinaklothing

Kaa mkao wa kula kwa kollektion inayofuatia, Samora avenue. Iko jikoni.
Amani.

Mkuki na Susan (Kina Klothing)

Friday, July 10, 2009

HII NDIO TANGA CITY- KWA WALE WASIOIJUA VIZURI!!!


Hapa maeneo yaTunakopesha Ltd, kama unaelekea Tanesco!




Hapa ni stendi ya mabasi ya mikoani, tazama mabasi yanavyong'ara huku watu wakipita




Eneo hili ni nyuma ya Club maarufu jijini Tanga Lacasa Chica. Lakini ukisogea kwa mbele utakutana na jengo la TTCL na jengo la Benki ya Posta.


Hili ni jengo maarufu kwa kukodisha ofisi. Humo kuna ofisi nyingi- jengo hili linatazamana na jengo la Nasaco karibu na hoteli ya Meridian



Hapa ni makutano ya barabara ya kwenye hospitali ya Bombo na Bandari ukiwa unatokea maeneo ya Tanesco.

Ushawahi kusikia zile barabara za namba, yaani kuanzia moja hadi ishirini..? Basi hii ni Taifa Road lakini ikiwa ni barabara ya 12 jijini Tanga.


Huku ni maeneo kama unaelekea Splendid Hotel, moja kati ya hotel maarufu jijini Tanga.



Hilo jengo la rangi ya pinki, ni jengo la Benki ya Exim. Moja kati ya benki zinazotoa huduma nzuri.



Maeneo ya jengo la TTCL likiwa limepakana na jengo la chuo cha Engusero hapa jijini Tanga.



Jamani eeh, hili ni moja kati ya majengo maarufu Tanga. Lipo maeneo ya Four Ways. Kuna huduma nyingi za kijamii zinatolewa hapo.



Hi ni clock tower ambayo ipo maeneo ya Chumbageni kama unaelekea Chuda Raha.



Hili ni jengo la Toyota, kama unahitaji magari ya aina hiyo utayapata jijini Tanga pia. Uliposikia Tanga ni jiji, sio masihara mdau!!




Makutano ya barabara ya Tanesco kwa magari yanayofanya mizunguko ya mji kuelekea Raskazoni.



Hili ni jengo la Benki ya Baclays hapa jijini Tanga. Moja kati ya mabenki ambayo yameamua kutoa huduma zake kwa wakazi wa hapa.




Stendi tena, tazama dada na ushungi wake akikatiza mitaaa!!



Kwa wale wapenda starehe, naweza kusema MAMBO IKO HUKU!!! Jengo la klabu Lacasa Chica- Club maarufu jijini Tanga kwa starehe. Wasanii wote wa muziki hufikia hapa kwa ajili ya kukonga nyoyo za wapenda raha- TANGA RAHA!!!



Maeneo ya Four Ways, hili pia ni jengo ambalo kwa hakika linatia fora. Kwa pembeni kama unaelekea barabara hiyo, kuna bonge moja ya Bar maarufu sana kwa nyama choma!!


Tazama bustani zilivyonakshiwa vizuri. Hili jengo linatazamana
na viwanja vya Tangamano ambavyo ni maarufu sana kwa soko huria.



Jamani...hii yote ni Tanga. So enjoy ili na wewe siku moja uje kupaona!



Jengo refu kuliko yote jijini Tanga la Bandari, ambalo kwa hakika ni moja kati ya vivutio. Ukipanda jengo hili utaiona Tanga nzima, na pia kwa upande wa pili utaiona bahari ya Hindi ambayo watu wa Tanga pia tumebarikiwa.


Next time nitawawekea picha za vivutio vya asili ambavyo vipo Tanga kama mapango ya ambaoni n.k.- Hii ni zawadi kwa wadau wangu popote pale mlipo. Karibuni Tanga jamani, tule raha na kufurahia upepo wa pwani!!!



Tuesday, June 30, 2009

ROMA KUTOKA NA MR. PRESIDENT- GET READY MDAU!!!


Msanii kutoka Tanga, Tanzania ambaye ameonekana kuleta mapinduzi makubwa kunako game ya muziki wa bongo flava Rymes Of Magic Attraction a.k.a ROMA- amepiga story na Blog hii kutanabaisha kuwa yupo mbioni kutoka na ngoma nyengine atakayoiita Mr President.
Roma ambaye pia anatamba na wimbo Tanzania, ambao kwa namna moja ama nyengine umekuwa ukifanya vizuri karibu redio zote nchini.
Kama umepata bahati ya kusikiliza wimbo huo utakubaliana na mimi kuwa ROMA- sio mkali tu wa kwenye Ku'Burst hata kwa mashairi pia amekuwa akikimbiza sana.
Mashairi ya wimbo wa Tanzania umekuwa ukigusa hisiza za watu wengi sana, kiasi cha kufanya msanii huyo kupata mialiko tofauti tofauti hapa nchini.
Hata hivyo ROMA hakutaka kutaja ngoma yako hiyo mpya ya Mr. President ataifanyia wapi, ila amewataka mashabiki wake kote nchini kukaa tayari kwa jiwe hilo jengine.
Mwana'Hip Hop huyo ambaye anaamkini kuwa HARAKATI ZA MAPINDUZI NDIO JADI amedai kuwa, ili wasanii waweze kujikwamua kunako game ya muziki wa bongo flava nchini Tanzania basi wawe wabunifu kwani sanaa ni kazi!!
HAYA NI MASHAIRI YA WIMBO TANZANIA YA MSANII ROMA- LAKINI KWA LUGHA YA KIINGEREZA
Verse 1
I1961 kambaragle became a heroYess R.I.P Maria is crying for youIn soul you are with us but in body you are lost alreadyYou resigned when we still needed youYou didn’t wanted to long in powers, you left them to Ali HadjiNow they fight for presidential house with raw lustWords of their campaign is to get income to the citizenTZ is rough everything is zigzagGood people die early, why bad people don’t?Racism and corruption in offices are obviousHe was a vetenary, abrupt he is football secretaryThey bought certificate that they could get degreeAcademic with no future to people who studied scienceBuildings are falling due to engineers forgeryIm hustling, sweat is spilling just for money to buy food Mamy don’t cry daddy weep your tears stop cryingNay real stop cryingI see you much excited like morale of masai
Chorus
This is TanzaniaCountry with a sinful soilThey are looking for diadem of winningSay TanzaniaIm holding bible protesting who fights to be kings or queensThis is TanzaniaThey got endowments of reprobationThey do projects inside our religionsIm saying TanzaniaThe lost state, Tanzanian are crying for your fake promises
Verse 2
If only God could decide that we should attend funerals dailyI belive we could have learnt how to liveEva remember gomor, Adam remember SodomThen together lets pray, that wouldn’t happen as in nuru and safinaCoz in house of prayers they do sinsOpium in streets, that they could get winning diademThey use religion envelops to sell drugsRemoving demons with the power of darknessThey break the sixth commandment in churchsAnd worshiping gods inorder to get moneyInfront of Getrude Rwakatale’s altarOr bishop kakobe they fall infront of altareeeeeeeeeeeThey have given false testimonyReligion has become business, members of the church are corruptedThey wrote false proposal that they could get luckyThey pretend this reprobation as entrepreneurshipSee, police in streets their bosses are drug dealersHigh rank leaders gives out their phone numbers that would get corruptionStill they open places to aid people who have AIDSThey don’t have talents they establish them to get economy profit………………. There ustadh hold your heart Better the blessed one with clean heart,I don’t know what he knows about methewThey prepare robberies, broke in and rob the bankThey met to a bar to divide 10percent among themselvesMoney is too illicit it jeopardized even PetroAfter cock crowed he discovered he forsaken ChristIm recording my track with bible in my left handIm crying for Tanzania tears fill my eyes
Verse 3
I have been hearing about reprobationAnd as they increase is as more I get excitedThey use government fund to start their businessThey own mines and house like sinagogThey were set up that they raped childrenThey are convicted without evidence, Pilato’s like judgementThose who steal millions go unpunishedMy uncle’s son got two years in prison because of bhangi smoking…………….distress cause his deathWho deserved conviction? Him or friend of ……………….I hate entertaining cowards disciplineI cant ignore the sins i witnessI know who talks the truth dies early, I don’t careIf you killed Amina, here I stand strong1st I got permission from home and my grand slaughtered a cow for meI drank its blood and he blessed me that I come to town to stand 4 inferiorsPayment is in the world, now they die one by oneAnd they leave behind their wealth, they didn’t know “dunia mapito”Life is not fair, if was like CollinaDefenders are bullied like sarafina’s teacher Their drivers approach women for their safeKills a lot of innocent bloodsTheir wives go out with youth undisciplinedBecause their husband are busy with illegal dealsThe price of their cars can build a school in villageThere are illiterate children grazing cows in villagesIm standing still like sayuni mountainFor this strike I believe I won over satan .
Kaeni tayari kwa ngoma mpya ya ROMA ambayo itaitwa Mr. President

Friday, June 26, 2009

MICHAEL JACKSON AFARIKI DUNIA- REST IN PEACE!!

Mwanamuziki wa Pop ulimwenguni Miachel Jackson, amefariki dunia usiku wa jana wa tarehe 25/06/2009 huko nchini Marekani mjini Los Angeles baada ya moyo wake kushindwa kufanya kazi.



Bila kujua kwamba amebakiza siku 113 tu za kuishi duniani, Michael Jackson alipokutana na waandishi wa habari mjini London Machi mwaka huu, aliwaahidi mashabiki wake wa Uingereza kuwa onesho lake lililopewa jina la THIS IS IT TOUR lililopangwa kufanyika O2 Arena kuanzia July 09 mwaka huu, lingekuwa onesho kali la kufungia pazia katika historia yake ya maonesho!


Masikini, hilo halikutokea kama alivyotaka, kwani Mungu naye tayari alikuwa na mipango yake isiyobadilika. Inaelezwa kuwa tiketi za onesho lake zilikuwa zikiuzwa kati ya paundi 50 na 75 na zilitararajiwa kumuingizia jumla ya paundi milioni 175!!!! Hii ingekuwa imemaliza kabisa matatizo yake ya kifedha aliyokuwa nayo

katika press hiyo, Michael aliahidi kwa kusema maneno yafuatayo kwa wanahabari wa Uingereza: “I’ll be performing the songs my fans want to hear. This is really it. This is the final curtain call. I’ll see you in July.” (Nitaimba nyimbo wanazopenda mashabiki wangu kuzisikia, huu ni uhakika. Huu ni wito wangu wa mwisho, tutaonana mwezi wa saba)


Michael Jackson amecha watoto watatu - Michael Joseph Jackson, Jr., Paris Michael Katherine Jackson and Prince "Blanket" Michael Jackson II


HAKIKA KIFO HAKINA HURUMA- PUMZIKA KWA AMANI NDUGU YETU MICHAEL JACKSON A.K.A WACKO JACKO





Mashabiki wa Michael Jackson wakiomboleza msiba kwenye mitaa mbalimbali huko nchini Marekani.




Watu wakitazama Video za msanii Michael Jackson mara tu baada ya kupata habari juu ya kifo chake.


Njemba ikiomboleza


Kweli Wacko Jacko alikuwa ni mtu wa watu!

Jamani eeh, Think- How many stopped breathing since the year started..? How many had bad accidents which left disabled?? Tunapaswa kumrudia Mungu.

Kila hatua katika maisha yako ifanye kama funzo, yeyote atokae upeoni mwako kwa njia ya kifo chukulia kama ndugu yako kwani ipo siku yatakufika pia, wahenga wanasema KIFO HAKINA MWENYEWE!!

RAMBIRAMBI KWA WADAU

DJ CHOKA: Ur the best Michael.....1 in a million....truely amazing. RIP. Condolences to your family. And all the mother %$^&% who dont like michael.....die in hell.

3232 Dar:i grew up listening to ur songs michael....cant believe ur gone....peace be on ur soul.... ur the King ...ur the King...!!

LETH: Rest in peace. Just saw his wife's profile on milllionaire personals site """"" W e a l t h y D a t e r . c o m """""" last week. I am wondering what kind of relationship she is looking for on that site.

LUCY NGOWI:condolence to the family of Michael Jackson,we are saddened for the untimely death of a great artist,may you rest in peace mike,we will never forget you,we will surely miss yo

CUTE:weve lost the best singer and dancer and i think no one can be as good as him.HES THE BEST. safia Dubai UAE

HASNA: sikutegemea kama mwisho ungekuwa kama mshumaa unaozimika kwenye upepo, RIP Wacko!

IDDA ELIAS:AFTER DEATH IS JUDGEMENT.LET US ALL LEARN FROM THIS MAN.I WILL NOT LIKE TO JUDGE HIM BUT MY HEART GOES OUT TO HIS FAMILY


ANKO MO: Michael you are great hero and we love you but God love you most, may your soul rest in perfect peace.

Sunday, June 21, 2009

BENNIE MAN KUPIGA SHOW TANZANIA- ARE YOU READY.!!!

Msanii Bennie Man kutoka nchini Jamaica, anatarajiwa kutua nchini Tanzania kunako jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kupiga show moja ya ukweli. Kwa mujibu wa Str8 Music Entertainment moja ya wadhamini wa show hiyo, Binnie Man atasindiizwa na T.I.D, Makaumua na Q Jay, Hussein Machozi, TMK Wanaume Familiy, CP, Mangwear pamoja na wa vipaji kutoka Tanzania House of Talent (THT). Wazeeeeya kaeni mkao wa kula pande za DSM!!


JAMANI! TUNAELEKEA MISS TANZANIA.

Nawakumbusha tu wadau wangu hususani wakazi wa Tanga kuwa tunaelekea Miss Tanzania, Je dada yetu Glory Chuwa atapenya hapa..? Tumuombeeni heri na baraka.

Saturday, June 13, 2009

MWAMBAO FM ILIVYOVUMBUA VIPAJI VYA UWIMBAJI!!


Dj Shago 66 na Dj Bob Nas wa Mwambao Fm wakiweka mambo sawa kuhakikisha muziki unatoka vizuri ili kuwapa shangwe mashabiki pamoja na wasanii.


Msanii kutoka kundi la Street Coulor akiwakilisha vya kutosha kwenye stage. Fainali hiyo ilifanyika kwenye ukumbi wa La Club Tanzanite.

Star B akiwa kama ni solo artist, akijituma ipasavyo kuhakikisha anaibuka bingwa!


Masotojo kutoka Tanga alipiga show katika harakati za kuchuja wasanii watakaoingia mkataba na Mwambao Fm kupitia Mwambao Record.


Mshiriki anayejulikana kwa jina la The Drama, akionyesha kipaji chake jukwaani.

Wazee wa Shino Style- Shomy Luv pamoja na Big Smart wakitoa burudani kali kwenye ukumbi wa La Club Tanzanite siku hiyo ambapo wasanii wanne waliweza kuingia mkataba na Mwambao Record.


Baadhi wa Presenters wa Mwambao Fm, Mamaa Nusura Abdalah wa kwanza- Dj Rach Kuty aliyevaa fulana ya kijani pamoja na Benedict Kaguo a.k.a Father K wakifuatailia kwa makini fainali hiyo.


Usipiime!! Kulijaa watu sio mchezo. Hakuna aliyetaka kupitwa- wadau wote wa muziki wa bongo flava waklikutana hapa.



Majaji walikuwa na kazi nzito!! Wa kwanza ni Jaji Anko Mo kutoka Mwambao Fm na aliyevaa kofia ni Dr Leader ambaye pia ni msanii- pamoja na Sam Chad Producer kutoka King Falcon.


Dr Leader na Sam Chad wakiteta jambo.

Leader akaona haitoshi- akamgeukia Anko Mo kwa kuteta mengine zaidi.


Dj Bob Nas akijaribu kumueleza jambo mshereheshaji wa fainali hiyo Ahmed Khatibu (wawoo)- Shindano hilo la kutafuta vipaji lilidhaminiwa na redio Mwambao Fm kwa lengo la kuwapa vijana ajira kupitia tasnia ya muziki. Washindi walikuwa ni Razy Flava, Chabo, Star B pamoja na The Drama.