BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, August 17, 2009

SHOW YA TMK FAMILY NA TIP TOP CONNECTION JIJINI TANGA- AIBU TUPUUU!!! (PART ONE)



Meneja wa kundi la Tip Top Connection Hamisi Tale maarufu kama Babu Tale akipiga msosi, kabla ya show kuanza

Nae raisi wa Manzese- Madee akipiga menyu kali katika kuhakikisha anakamua ipasavyo stejini
Mkubwa Fela pamoja na Tunda Man wakiteta jambo kwenye hoteli waliyokuwa wanapata chakula mchana wa jana kabla ya show

Hapa nje ya uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga- watu wakiwa kwenye foleni ya kukata tiketi kwa ajili ya kuinghia ndani.

Show ilichelewa kuanza- na hata ilipoanza ilikuwa tayari watu wameshachoka. TMK ndio walioanza kutoa burudani.


Kilichowashangaza watu wengi ni kwamba, hakukuwa na STEJI hivyo wasanii wote kulazimika kufanya show kwenye vumbi.



Pamoja na kupiga show kwenye VUMBI lakini Wanaume walipiga mzigo hivyo hivyo huku Chege Na Temba wakionekana kuokoa jahazi.

Dah mdau usipimeee!! ilikuwa noma- wasanii walikuwa wanaimba huku wakiwa na nyuso za huzuni kutokana na kutofurahia mazingira yale ya vumbi. Ilikuwa kama tupo kwenye hizi disko za mitaani maarufu kama DISKO VUMBI!


Miguu ya msanii maarufu nchini Cassim kama inavyoonekana katika picha ikiserebuka
Tunda Man alikuja baadae sana nae kuokoa jahazi- hata hivyo alipigiwa shangwe alipoimba wimbo wa Nipe Ripoti na Neila


Zantel nao walikuwepo kutoa sapoti kwa CHAMA KUBWA!!


Bra-A aliyevaa kikoti na Anko Mo kutoka redio Mwambao wakiwa na msanii Keisha

Ilipigi Mkubwa Fela amsimamie Dj kutokana na mauvundo aliyokuwa akiyafanya




Keisha aliimba wimbo mmoja tu wa Uvumilivu aliomshirikisha Squizer- kushoto aliyevaa kofia na kitambaa ni Abdu Bonge wa Tip Top.
Pamoja na kukosekana kwa Steji- jamani hata TAA pia hazikuwepo. Uwanja mzima ulikuwa kiza- wasanii walifanya show kwenye vumbi huku wakimulikwa na taa za magari matatu yaliyokuwa yamewasha taa za mbele.
Kwa upande fulani, show ilikuwa kama yakulazimasha sanaaaa! Coz tayari watu ndio wameshaingia, pesa wameshatoa- kurudisha itakuwa ngumu na wakati huo huo hakuna STAGE hakuna TAA. Ikabidi iwe hivyo hivyo bora liende ili kuepusha shari.


Kutoka Da Hot Beat Show ya Mwambao Fm Redio jijini Tanga: Bra-A, Moshen Habib na mtu mzima Anko Mo wakifuatilia show ya Chama Kubwa kwa makini.


TMK Wanaume Familiy na Tip Top Connection wapo kwenye ziara mikoani kutambulisha albamu tatu kwa pamoja ambazo ni FELA NA WANAWE ya kwakwe Mkubwa Fela- PESA YA Madee na Mtoto wa Kichaga ya Mh. Temba.
Kama kuna mikoa ambayo tayari wamepita na kufanya show- basi hii ni show yao ya kwanza kuharibu hapa Tanga. Kama una maoni kuhusiana na show hii niandikie kupitia E-mail yangu ambayo ni
ankomo25@yahoo.com MAONI YOTE NITAYAWEKA HAPA HAPA!!
Hii ni Part One jamani-




2 comments:

  1. SASA NAOMBA KUULIZA, HIYO SHOO ILIONEKANA KWELI KAM HATA TAA MLITUMIA ZA MAGARI? MAANA HATA HIZO PICHA HAZIONEKANI! KWANI KIINGILIO KILIKUWA SH. NGAPI?

    ReplyDelete
  2. Nimefurahi kuona taswira mbalimbali hususani ya Tanga. Karibu nawe kibarazani kwangu kubadili mawazo

    ReplyDelete