BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, March 31, 2010

TID AJITOA TUZO ZA KILI!

Naomba radhi kwa mashabiki wangu wote kutoka pande zote za sayari hii najua mlikua mnasubiria kunipigia kura kwenye hiki kinyanganyiro cha award hizi za kilimanjaro,najua imekua uamuzi muafaka kwangu kujitoa kwene awards hizi basi naomba muelewe sababu zangu hizi za msingi:

1.Kwanza nahisi mimi kama TID na mziki ninao perfom kwa kipindi chote hiki cha miaka saba toka nimepewa tunzo hizi sina umuhimu wa kuwa shiriki sababu hata nikitengeza wimbo ambao unakubalika sana na wapenzi wa muziki huu wa kizazi kipya sipewi tuzo kwa mantiki hiyo naona sioni sababu ya kuwa kwenye tuzo hizi.

2.Pia nilidhani labda ni upungufu wa mawazo ya majaji ama waandaaji ambao imewezekana nilitofautiana nao kipindi fulani nilipokuwa nafanya nao kazi za maonesho,inauma sana unapoona wengine ambao uko nao kwenye same field wanapewa nafasi kubwa ambayo pia mimi nastahili kutokana na juhudi ambazo nafanya kwenye sanaa hii ya kizazi kipya hapa nahisi sihitajiki kwani kama wimbo wangu wa bendi ni bora wa mwaka kwanini nisiwe mwanamuziki bora wa kiume mwaka huo,pia hata video zangu huwa za viwango vya juu nazo hazipewi nafasi kwenye video bora za mwaka!

3.Kwa sababu hizi ambazo mimi naona kwangu hazinijengi sioni sababu ya kuwepo kwenye TUZO hizi tena kwani sidhani kama ni wakati wa kuwaangusha mashabiki wangu ambao natumia muda mwingi na effort binafsi bila ya mdhamini kuwaunganisha na muziki wangu basi nisameheni kama nimewakosea lakini hainisaidii chochote endeleeni na hao mnaowapa kila category i will never stop making good music for my country surely i wont,i was born to do THIS,.. THANK habari kutoka topbandtz.blogspot.com

Kwa mwaka huu msanii huyo kupitia Top Band na wimbo wa ASHA alikuwa akichuana kunako tunzo ya Wimbo Bora wa Kiswahili kwa upande wa bendi, ambapo Machozi Band (Nilizama), African Stars Band-Twanga Pepeta (Mwana Dar es Salaam), FM Academia (Vuta Nikuvute) Extra Bongo (Mjini Mipango) zikiwa kwenye category moja.

MADEE ASHINDWA KUSIKILIZA WIMBO WA 'PENDO'

Msanii wa kundi la Tip Top Organization Ahmad Ally a.k.a Madee ambaye hivi karibu alifiwa na mchumba wake anayejulikana kwa jina la Pendo, amekamilisha wimbo wa kumuenzi mpenzi wake huyo ambao ameupa jina la PENDO akiwa amemshirikisha Matonya kutokea Tanga!

Kwa mujibu wa meneja wake Babu Tale amesema kuwa wimbo huo umetengenezwa Tongwa Record na msanii huyo ameimba kwa hisia kali kiasi cha kufanya utoe machozi utakapousiukiliza.

Aidha Tale amesema kuwa punde tu baada ya wimbo huo kumalizika, Madee alishindwa kuusikiliza kutokana na machungu ya kuondokewa na mpenzi wake ambaye katika wimbo huo amedai kuwa maisha yake yatakoma.

"Ni kwamba alipo maliza kurekodi alishindwa kuisikiliza aliishia kulia na akaondoka mpaka mie nikaifuata jana studio" alimalizia Tale

Tuesday, March 30, 2010

RICHA ADHIA DOES TANZANIA PROUD

Samsung Miss Tanzania India Richa Adhia , Tanzania’s First representation at the 19 Miss India Worldwide pageant, saw this Stunning beauty enter top Ten at the glamorous Pageant held at the International Convention center , in Durban on 27 March 2010.

Richa won The TOP MODEL awards at the Contest which was Won by South Africa’s kajal Lutchminarain whose first and second runner up were United Kingdoms Niharica Raizada and Suriname Cher Marchand respectively.

The 20 Miss India Worldwide will be Held on 26 March 2011 in Hague, Netherlands.

TATIZO HAWAJUI KUANDIKA- MASTER J

nini haswa kinachowafanya wale nyota wa taji kubwa la Bongo Star Search BSS kila mwaka...kushindwa kuwika kwenye soko la muziki kama ambavyo wengi wetu tunategema,mmoja wa majaji wa tuzo hizo na akiwa mmoja wa Maprodyuza walioishep Bongo Fleva wakati inasimama na kukubalika pamoja na aina nyingine ya muziki anasema sababu kubwa la nyota hao kutoonyesha cheche sokoni ni kwasababu hawawezi kuandika.

“Tatizo si BSS, Benchmark, Madam Rita wala majaji, tatizo ni wasanii wenyewe kwa sababu hawana uwezo wa kuandika na kuandaa nyimbo zao ili zikubalike. “Wasanii wanaposhiriki BSS, wanaimba nyimbo za watu, kwahiyo wanaonesha uwezo wao kwa kuimba tu, hivyo wanakubalika na wanapigiwa kura lakini kwenye kutunga hakuna.

“Hii ndiyo sababu Jumanne Idd (mshindi mwaka 2007), Misoji Nkwabi (2008) wameishia njiani, unaona hata Pascal Cassian (2009) bado hajasimama, angalau Peter Msechu (1st runner up 2009) anaokoa jahazi.

“Nilitoa ofa ya wasanii wote walioingia Top 5 kurekodi nyimbo kwenye studio yangu (MJ Production) ili kuonesha mwanga ili Watanzania waone kwamba kumbe inawezekana Staa wa BSS akawa mfanyabiashara mzuri wa muziki nchini.

“Hilo tumeliangalia kwa mapana na mikakati ya BSS mwaka huu ni pamoja na kutafuta watu watakaowaandikia nyimbo washindi na kuwachagulia ala, kwahiyo baada ya shindano wataingia studio na kufyatua mawe yenye akili.”

Monday, March 29, 2010

MKUU WA MKOA WA TANGA SAIDI SAIDI KALEMBO AWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA ZAHANATI MPYA WILAYANI PANGANI

Mh mkuu wa mkoa wa Tanga meja jenerali mstaafu Saidi Saidi Kalembo akiweka jiwe la msingi kwenye jengo jipya la zahanati lililojengwa katika kijiji cha Kwa Kibuyu kata ya Kipumbwi wilayani Pangani hivi karibuni alipokuwa ziarani.

Mkuu wa mkoa akiwa katika uso wa tabasamu wakati akimalizia kuweka jiwe la msingi. Zahanati hiyo mpya imejengwa na kampuni ya upandaji miti ya Tanga Forest.

Mkuu wa mkoa akiwaeleza jambo wananchi wa kijiji cha Kwa Kibuyu punde tu baada ya kufungua zahanati hiyo.

Mapokezi yalikuwa mazuri, akina mama wakimpokea mkuu wa mkoa wa Tanga Saidi Saidi Kalembo.

Akiwa katika msafara huku akiongozwa na mwenyeji wake.

Mwenyeji wa mkuu wa mkoa Bi Zipora Pangani ambaye ni mkuu wa wilaya ya Pangani akimtambulisha mheshimiwa Kalembo kwa wananchi wa Kwa Kibuyu.

Mfanyakazi wa Tanga Forest Bi Anitha Ngailo akimpa mkono mkuu wa mkoa baada ya kumsomea risala muhimu juu ya zahanati mpya ambayo kampuni yake imejenga.

Bi Anitha akisoma risala kwa mkuu wa mkoa.

Wananchi wa Kwa Kibuyu wakiwa makini huku mkuu wa mkoa akisikiliza risala iliyoandaliwa na Tanga Forest.

MITINDO INAVYOZIDI KUSHAMIRI JIJINI TANGA




Je umependa mavazi....?

Masai Style
Khanga Style
Kitenge Style
Batiki Style
Kikoi Style
Vikapu Style

Wasiliana nao, Wapo Tanga Tanzania.

Contact:

E-mail: aish_tz2000@yahoo.com
Phone: +255713510530


MISOSI NAE ATAJWA TUZO ZA KILI!

Baada ya msanii Roma kutokea Tanga kutajwa kwenye tuzo za Teen Extra za Clouds Fm. Mkoa wa Tanga umezidi kujidhihirishia kuwa upo juu katika anga za muziki baada ya msanii mwengine kutokea hapa kutajwa kwenye tuzo za Kili kwa mwaka huu.

Msanii huyo ni Bwana Misosi ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wake wa Mungu Yupo Busy ambapo hivi karibuni aliibuka na video kali ya wimbo huo. Misosi ametajwa katika kipengele cha kuwania tuzo bora ya wimbo wa Ragga kupitia wimbo wake huo wa Mungu Yupo Bize ambapo anachuana na wasanii wengine kama Dully Sykes (Shikide), Drezzy Chief (Wasanii) pamoja na Benjamin wa Mambo Jambo (Fly).

Kama wewe ni mdau wa muziki wa Bongo Flava kutokea Tanga, hakikisha Bwana Misosi anachukua tuzo hiyo ili watanga wote tupate cha kujivunia. Pia endelea kumpigia kura msanii Roma kupitia http://www.nipe5.com au bonyeza hapa kupiga kura kwa Roma.

Friday, March 26, 2010

UNAPENDA MOVIES ZA UKWELI..? ITAFUTE HII

TUSIKIMBIE VIKAO VYA BASATA- AFANDE SELE

Mfalme pekee wa mashairi ndani ya Bongo Flava, Seleman Msindi a.k.a Afande Sele amechana ujumbe maalum kwa artists wa field hiyo kuacha tabia ya kusepa vikao vya kujadili mwenendo wa game vinavyoendelea hivi sasa ambavyo kwa kiasi kikubwa vimekuwa vikijadili kuhusu umoja wa wasanii.

Msindi alisema hayo last Weekend muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao cha kujadili muziki huo ambacho kilihudhuriwa na nyota kiduchu.

“Jamaa wanatakiwa wafahamu kwamba hivi vikao vina umuhimu, hakuna wa kutusaidia kudai haki zetu kama sisi wenyewe tutashindwa kuwa na umoja... Nawasihi sana washkaji wasisepe, waje tuweke mikakati,” alisema Afande ambaye anapenda kuitwa Baba Tunda.

Members wa chama hilo, ambao tayari wameshajisajili BASATA ikiwa ni pamoja na kulipa ada hukutana kila wakati kujadili mambo mbalimbali ya muziki huo, lakini wasanii upcoming wamekuwa wakitia timu kwa wingi, huku masupastaa wakikacha kiaina.

'TUNAMTAKA NACY SUMARI MWENGINE'- MWANSOKO

Mkurugenzi wa Maendeleo na Utamaduni toka Wizara ya Habari na Utamaduni Bwana Herman Mwansoko amesema ni wakati sasa wa Tanzania kuinuka na kufanya vyema kwenye mashindano ya urembo ya Dunia.

Akiongea na Wakala wa Miss Tanzania toka Mikoa yote 20 ya Tanzania,Bwana Mwansoko alisema ya kuwa Watanzania wamechoka kuwakilisha kila mwaka na sasa ni wakati wao wa kwenda kushindana.

Mwansoko aliitaka kamati hiyo kufanya kama ilivyokuwa miaka iliyopota pale mrembo toka Tanzania Nancy Sumari alipofanya vizuri kwa kuipeperusha juu bendera ya Tanzania kwa kutwaa taji la Mrembo bora wa Afrika.

“Serikali pamoja na jamii ya Watanzania wanatamani mno kuona washiriki wa Tanzania kwenye shindano la Dunia wanafanya vizuri na jambo hilo linawezekana endapo tu mawakala watatafuta washiriki wenye sifa na ubora wa uhakika ambao watachuana kumpata Miss Tanzania.” alisema Mwansoko.

MAJINA YA WANAOWANIA TUZO ZA KILI

Wanaowania tuzo ya Mwimbaji bora wa kike.

Lady Jaydee
Mwasiti Almasi
Maunda Zorro
Vumilia Mwaipopo
Khadija Yusuph

wanaowania tunzo ya Mwimbaji bora wa kiume.
Marlow
Banana Zorro
Mzee Yusuph
Alikiba
Christian Bella

Wanaowania Albamu Bora ya Taarab

Jahazi Modern Taarab (Daktari wa Mapenzi),
5 Stars Modern Taarab (Riziki Mwanzo wa Chuki),
Coast Modern Taarab (Kukupenda Isiwe Tabu),
New Zanzibar Star (Powa Mpenzi)
East African Melody (Kila Mtu Kivyakevyake).

Tunzo ya Wimbo Bora wa Taarab inawaniwa na

Daktari wa Mapenzi’ na ‘Roho Mbaya Haijengi’ (zote Jahazi Modern Taarab), ‘Wapambe Msitujadili’, ‘Riziki Mwanzo wa Chuki’ (zote 5 Stars Modern Taarab) na ‘Kukupenda Isiwe Tabu’ (Coast Modern Taarab).

Tunzo ya Wimbo Bora wa Mwaka inawaniwa na

Marlow ‘Pii Pii-Missing my Baby
Diamond (Kamwambie)
Banana Zorro (Zoba)
Hussein Machozi (Kwa Ajili Yako).

Tunzo ya Wimbo Bora wa Kiswahili kwa upande wa bendi ni

Machozi Band (Nilizama),
African Stars Band-Twanga Pepeta (Mwana Dar es Salaam),
Top Band (Asha),
FM Academia (Vuta Nikuvute)
Extra Bongo (Mjini Mipango).

Tunzo ya Albamu Bora ya Bendi inawaniwa na

African Stars Band ‘Twanga Pepeta’ (Mwana Dar es Salaam),
Kalunde Band (Hilda)
Msondo Ngoma Music Band (Huna Shukrani).

Kwa upande wa Tunzo ya Wimbo Bora wa R&B, wanaoiwania ni

Belle 9 ‘Masogange’,
Diamond (Kamwambie),
AT na Stara Thomas (Nipigie),
Maunda Zorro (Mapenzi ya Wawili)
Steve (Sogea Karibu).

Tunzo ya Wimbo Bora wa Asili ya Kitanzania unawaniwa na

Mrisho Mpoto (Nikipata Nauli),
Machozi Band (Mtarimbo),
Offside Trick (Samaki),
Wahapahapa Band (Chei Chei)
Omari Omari (Kupata Majaaliwa).

Wanaowania Tunzo ya Wimbo Bora wa Hip Hop ni

Joh Makini (Stimu Zimelipiwa),
Quick Racka (Bullet),
Chid Benzi (Pom Pom Pisha),
Mangwea (CNN) na Fid Q (Iam a Professional).

Tunzo ya Wimbo Bora wa Reggae inawaniwa na

Hemedi (Alcohol),
Dabo Ft. Mwasiti (Don’t Let Go),
Man Snepa (Barua)
Matonya Ft. Christian Bella (Umoja ni Nguvu).

Kwa upande wa Tunzo ya Wimbo Bora wa Ragga, wanaoiwania ni

Dully Sykes (Shikide),
Bwana Misosi (Mungu yuko Bize),
Drezzy Chief (Wasanii)
Benjamin wa Mambo Jambo (Fly)

Tunzo ya Rappa Bora wa Mwaka inawaniwa na

Chokoraa,
Ferguson,
Kitokololo,
Totoo ze Bingwa
Diouf.

Tunzo ya Msanii Bora wa Hip Hop ni
Joh Makini
Fid Q
Chid Benz
Mangwea
Profesa Jay.

Tunzo ya Wimbo Bora wa Afrika Mashariki inawaniwa na

Blue 3 Ft. Radio and Weasal -Good Life ‘Where you are’,
Kidumu Ft. Juliana (Haturudi Nyuma),
Cindy (Na Wewe),
Radio and Weasal - Good Life (Bread and Butter)
Kidumu akitupa karata na wimbo ‘Umenikosea’.

Tunzo ya Mtunzi Bora wa Nyimbo ni

Mzee Yusuph
Mrisho Mpoto
Lady Laydee
Banana Zorro
Mzee Abuu, Fid Q

Tunzo ya Watayarishaji Bora wa Muziki
Lamar
Marco Chali
Hermy B
Allan Mapig0
Man Water

Video Bora ya Muziki wa Mwaka inawaniwa na

Lady Jaydee (Natamani kuwa Malaika)
Diamond (Kamwambie),
AY (Leo)
Banana Zorro (Zoba)
C Pwaa (Problem).

Tunzo ya Wimbo Bora wa Afro Pop inawaniwa na

Banana Zorro (Zoba)
Alikiba (Msiniseme)
Marlow (Pii Pii Missing My Baby)
Mataluma (Mama Mubaya)
Chegge (Karibuni Kiumeni)

Tunzo ya Msanii Bora Anayechipukia

Belle 9
Diamond
Barnaba
Quick Racka
Amini

Tunzo ya Wimbo Bora wa Kushirikiana inawaniwa na

AT - Stara Thomas (Nipigie)
Mangwea Ft. Fid Q (CNN)
Barnabas Ft. Pipi (Njia Panda)
Mwana FA Ft. Profesa Jay na Sugu (Nazeeka Sasa)
Hussein Machozi Ft. Joh Makini (Utaipenda).

Wednesday, March 24, 2010

MAADHIMISHO YA SIKU YA KIFUA KIKUU YALIVYOFANYIKA PANGANI KIMKOA!

Mh. Mkuu wa mkoa wa Tanga Major General (Retired) Saidi Saidi Kalembo akifungua maadhimisho ya siku ya kifua kikuu duniani ambapo katika mkoa wa Tanga yalifanyika wilayani Pangani siku ya jana. Kauli mbiu ilikuwa ni TUTUMIE MBINU MPYA KUONGEZA KASI YA MAPAMBANO DHIDI YA KIFUA KIKUU.

Mkuu wa mkoa akikaribishwa na mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Zipora Pangani.

Mkuu wa mkoa Saidi Saidi Kalembo akiwa anatoka jukwaani mara baada ya kutoa hotuba.

Mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Zipora Pangani akisema neno kabla ya kumkaribisha mkuu wa mkoa.
Viti vikipangwa vyema kwa ajili ya wageni waalikwa.

Kazi ikaanza kama hivi. Hao ni wapiga ngoma wa kikundi cha Atomic kutokea wilaya ya Pangani kata ya Bushiri, wakitoa burudani.

Kisha wakaingia wacheza ngoma. Ngoma za asili ndio zilikuwa kitovu cha burudani. Atomic Group wakisakata ngoma.

Bi Zipora ambaye ni mkuu wa wilaya, alishindwa kuvumilia. Akaingia kutunza.

Hapa ilikuwa juu kwa juu.
Wakatoka, nikajua kazi imeisha. Kumbe walikwenda kuchukua vibatari vya moto. Tazama mambo hayo- huyo dada wa mbele alitia fora!

Kiongozi wa ngoma hiyo ya asili akiongoza jahazi. Shamrashamra hizi zilifanyika kwenye uwanja mkuu wa stendi ya mabasi yaendayo Tanga.

Mkuu wa mkoa akisema jambo.

Mkuu wa mkoa na wenyeji wake.

Wa kwanza ni mbunge wa Pangani Mh Rished, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa, mwenyekiti wa CCM wilaya ya Pangani pamoja na katibu wake kule mwisho.

Mh Rished mbunge wa Pangani.
Wananchi walijitokeza kuja kusikiliza ujumbe wa siku ya kifua kikuu duniani.

Shaabani Kizamba ambaye alikiwa Mc pamoja na kiongozi wake Bwana Semnangwa, ambaye ni afisa utamaduni wa wilaya ya Pangani.

Kizamba akiwajibika wakati shughuli zikiendelea.

Wanachini wajaribu kukwepa camera ya VIJIMAMBO VYA TANGA , haya tena jamani.

Tuesday, March 23, 2010

MASOMO YAMPUMZISHA KEISHA JUKWAANI!

Hofu ya kudunda (kufanya vibaya) kwenye pepa yake ya kidato cha sita imemfanya msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini na mwanachama wa Tip Top Connection, Khadija Shaban ‘Keysha’ kuweka kando kidogo masuala ya muziki.

Msanii huyo bora wa kike katika tuzo za muziki za Kili, ni mwanafunzi wa Shule ya kimataifa ya Cambridge, akichukua masomo ya Historia, Jiografia na Lugha (HGL), anatarajiwa kufanya mtihani wake wa mwisho Juni mwaka huu.

Akilonga kwa njia ya simu katika kuhusiana na kutoonekana kwake kwenye majukwaa ya muziki, Keysha alisema kunatokana na kutingwa na masomo na hasa ikizingatiwa amebakiza miezi michache kabla ya kufanya mitihani yake ya mwisho.


“Nimetingwa sana na masuala ya kitabu, hivyo imenibidi niweke muziki pembeni, si unajua mshika mawili...hivyo mashabiki wangu wasihofu, nitakapomaliza mitihani nitaingia jukwaani kama kawaida,” alisema.

Keysha ambaye amejipatia umaarufu mkubwa tangu ajitose kwenye ulingo wa muziki wa kizazi kipya, ambako nyimbo alizotoa zimeweza kufanya vizuri, huku tayari akiwa ameishatoa albamu mbili, ‘Usinitenge’ na ‘Keysha’.

MIKOANI TUNAVYOKUJA KASI KWENYE ANGA ZA BLOG!

Tazama blog ya Mtwara na ujue mambo yote yanayotokea mkoani humo. http://www.mtwaraleo.blogspot.com/ au bonyeza hapa kutembelea blog hiyo.

Monday, March 22, 2010

KIVUKO KIPYA CHA PANGANI LEO MCHANA WAKATI KINAPIGA 'MISELE'

Nilisikia kinafunguliwa mwezi huu wa tatu jamani.
Tunakisubiri kwa hamu.