BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, July 28, 2011

VIJANA WA TANGA TOWN!

Msanii mashuhuri wa muziki wa Bongo Flava kutokea Tanga Dk Leader aliyevaa fulana nyeupe akiwa na washkaji zake. Katikati ni The Don pamoja na Producer wa Huruma Records ya jijini Tanga anafahamika kama Andrew.



Hapa ni maeneo ya Chumbageni wakati camera ya Anko Mo ilipowakuta wakibadilishana mawazo.

CLUB LACASA CHICA NI BURUDANI MWANZO MWISHO JIJINI TANGA!









WHITE PARTY



Wednesday, July 27, 2011

ALBINO KUPANDA MLIMA KILIMANJARO

KATIKA kukabiliana na dhana potofu iliyojengeka katika jamii dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwamba hawana uwezo sawa na wengine, Josephat Torner ameamua kuvunja ukimya kwa kupanda Mlima Kilimanjaro.

Anatarajia kuanza safari yake hiyo itakayomchukua siku nane, Jumamosi wiki hii kuelekea kileleni kwa lengo la kuithibitishia jamii ambayo bado inaendeleza vitendo vya ukatili na unyanyapaa dhidi ya albino kwamba wao wanaweza kufanya kila kitu.

Torner ametoa kauli hiyo kwenye mkutano na waandishi wa habari na kusema lengo pamoja na kufikisha ujumbe huo muhimu ni kuwa albino wa kwanza Tanzania kufanya kitendo hicho cha kishujaa cha kufika kwenye kilele cha Kilimanjaro, mlima mrefu barani Afrika.

“Nipo mbele yenu hapa leo kuweka msimamo dhidi ya mawazo potofu yaliyopo katika fikra za baadhi ya Watanzania na Waafrika wengi ambao wanaamini kwamba albino hana uwezo sawa na watu wengine, fikra hizi ni hatari zimeendelea kusababisha ubaguzi, kutengwa, ukatili na mauaji dhidi yetu kwa muda sasa,” amesema.

“Jumamosi ya Julai 30, mwaka huu, nitaanza safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro lengo kuu ni kufikisha haki za albino kileleni mwa Afrika na kutangaza kwa sauti kubwa niwezavyo kwamba albino sio mtu wa kuogopwa, kubaguliwa, anayestahili kuwindwa kama mnyama wa porini akikatwa vipande kwa ajili ya biashara, bali ni binadamu kama wengine.”

Torner amebainisha kuwa, uamuzi wake huo umetokana na kasi ya vitendo vya ukatili na mashambulizi yanayoendelezwa na baadhi ya Waafrika kutokana na imani za kishirikina zilizochochea biashara ya viungo vya albino na kusababisha madhara mengi kwao hasa kulazimishwa kuishi kwa wasiwasi.

“Nitakapopanda mlima nitapanda kwa ajili ya albino wote waliolazimishwa kuondoka nyumbani kwao kwenda kuishi kwenye kambi maalumu zinazowatenga na familia zao na kuwapa upweke na kuwaambia iwe mwisho wa kujificha kwenye kivuli cha jua tena, ndoto yangu ni kuunganisha albino wote ili tuuthibitishie ulimwengu tuna uwezo sawa na binadamu wengine ila tunatofautishwa na mahitaji,” amesema.

Takriban miaka mitano sasa, hali ya albino nchini imekuwa si shwari kutokana na kasi ya ushambuliaji, uwindaji na mauaji ya kikatili yaliyosababisha vifo zaidi ya 60, huku Serikali ikilazimika kuhamisha wanawake na watoto 118 katika shule maalumu ili kuimarisha ulinzi na usalama wa maisha yao dhidi ya wawindaji.


Na Anna Makange, Tanga.

Monday, July 25, 2011

PROFESSOR JAY AND DITTO MEET WITH STUDNETS IN TANGA USING PERFORMANCE TO FIGHT MALARIA

On the 21stof July, students from ten schools came together at Usagara Secondary School in Tanga town to take part in malaria themed song, theatre and poetry competitions. The competition was a part of the Zinduka! club initiative, in which youth are empowered with the knowledge and tools to drive forward the fight against malaria in local communities.

The judges were treated to a spectacle of talent as they witnessed an array of performances including poetry readings, songs and even theatrical performances
On reaching the final round, Tanzanian artist, Ditto, took to the stage to talk to the students about how important it is to protect themselves from malaria to ensure they secure their future, before the artist sang the malaria he had written for the Zinduka! campaign which has now become an anthem for a generation fighting against malaria.
The students were then surprised when another guest Bongo fleva rapper and Zinduka! goodwill ambassador Professor Jay joined Ditto on stage to sing the anthem.

The artist has been a prominent figure in the fight against malaria, featuring in the launch of the Zinduka! campaign in 2010 and making regular appearances for the campaign in the field and on TV.Professor Jay then took time to hand out awards to the lucky competition winners.

Professor J had this to say, “I joined the Zinduka! campaign with the hope that through my music I could help to fight malaria in Tanzania. But to see kids wanting to get involved and using music as the platform to fight malaria in their communities, that’s what makes me most proud of the work we have done.
Professor Jay and Ditto then invited youth to join him as he visited a number of houses near Tanga town, where the youth spoke to households about what measures they use to protect themselves from malaria and what they think needs to be done to eradicate malaria in Tanzania.

The Malaria Haikubaliki Campaign is led by the Tanzanian Government behind the leadership of President JakayaKikwete. It is supported by partners including Malaria No More, Tanzania House of Talent (THT), Johns Hopkins University, Population Services International and United Against Malaria. The goal of the program is to achieve universal bed net coverage and eliminate malaria deaths by urging all Tanzanians to Zinduka! (“Wake up!”) to the threat of malaria and protect themselves against the disease

SERENGETI FIESTA 2011 NI FULL MAJOTROOOOO


Wananchi wa Tanga wakifurahia Serengeti Fiesta 2011 iliyofanyika jijini Tanga siku ya jana Jumapili ya tarehe 24/07/2011 kwenye uwanja wa Mkwakwani......hakika ilikuwa bonge moja la show! wakazi wa Tanga walijitokeza wka wingi na majatrooo yaliwabamba vilivyo.



Dayna akifanya vitu vyake jukaani

Mimi pamoja na mashosto wa kitanga


Mataaluma akitoa burudani



Sheta akionyesha umahiri wake wa kucheza



Mwana Fa akiangusha burudani.



Dj Bulla ndio alikuwepo kwenye moja na mbili



Belle ( kwa stage akitoa majotroooo


Mzee wa dushelele Ali Kiba kama kawa akiwakilisha



Thursday, July 21, 2011

HATIMAE JAIRO KIBARUA KIMEOTA NYASI!

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, amesimamishwa kazi rasmi kufuatia kutangazwa rasmi habari hizo na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemo Luhanjo wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma.

Kutimuliwa kazi kwa Jairo kumekuja baada ya Beatrice Shelukindo mbunge wa Kilindi Mkoani Tanga kulipua bomu Bungeni akimtuhumu Katibu Mkuu huyo wa zamani wa Wizara ya Nishati na Madini juu ya kutumia zaidi ya Sh 1 bilioni kwa ajili ya kutoa rushwa kwa watu mbalimbali ili bajeti ya wizara hiyo iweze kupitishwa na Bunge.

Wednesday, July 20, 2011

HAWA NAO WATAKUWEPO KWENYE SERENGETI FIESTA 2011 PALE MKWAKWANI SIKU YA JUMAPILI

Msanii wa hip hop anafahamika kama Godzila, ni miongoni mwa wasanii watakaokuwepo siku ya jumapili ya tarehe 24 mwezi 7 pale Mkwakwani katika Serengeti Fiesta 2011.

Anaitwa Mataaluma wakazi wa Tanga wanaisubiri mama mubaya kwa hamu ndani ya Serengeti Fiesta 2011 Mkwakwani siku ya Jumapili.

Linex karibu sana Tanga.

Joh Makini atapiga show mwanzo mwisho.

Belle 9 kutoka Moro mpaka Tanga ndaani ya uwanja wa Mkwakwani siku ya Jumapili.

Bob Junior raisi wa Masharobaro kama kawa ndani ya Mkwakwani kwenye Fiesta.

Prof Jay. Msanii mkongwe kwenye Bongo Flava nae atakuwepo Tanga kwenye Serengeti Fiesta 2011 Mkwakwani.

Linah kutoka THT nae atakuwepo kuwakilisha Fiesta.

Ali Kiba pia atakuwepo kwenye Serengeti Fiesta 2011 kwenye uwanja wa Mkwakwani.

Anaitwa Top C ni msanii wa Bongo Flava anayefanya vizuri hivi sasa. Nae atakuwepo siku ya jumapili. Top C asili yake ni mkoani Tanga, hivyo wakazi wa Tanga kaeni tayari kumpokea.

SHELUKINDO ALIVYOFUNGUKA BUNGENI!

Beatrice Shellukindo

Beatrice Shellukindo amelipua bomu Bungeni akimtuhumu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, kwa kutumia zaidi ya Sh 1 bilioni kwa ajili ya kutoa rushwa kwa watu mbalimbali ili bajeti ya wizara hiyo iweze kupitishwa na Bunge.

Tuhuma hizo nzito zinakuja kipindi ambacho tayari Wabunge wa Kamati ya Nishati na Madini wakiwa wameibua tuhuma kama hizo za baadhi ya wajumbe kutaka kuhongwa na maofisa wa wizara hiyo, ili kurahisisha upitishaji wa bajeti ndani ya kamati.

David Jairo

Takriban wiki tatu tangu wabunge wa kamati hiyo kuibua tuhuma hizo ambazo zilifika hadi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, hivi juzi tena Shellukindo alikoleza moto huo wakati akichangia bajeti ya wizara.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikubaliana na tuhuma hizo. Akitoa hoja ya kuondoa bungeni hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini, Pinda alisema alikuwa akisubiri Rais Jakaya Kikwete afike Afrika ya Kusini alikokwenda katika ziara ya kiserikali ili aweze "kumshtaki" Katibu Mkuu huyo kutokana na tuhuma zilizotolewa dhidi yake. Pinda alisema hawezi kuchukua hatua dhidi ya Jairo kwani kwa mujibu wa sheria, mamlaka ya uteuzi ndiyo inayoweza kuchukulia hatua dhidi yake.

Beatrice Shelukindo ni mbunge wa jimbo la Kilindi mkoani Tanga kupitia chama cha mapinduzi.

Tuesday, July 19, 2011

SERENGETI FIESTA 2011 INAKUJA TANGA JUMAPILI YA TAREHE 24/07/2011

Roma ni mmoja kati ya wasanii wa Hip Hop wanaotokea Tanga ambaye atakuwepo kwenye Fiesta kuuwakilisha mkoa wa wake. Kupitia Anko Mo BlogSpot utapata kuwajua wasanii wote watakaopanda kwenye Serengeti Fiesta 2011 kunako uwanja wa Mkwakwani. Tunaanza na wasanii wanaotokea Tanga.

Mwana Fa ambaye asili yake ni kule wilayani Muheza. Pia atakuwepo siku ya jumapili kwenye uwanja wa Mkwakwani na atapiga show mwanzo mwisho. Wasanii wengine watakaopanda siku hiyo utawapata kuwaona hivi punde. Endelea kutembelea Blog.

KIJANA AANGUKA NA KUPOTEZA FAHAMU AKIJARIBU KUKWEPA NYAYA ZA UMEME

Kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja, alianguka na kupoteza fahamu katika eneo la Gofu hapa jijini Tanga karibu kabisa na ofisi za mkuu wa mkoa. Kwa mujibu wa wapita njia wengine waliomuona wakati anaanguka, walidai kuwa kijana huyo alikuwa akijaribu kukwepa nyaya za umeme zilizokuwa zimeanguka barabarani. Tukio hilo lilitokea siku ya jana majira ya saa mbili asubuhi.

Wasamaria wema wakimtazama kijana aliyeanguka huku wakijadili namna ya kumsaidia.

Mzee huyu alijitoa mhanga kwa kuzitoa nyaya za umeme zilizoanguka barabarani na kufanya kijana huyo kuanguka na kupoteza fahamu. Mpaka naondoka eneo la tukio, kijana huyo aliweza kupata msaada na kupelekwa hospitali ya Bombo.

Monday, July 18, 2011

TIMU YA DALADALA ILIVYOFANYA KAZI YA KUREKODI VIPINDI MKOANI TANGA

Tayari timu nzima ya kipindi cha daladala kimeshafanya baadhi ya vipindi mkoani Tanga, ambapo vipindi hivyo utakuja kuviona kwa luninga yako kupitia televisheni ya ITV kila siku kuanzia saa kumi na mbili na nusu mpaka saa moja jioni.

Maswala mbali mbali kuhusiana na mgao wa umeme, maendeleo ya bandari ya Tanga- wananchi wanaionaje. Swala la elimu na mmomonyoko wa maadili pia vimezungumziwa katika moja ya vipindi vilivyorekodiwa na timu ya daladala iliyotua jijini Tanga.

(Pichani mimi na Daniel Kijo, mtangazaji wa kipindi cha daladala)

Nikiwa mmoja wa watu walioshiriki kutoa maoni mbalimbali katika kipindi cha daladala, kwa kweli katika mijadala yote niliyoishuhudia wakati wa kurekodi vipindi- wananchi wa mkoa wa Tanga wameonyesha ushirikiano wa kutosha na wengi wamezungumza kwa hisia kwa kile ambacho kilikuwa kinawagusa moja kwa moja.

(Pichani Daniel akiwa na mdau wa kipindi cha daladala, barabara ya nane)

Safari ilianzia Mwahako mpaka eneo la stendi ambapo walipanda abiria wengine na mjadala kuendelea. Badae tena daladala ilikwenda eneo la Magomeni na kisha wanafunzi wa chuo kikuu cha Tanga cha Eckenford nao walipata nafasi ya kutoa maoni yao pia kuhusiana na swla zima la elimu huku bwana Kombo ambaye ni afisa wa elimu ya sekondari wilaya ya Mkinga akiwa chachu ya mada hiyo.

(Timu ya kipindi cha daladala wakiwa na afisa elimu Kombo wakati wa kuelekea kurekodi)

wananchi wa Tanga wakae mkao wa kula kutazama vipindi vilivyotengenezwa kutokea hapa Tanga kuanzia leo tarehe 19 siku ya jumanne kuanzia saa kumi na mbili na nusu mpaka saa moja kujua mengi kuhusiana na mkoa wa Tanga.

(Daniel kwenye bustani za Tanga)

Eldad Mark Film Director akiwa na Deogratius Sizya Camera man wa kipindi cha Daladala pamoja na afisa wa elimu za sekondari wilaya ya Mkinga Bwana Kombo wakijiandaa na mahojiano.

Kipindi cha daladala pia kilikutana na rais wa Eckenford Tanga University bwana Amos Fide na kufanya nae mahojiano. Pichani ni Daniel Kijo, Eldad Mark pamoja na Fide.

Vijana wa Kazi.

Mimi nikiwa na Bibi Kiroboto. Bibi mcheshi huyu sijapata kuona. Hapa tukiwa Tanga Televisheni kwa ajili ya mahojiano na kuwapa taarifa wananchi wa Tanga juu ya ujio wa daladala. Ukiiona tu, unakimbilia na kupata kisha ukifika ndani unatoa maoni yako!! Daladalaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!

Daladala ni kila kona bwana! Hapa ni katika kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh. Bibi kiroboto akiwa na dereva wa daladala bwana Emanuel Zing pamoja mwenyeji wetu bi Winfrida Magawa aliyesimama.

Daniel Kijo akibadilishana contacts na baadhi ya wakuu wa kiwanda cha Tanga Fresh

Mazungumzo ya hapa na pale pia yalikuwepo tulipofika Tanga Fresh.

Daladalaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!

Kwa mbali daladala ikionekana na jengo kubwa la kiwanda cha Tanga Fresh

Tulifika pia Eckenford Tanga University.

Huyu mama alitupa raha sana! Alistaajabu alipomuona bibi Kiroboto. wacha amkumbatie bwana! Raha kuwa na daladala!

Baadhi ya wanafunzin wa Eckenford Tanga Univertisty wakibadilishana mawazo za timu ya daladala.

Wanafunzi wa chuo kikuu cha Eckenford Tanga

Wanafunzi wakiingia kwenye daladala

(Timu nzima ya Daladala iliyokuwepo jijini Tanga ni pamoja na Dani Kijo na Bi Kiroboto ambao ni watangazaji. Wengine ni Eldad Mark Film Director, Emanuel Zing Driver, Deogratius Sizya Camera man, Tanya creative producer, Anton second driver na Steve Martin researcher.)