BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, October 26, 2011

WHITE BEACH PARTY NDANI YA RASKAZONE TANGA!!!!


Sio ya kukosa

SEKONDARI YA SHEMSANGA YAUNGUA TENA MOTO, SAFARI HII CHANZO CHAKE NI HITILAFU YA UMEME

Shule Ya Shemsanga Inayomilikiwa Na Jumuiya Ya Wazazi Wa Ccm Iliyopo Wilayani Korogwe Imeungua Moto Na Kusababisha Hasara Inayokadiriwa Kufikia Kiasi Cha Shilingi Milioni 10

Mkuu Wa Shule Ya Shemsangaga Bw. Paschal Deogradius Akiangalia Huku Haamini Moja Ya Chumba Ambacho Kilikuwa Ni Bweni La Kulala La Wanafunzi Hao.

Moja Ya Bweni Ambalo Limeteketea Kabisa Katika Shule Hiyo.


Thursday, October 13, 2011

JULIO NA MAZOEZI KABAMBE YA COASTAL UNION, LENGO NI KUINASUA MKIANI

Kocha Jamhuri Kihwelo 'Jullio' Akiweka Koni Ikiwa Ni Siku Yake Ya Kwanza Kuinoa Timu Yake Mpya Ya Coastal Union Kwenye Uwanja Wa Gymkhana Ambako Timu Hiyo Inachukua Mazoezi.

Wachezaji Wa Timu Ya Coastal Union Wakiw Ana Kocha Wao Jamhuri Kihwelo 'Julio' Wakifanya Mazoezi Kwenye Uwanja Wa Gymkhana Jijini Tanga Ambako Timu Hiyo Inafanya Mazoezi.


WAFUKIWA NA KIFUSI WAKITAFUTA RUPIA WALIKUWA WAKICHIMBA CHOO NDANI, MMOJA AFA PAPO HAPO

Mama Zaina Ramadhani Ambaye Nyumba Yake Kwa Nyuma Aliwaita Watu Watatu Wamchimbie Choo Kwa Ndani (Nyumba Ya Makuti Inayoonekana Nyuma Ya Picha) Watu Hao Walipoanza Kuchimba Wakaeleza Kwamba Wameona Dalili Ya Kuwepo Kwa Rupia Za Kijerumani Hivyo Wakaendelea Kuchimba

Hadi Shimo Likafika Kwenye Nyumba Hii Ya Bati, Ambako Mtu Mmoja Anayeitwa Saleh Wazir Alifukiwa Na Kifusi Humo Ndani Na Kufa Wakati Mmoja Anayeitwa Simon Alifunikwa Lakini Bahati Yake Miguu Yake Ilifunikwa Akawahi Kutolewa Huku Mwenzao Mmja Anayeitwa Otborn Aliwahi Kukimbia Na Kuwaacha Wenzake.

Nyumba Ambayo Shimo Limetokeza Kwa Ndani Na Kuua Mtu Mmoja Huko Mnyuzi

KOROGWE WAZINDUA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA UHURU WA TANGANYIKA

Kaimu Mkuu Wa Wilaya Ya Korogwe Methew Nasei Akisaliana Na Wananchi Mara Alipowasili Kwenye Viwanja Vya Magoma Shuleni Kulikofanyika Maadhimisho Ya Uzinduzi Wa Sherehe Za Miaka 50 Ya Uhuru Wa Tanganyika Ambapo Kiwilaya Zilifanyika Magoma Na Kuhudhuriwa Na Watu Wengi

Amanda Wa Jwtz Akiwa Na Kikosi Chake Cha Mgambo Ambacho Kimeanza Mafunzo Katika Kijiji Hicho Cha Magoma Mara Nyini Wana-Mgambo Ni Jeshi La Akiba Ambapo Katika Sherehe Hizo Za Uzinduzi Walinogesha Sherehe Hizo Kwa Gwaride Lao Zuri.

Katibu Tawala Wa Wilaya Ya Korogwe (Kushoto) Akiwa Na Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Korogwe Mr. Masembejo Wakiangalia Ratiba Ya Sherehe Za Uzinduzi Wa Sherehe Za Miaka 50 Ya Uhuru Magoma.