BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, December 23, 2011

TAKUKURU FUATILIENI FEDHA ZINAZOTOLEWA NA SERIKALI HALMASHAURI-GALLAWA


MKUU wa mkoa wa Tanga, luteni (mstaafu) Chiku Gallawa, ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuongeza kasi ya kufuatilia fedha zinazopelekwa na serikali katika halmashauri nchini ili ziweze kutumika vizuri kwenye miradi mikubwa ysa maendeleo iliyokusudiwa.

Akifunga Mkutano Mkuu wa mwaka wa takukuru kwenye hoteli ya Tanga beach Resort kwa maofisa wa taaisis hiyo kutoka mikoa yote ya tanzania bara, Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa takukuru wamebeba dhamana kubwa ya kustawisha maendeleo kwa kufautilia watendaji kwenye halmasauri ambao wanatumia vibaya fedha zinazoolewa na serikali kwa ajili ya maendeleo.

Amesema serikali hasa ya awamu ya nne, imekuwa ikitoa fedha nyingi katika halmashauri kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maeneleo hasa ya elimu, afya, barabara na kujenga majengo mbalimbali lakini fedha hizo wakati mwingine zimekuwa zikitumika visivyo na hivyo kuleta malalamiko kutoka kwa wananchi.

Mkuu huyo wa mkoa pamoja na kuipongeza taasisi hiyo kwa kufanikiwa kuokoa fedha za serikali kiasi cha shilingi bilioni 97.5, lakini ameitaka takukuru kuhakikisha inaongeza kasi ya mapambano ya rushwa kwa kuwa kufanya hivyo kutasaidia mipango mbalimbali ya maendeleo ya nchi.

Kuhusu wananchi mkuu huyo wa mkoa amewataka kutoa ushirikiano kwa taaisis hiyo na waache kulalamikia masuala ya ufisadi wakati kama watatoa ushirikiano masula hayo yanaweza kudhibitiwa kwa watu kuogopa fedha za umma hatua ambayo mwelekeo wa taasisi hiyo inakoelekea na kwamba waongeze jitihada kutumia nyenzo walizokuwa nazo katika mapambano hayo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Dkt Edward Hosea alisema kuwa wataendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu suala la mapambano ya rushwa ikiwemo kuwafundisha watumishi wake kwenda sambamba na mabadiliko ya teklonojia katika masuala ya rushwa.


Sunday, November 20, 2011

MKUU WA MKOA WA TANGA ATEMBELEA MGODI WA KUZALISHA UMEME WA HALE, AKUTANA NA CHANGAMOTO

MKUU WA KITUO CHA KUZALISHA UMEME CHA NEW PANGANI FALLS POWER STATION INJINIA PAKAYA MTEMAKAYA AKIMSOMEA TAARIFA MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI (MSTAAFU) CHIKU GALLAWA ALIPOTEMBELEA KAIKA MGODI WA KUZALISHA UMEME ULIOPO HALE WILAYANI KOROGWE.

INJINIA PAKAYA MTEMAKAYA (ALIYENYOOSHA MKONO JUU) AKIMWELEZA MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI CHIKU GALLAWA (KUSHOTO) NAMNA UZALISHAJI UNAVYOFANYIKA KWENYE MGODI HUO WA KUZALISHA UMEME HALE.

INJINIA MUSIMU MAKUNGA MSIMAMIZI WA MGODI WA KUZALISHA UMEME WA PANGANI FALLS AKITOA MAELEKEZO WA JINSI WANAVYOWEZA KUENDESHA MITAMBO HIYO YA KUZALISHA UMEME KATIKA MAJUKUMU YAO YA KILA SIKU.

HAPA MKUU WA MKOA LUTENI CHIKU GALLAWA AKIWA NA MSAFARA WAKE WAKIANGALIA KINA CHA MAJI KATIKA BWAWA LILILOZUIWA KWA AJILI YA KUPELEKA MAJI KATIKA MGODI HUO


KAMATI YA BUNGE YA MIUNDOMBINU YATEMBELEA BARABARA YA TANGA/HOROHORO, BANDARI YA TANGA

KATIBU MKUU WA WIZARA YA MIUNDOMBINU INJINIA OMARI CHAMBO, AKITOA UFAFANUZI KWA WABUNGE WA KAMATI YA MIUNDOMBINU WALIOKUWA KWENYE MKUTANO KWENYE JENGO LA BANDARI HOUSE TANGA

WATENDAJI WA BANDARI YA TANGA WAKIFUATILIA KWA MAKINI MICHANGO YA WABUNGE WA KAMATI YA MIUNDOMBINU

KATIBU MKUU WA WIZARA YA MIUNDOMBINU INJINIA OMARI CHAMBO (KATIKATI) AKIELEZEA JAMBO KWA WABUNGE WA KAMATI YA MIUNDOMBINU WALIOTEMBELEA BANDARI YA TANGA KUPATA TAARIFA MBALIMBALI

MJUMBE WA KAMATI YA MIUNDOMBINU BW. HERBERT MNTANGI AMBAYE NI MBUNGE WA MUHEZA (BONDE) AKIWAELEKEZA WAJUMBE WENZAKE JINSI KISIWA KILICHOPO JIRANI NA BANDARI YA TANGA KINAVYOWEZA KUZIDISHA KUJAA KWA MCHANGA KATIKA BANDARI YA TANGA

Wednesday, October 26, 2011

WHITE BEACH PARTY NDANI YA RASKAZONE TANGA!!!!


Sio ya kukosa

SEKONDARI YA SHEMSANGA YAUNGUA TENA MOTO, SAFARI HII CHANZO CHAKE NI HITILAFU YA UMEME

Shule Ya Shemsanga Inayomilikiwa Na Jumuiya Ya Wazazi Wa Ccm Iliyopo Wilayani Korogwe Imeungua Moto Na Kusababisha Hasara Inayokadiriwa Kufikia Kiasi Cha Shilingi Milioni 10

Mkuu Wa Shule Ya Shemsangaga Bw. Paschal Deogradius Akiangalia Huku Haamini Moja Ya Chumba Ambacho Kilikuwa Ni Bweni La Kulala La Wanafunzi Hao.

Moja Ya Bweni Ambalo Limeteketea Kabisa Katika Shule Hiyo.


Thursday, October 13, 2011

JULIO NA MAZOEZI KABAMBE YA COASTAL UNION, LENGO NI KUINASUA MKIANI

Kocha Jamhuri Kihwelo 'Jullio' Akiweka Koni Ikiwa Ni Siku Yake Ya Kwanza Kuinoa Timu Yake Mpya Ya Coastal Union Kwenye Uwanja Wa Gymkhana Ambako Timu Hiyo Inachukua Mazoezi.

Wachezaji Wa Timu Ya Coastal Union Wakiw Ana Kocha Wao Jamhuri Kihwelo 'Julio' Wakifanya Mazoezi Kwenye Uwanja Wa Gymkhana Jijini Tanga Ambako Timu Hiyo Inafanya Mazoezi.


WAFUKIWA NA KIFUSI WAKITAFUTA RUPIA WALIKUWA WAKICHIMBA CHOO NDANI, MMOJA AFA PAPO HAPO

Mama Zaina Ramadhani Ambaye Nyumba Yake Kwa Nyuma Aliwaita Watu Watatu Wamchimbie Choo Kwa Ndani (Nyumba Ya Makuti Inayoonekana Nyuma Ya Picha) Watu Hao Walipoanza Kuchimba Wakaeleza Kwamba Wameona Dalili Ya Kuwepo Kwa Rupia Za Kijerumani Hivyo Wakaendelea Kuchimba

Hadi Shimo Likafika Kwenye Nyumba Hii Ya Bati, Ambako Mtu Mmoja Anayeitwa Saleh Wazir Alifukiwa Na Kifusi Humo Ndani Na Kufa Wakati Mmoja Anayeitwa Simon Alifunikwa Lakini Bahati Yake Miguu Yake Ilifunikwa Akawahi Kutolewa Huku Mwenzao Mmja Anayeitwa Otborn Aliwahi Kukimbia Na Kuwaacha Wenzake.

Nyumba Ambayo Shimo Limetokeza Kwa Ndani Na Kuua Mtu Mmoja Huko Mnyuzi

KOROGWE WAZINDUA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA UHURU WA TANGANYIKA

Kaimu Mkuu Wa Wilaya Ya Korogwe Methew Nasei Akisaliana Na Wananchi Mara Alipowasili Kwenye Viwanja Vya Magoma Shuleni Kulikofanyika Maadhimisho Ya Uzinduzi Wa Sherehe Za Miaka 50 Ya Uhuru Wa Tanganyika Ambapo Kiwilaya Zilifanyika Magoma Na Kuhudhuriwa Na Watu Wengi

Amanda Wa Jwtz Akiwa Na Kikosi Chake Cha Mgambo Ambacho Kimeanza Mafunzo Katika Kijiji Hicho Cha Magoma Mara Nyini Wana-Mgambo Ni Jeshi La Akiba Ambapo Katika Sherehe Hizo Za Uzinduzi Walinogesha Sherehe Hizo Kwa Gwaride Lao Zuri.

Katibu Tawala Wa Wilaya Ya Korogwe (Kushoto) Akiwa Na Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Korogwe Mr. Masembejo Wakiangalia Ratiba Ya Sherehe Za Uzinduzi Wa Sherehe Za Miaka 50 Ya Uhuru Magoma.

Saturday, September 24, 2011

HONGERENI CATHBERT KAJUNA NA DADA ESTER ULAYA KWA KUFUNGA PINGU ZA MAISHA

Cathbert Kajuna na dada Ester Ulaya hatimaye wamefunga pingu za maisha. Maharusi wote ni marafiki wa karibu wa Anko Mo Blogspot. Mungu awape neema na baraka katika maisha yenu ya ndoa.



Hapa wakionyesha vyeti vyao vya ndoa.

Kajuna najua hapa presha ilikuwa inapanda na kushuka. Hongera sana kaka.



Monday, September 19, 2011

SHILLINGI VIT CLASS USAFIRI PANGANI- TANGA MPAKA DAR

SHILLINGI VIP CLASS ni mabasi mapya kabisa ambayo yanafanya safari zake PANGANI-TANGA mpaka DAR kila siku kuanzia saa moja kamili asubuhi. Halafu DAR- TANGA mpaka PANGANI.



Unafika mpaka Pangani na kuina fukwe nzuri za kuvutia.


Wednesday, September 7, 2011

KISIMA CHA MAJI CHAZINDULIWA LUSHOTO

Na Oscar Assenga,Lushoto.
MRADI wa Kisima cha maji katika kituo cha Afya Kangangai uliofadhiliwa na kikundi cha urafiki wa ujerumani na Tanzania (Deustsch Tanzanischer freundeskreis DTF)umezinduliwa juzi wilayani Lushoto.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo,Daktari Mfawidhi wa kituo hicho,Bakari Mavura alisema mradi huo ulianza mwaka 2008 kutokana na kuwepo kwa tatizo la maji katika kata ya Mwangoi tarafa ya Mlalo ambapo waliamua kukaa chini na kuanza kubuni mradi huo wakishirikiana na kamati ya afya ya kituo hicho.Mavura alisema baada ya kubuni mradi huo waliweza kuishirikisha jamii na kuweza kupata marafiki wa kikundi cha wajerumani na walipotoa mawazo na uweza kuyafanyia kazi.


Katika mradi huo shilingi milioni 16.2 zimetumika kati ya hizo shilingi milioni kumi laki mbili zimepatikana kutoka kwa kikundi cha urafiki na halmashauri ya wilaya ya Lushoto imechangia shilingi milioni sita.


Mavura alielaza maji hayo yatakuwa ni kwajili ya kituo hicho pamoja na watumishi wanaofanya kazi ambapo zaidi ya watumishi 10 pamoja na wananchi 22,000 watanufaika mradi huo pamoja na wagonjwa ambao watakwenda kupata matibabu kwenye kituo hicho cha afya cha Kangagai. "Wananchi wanapaswa kukitunza vizuri kisima hicho ili kuweza kuondokana na tatizo la maji "alisema Mavura.


Aidha aliongeza kuwa wanatarajiwa kuishirikisha jamii katika utunzji wa kisima ili kiweze kuwa endelevu.Alieleza kuwa licha ya kukamilika kwa kisima hicho wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa shillingi Millioni moja na laki nane kwa ajili ya kumalizia ufungaji wa mfumo wa maji safi na maji taka kwenye majengo ya kituo chicho.Mwisho.

ZUBEDA SEIF MKALI WA KUIGIZA VODACOM MISS TANZANIA

Mrembo Zubeda Seif kutoka Tanga aliyejinyakulia kitita cha Dola 1000 akimnanga muingizaji nguli Jacquline Wolpa wakati wa kutafuta mrembo wa Vodacom Miss Tanzania aliye na kipaji cha uigizaji lililozaminiwa na Kampuni ya Papazi.

Monday, September 5, 2011

HOTELI MPYA YAZINDULIWA TANGA

MMILIKI wa hoteli mpya inayojulikana kwa jina la NYUMBANI Hotel & Restaurant Bw. Aloyce Kimaro aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro, amewataka wafanyabiashara na wananchi wa Jiji la Tanga, kumuunga mkono katika uwekezaji wake mpya wa sekta ya hoteli ili kusaidia kuongezeka kwa pato la uchumi la mkoa wa Tanga.

Akitoa neno la shukurani kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa hoteli hiyo iliyopo mkabala ya jengo la posta katikati ya Jiji la Tanga, mbunge huyo wa zamani alisema alipata wazo la kufungua hoeli hiyo mkoani Tanga, kushirikiana na wana-jamii kuongeza pato la mkoa hasa kutokanana uwepo wa bandari na shughuli nyingine za kiuchumi.

Alisema kutokana na uwepo wa bandari na kukua kwa shughuli nyingi za kibiashara alionelea kufungua hoteli hiyo hivyo amewataka wananchi na wafanyabiashara kushirikiana naye kumsapoti katika kuhakikisha hoteli hiyo inatoa huduma za kisasa na za kimaaifa.

Bw. Kimaro ambaye anaendesha hoteli hiyo akiwa na wakurugenzi wengine Bw. John Kessy na Mansfeld, wanatarajia kufungua hoteli zenye jina hilo katika mikoa yote nchini ili kuhakikisha wanawekeza katika sekta hiyo wakiwa kama Watazania na kusaidia kukua kwa uchumi wa Tanzania. Hoteli hiyo ya Tanga inafuatia kuwepo kwa hoteli nyingne zenye jina hilo la nyumbani katika miji ya Mwanza na Moshi.

Akizindua hoteli hiyo Waziri wa Uchukuzi, Injinia Omar Nundu ambaye ni mbunge wa jimbo la Tanga, alisema katika kutembea kwake Ulaya hoteli hiyo inaingana kabisa na ambazo amezishuhudia na kwamba hoteli ya Nyumabni ni moja ya hoteli yenye hadhi kubwa mkoani Tanga na ambayo itafungua ukurasa mpya kwa wawekezaji wengine.

"Mbunge wenu mnajua nimemaliza huko Ulaya, lakini hoteli hii nilipoingai kwenye vyumba nimekuta vitu ambavyo nikiwa huko Ulaya kwenye mahoteli makubwa nimekutana na mambo makubwa mabyo yamo humu ndani, hii ni changamoto kwa wawekezaji wengine kuona umuhimu wa kuwekeza mahoteli makubwa kama haya katika Jiji letu," alisema Injinia Nundu.



Na Mashaka Mhando, Tanga

Saturday, September 3, 2011

WAZIRI MKUU AWASILI MKOANI TANGA

Waziri Mkuu, Mizwngo Pinda akisalimiana na Mkuu wa Kanisa la Anglicana nchini, askofu Mokiwa baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Tanga septemba 3, 2011 akielekea Korogwe ambako Septemba 4, 2011 atakuwa mgeni rasmi kwenye ibada ya kuwekwa wakfu Askofu Mteule Maimba Modlwa wa Dayosisi ya Tanga (Picha na ofisi ya waziri mkuu)




Tuesday, August 30, 2011

ANKO MO BLOGSPOT INAKUTAKIA EID MUBARAK NJEMA

Anko Mo Blogspot inawatakia waislam wote Eid Mubark njema. Ni muda mrefu hatukuwa pamoja japokuwa mlikuwa mkipata habari za hapa na pale, yote hiyo ilitokana na Mwezi Mtukufu wa ramadhan. Libeneke linaendelea.

Saturday, August 27, 2011

Friday, August 26, 2011

KING MAJUTO KUTOKA TANGA!

MSANII mkongwe wa vichekesho Nchini Amri Athumani 'King Majuto'amesema kuwa tangu ameanza kuigiza hajawahi kufikiria kuacha na wala hana mpango huo ingawa umri wake ni mkubwa.Msanii huyo ambae pamoja na umri wake mkubwa ana uwezo wa kuigiza nafasi zote ukitaka awe kijana nakua na ukitaka awe mzee anakua.


Alisema anawashangaa wanaofikiria kwamba ataacha leo au kesho kuigiza wamesahau kuwa hiyo ni kazi yake."Nawashangaa wanadhani nitaacha kuigiza leo au kesho eti umri wangu mkubwa mbona kwenye mashindano mbali mbali nawafunika"alisema Majuto.

Alifafanua kuwa pamoja na kuwafunika kwenye mashindano mbali mbali amekuwa halipwi fedha anazoahidiwa akishinda hivyo hataki tena kuitwa kwenye hayo mashindano uchwara.

"Nilishinda kwenyevshindano lililoandaliwa na Global Publishers lakini mpaka leo sijapewa zawadi yangu, wanaandaa mashindano bila kujiandaa matokeo yake kila nikishinda hawanipi changu hivyo sitaki tena na wakiniita siendi na ninawakumbusha mimi hii ndio kazi yangu kama alivyo Polisi .daktari ,mwalimu sasa kwani nini wanaidharau"alihoji Majuto.


Majuto alisema pamoja na misukosuko yote hiyo kupitia sanaa ya vichekesho amefanikiwa kujenga nyumba ya kuishi na anamiliki magari mawili.


Wednesday, August 24, 2011

MPIGIE KURA ZUBEDA SEIF

Mpigie Kura Miss Tanga, Zubeda Seif ili aweze kuibuka kidedea katika mashindano ya Miss Tanzania 2011. Kupiga kura andika neno 'mrembo' kisha acha nafasi unaandika namba 11 halafu unatuma kwenda namba 15550. Anza kumpigia kura sasa, onyesha uzalendo. Tanga inaweza!

Saturday, August 20, 2011

SIMBA NDANI YA MKWAKWANI LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA

Klabu Ya Simba Ya Jijini Dar Es Salaam, Itautumia Uwanja Wa Mkwakwani Kuchezea Michezo Yake Ya Ligi Kuu Ya Vodacom Inayotarajia Kuanza Augosti 20 Mwaka Huu, Kufuatia Uwanja Wa Taifa Ambao Ulipanga Kutumia Michezo Yake Kufungwa Na Serikali Baada Ya Kuharibika Kwa Michezo Ya Ligi Ya Kagame.


Kwa Mujibu Wa Habari Kutoka Kwa Mwenyekiti Wa Matawi Ya Simba Mkoani Tanga Mbwana Msumari Ni Kwamba Simba Itautumia Uwanja Wa Mkwakwani Kwa Vile Wanachama Wa Klabu Hiyo Wa Mjini Tanga Wameomba Hivyo Klabu Hiyo Kukubali.


Msumari Ambaye Pia Ni Meneja Wa Uwanja Wa Mkwakwani Alisema Kuwa Amewasiliana Na Mwenyekiti Wa Klabu Hiyo Ismail Aden Rage Kwa Njia Ya Simu Asubuhi Akiwa Dodoma Amemwakikishia Kwamba Klabu Hiyo Itatumia Uwanja Wake.


"Amenihakikishia Kabisa Kwamba Watatumia Uwanja Wa Mkwakwani Badala Ya Arusha Ambako Walisema Walipokuwa Kwenye Tamasha La Simba Day Hawakupata Mapato Ya Kutosha Hivyo Kuona Ni Vema Wakahama Uwanja Huo Na Kuutumia Uwanja Wetu," Alisema Msumari Na Kuongeza Kwamba Katika Tamasha Hilo Simba Walipata Milioni 25 Tu.


Kama Itakuwa Hivyo, Mashabiki Wa Tanga Wataweza Kupata Uhondo Mkubwa Hasa Timu Hiyo Ikija Kupambana Na Mtani Wake Yanga Ambaye Juzi Wamempa Kipacho Cha Mabao 2-0, Tusubiri Tuone Na Blogu Yako Hii Italifuatilia Kwa Karibu Suala Hili Ili Liweze Kukujuza.

Friday, August 19, 2011

JENGO LA WATU WENYE VVU NA UKIMWI LAZINDULIWA BOMBO TANGA

Mganga Mkuu Wa Mkoa Wa Tanga Dkt Ally Uledi Akisoma Risala Katika Ufunguzi Wa Jengo La Kliniki Ya Matunzo Na Matibabu Ya Watu Wenye Vvu Na Ukimwi Katika Hospitali Ya Bombo Mkoani Tanga.



Baadhi Ya Watu Mbalimbali Waliofika Kwenye Uzinduzi Huo Wa Kliniki Hiyo Ya Wagonjwa Wa Vvu Na Ukimwi Wakiwemo Waandishi Wa Habari Ambapo Kushoto Ni Lulu George Wa Nipashe Na Anyefuata Ni Fatma Matulanga Wa Tbc.

Mwakilishi Wa Shirika La Kimaraekani Cdc Dkt Stefan Wiktor Akitoa Salamu Kutoka Kwa Watu Wa Marekani Ambao Wamefadhili Mradi Huo Wa Ujenzi Wa Jengo Hilo Katika Hospitali Hiyo Aliteinama Ni Waziri Wa Fya Dkt Hadji Mponda Na Pembeni Yake Ni Katibu Tawala Wa Mkoa Wa Tanga Bw. Benedictor Ole Kuyan.


Meya Wa Jiji La Tanga Bw. Omari Guledi Akihitimisha Uzinduzi Huo Kwa Kueleza Kwamba Ili Kuondoa Mrundikano Wa Wagonjwa Kaika Hospitali Hiyo Ya Bombo, Halmashauri Ya Jiji La Tanga Wapo Mbioni Kujenga Hospitali Ya Wilaya Eneo La Masiwani.



Picha zote na Mashaka Mhando

Tuesday, August 16, 2011

COASTAL UNION KUKUTANA JUMAPILI



KLABU ya soka ya Coastal Union ya Tanga Agosti 13 inatarajia kufanya mkutano mkuu kwa ajili ya kukusanya na kuzungumza na wanachama kupanga mikakati itakayoifanya timu hiyo kung’ara kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Hemed Aurora alisema pamoja na mambo mengine madhumuni ya mkutano huo ni kuzungumza na wanachama ili kupanga mikakati ya kuhakikisha timu yao hiyo inafanya vizuri kwenye Ligi Kuu.


(Gari ya Coastal Union)


Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2011/2012 inatarajiwa kuanza Agosti 20 katika viwanja mbalimbali nchini ambapo Coastal Union watashuka dimbani kucheza na Mtibwa Sugar

Saturday, August 13, 2011

CRDB YAWASAIDIA WAKULIMA WA KILIMO CHA MPUNGA KOROGWE

Afisa wa benki ya crdb la mkoani tanga akiangalia moja ya mashamba ya mpunga wilayani korogwe ambayo benki hiyo imekuwa ikisaidia kilimo cha umwagiliaji kuwainua wakulima.



Mfereji wa maji yanayokwenda kwenye mashamba ya mpunga ambao umekarabatiwa kwa mamilioni ya fedha kwa ajili ya kuwasaidia wakulima wa mpunga wilayani korogwe kulikofanywa na benki hiyo ya crdb


COASTAL UNION YAITUMIA SALAM MTIBWA

KLABU ya Coastal Union imesema kuwa inatarajiwa kufanya vizuri katika mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu kati yao na Mtibwa Sugar ya Manungu Turiani katika mchezo unaotarajiwa kufanyika katika uwanja wa Mkwakwani agosti 20 mwaka huu.


Akizungumza na blog hii ,Mwenyekiti wa Klabu hiyo,Hemed Aurora amesema maandalizi ya mchezo huo hivi sasa yanaendelea vizuri ambapo timu hiyo inafanya mazoezi yake katika uwanja wa chuo cha Shinzu Mombasa chini ya kocha wao,Hafidhi Badru.

Aidha aliongeza kuwa uongozi wa Klabu hiyo unamshukuru mkuu wa mkoa wa Tanga,Said Kalembo ,mkuu wa wilaya ya Tanga pamoja na wabunge wa mkoa wa Tanga kwa kuwa msatri wa mbele kujitolea kuweza kuisaidia timu hiyo na kuhaidi kutowaangisha katika michezo mbalimbali ya ligi kuu msimu huu.

Aurora aliwataka wakazi wa mkoa wa Tanga pamoja na wadau wengine waliopo hapa nchini kujitokeza ili kuweza kuisadia timu hiyo ili iweze kufanya vizuri katika michuano ya ligi kuu na kuweza kurudisha heshima ya mkoa wa Tanga ambayo ilikuwa imepotea muda mrefu na hivi sasa imerudi tena.

Tuesday, August 9, 2011

MKAA TUFE- NISHATI MBADA ILIYOANZA KUTUMIKA LUSHOTO


MIONGONI mwa suala yanayotishia uhai wa viumbe na mimea duniani hivi sasa ni suala la mabadiliko ya tabia nchi na hali ya hewa kwa ujumla. Mabadiliko hayo chanzo chake kimetokana na uharibifu wa mazingira asilia unaoendelezwa na binadamu wakati anapojishughulisha ili kutafuta maendeleo pasipo kuzingatia kanuni za uasilia. Matokeo ya jumla ya shughuli hizo ni kuongezeka kwa joto duniani linalosababishwa na kasi ya uzalishaji wa gesi ya ukaa katika anga na kuathiri uhai wa Binadamu, viumbe hai wengine na mimea pia.

Athari kubwa itokanayo na mabadiliko ya Hali ya Hewa ni kupanda kwa kiwango cha joto duniani ambako husababisha mabadiliko katika nchi na kuleta matukio yenye athari hasi kwa binadamu kiuchumi na kijamii. Athari mbalimbali zimeendelea kuonekana katika maeneo tofauti tofauti duniani ikiwemo hapa Tanzania na kuanza kufifisha matumaini ya kiuchumi ya wananchi wengi katika maeneo mbalimbali hasa ikizingatiwa kwamba wengi kati yao wanategemea sana shughuli za kilimo na uvuvi kupata kipato.

Pamoja na mambo mengine kimsingi zimepunguza kasi ya utekelezaji wa shughuli muhimu za kiuchumi ambazo katika maeneo mengi zimekuwa zikitegemea uwepo wa bahari, mito na maziwa, mvua za uhakika pamoja na misitu. Matokeo ya mabadiliko hayo yamevuta hisia tofauti kwa taifa na wanaharakati mbalimbali wa mazingira kuanza kujaribu kuhamasisha jamii kupunguza shughuli hasi za kiuchumi na kijamii kwa mazingira kama mbinu ya kupunguza kasi ya vitendo vinavyochochea.

Kutokana na uzito wa matokeo hayo Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga, kwa kushirikiana na wanaharakati wa masuala ya mazingira imeanzisha kampeni maalumu ya kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kama njia ya kukabili tatizo. Lushoto ndiyo wilaya pekee katika mkoa wa Tanga iliyokuwa ikiongoza kwa kuwa na msimu mrefu wa baridi kwa mwaka, ikilinganishwa na maeneo mengine ya wilaya saba zilizosalia ambazo kwa pamoja zinaunda mkoa huo. Wenyeji wa wilaya hiyo wanabainisha kwamba ilikuwa ni jambo la kawaida kwa Mvua ya Barafu kunyesha kwenye maeneo mengi ya wilaya hiyo.

Hapakuwepo na msimu wa joto kutokana na uwepo wa misitu minene, iliyokuwa imefunika Tao la Milima ya Usambara Magharibi. Wanasema ni katika miaka ya hivi karibuni ndipo waliposhangaa kuona hali ikianza kubadilika na kushuhudia ukame unavyokausha mazao katika baadhi ya mashamba, kuanza kwa msimu wa joto ambao awali haukuwepo kabisa sambamba na idadi kubwa ya wananchi kuugua ugonjwa hatari wa Malaria unaoenezwa na Mbu ambao wanapenda kuishi zaidi kwenye maeneo yanye joto kali.

Wanasema hayo yote ni matokeo ya wananchi kujihusisha na shughuli za kijamii na kiuchumi kama vile uchomaji ovyo misitu, ukataji wa miti kwa ajili ya kuni, kuchoma mkaa, mbao na magogo, kilimo katika vyanzo vya maji pamoja na uchimbaji wa madini shughuli ambazo licha ya kuwaongezea kipato, sasa zimewatumbukia nyongo na kuanza kuwataabisha. Tegemeo kubwa la wakazi wa wilaya ya Lushoto ni kilimo cha matunda, mboga mboga na biashara ambavyo tayari vimeanza kuathiriwa na mabadiliko hayo ya tabianchi.

Majira ya mwaka yanabadilika kiasi kwamba ratiba ya mvua haieleweki, hasa kwa vile wakati na kiasi cha mvua za masika na vuli kunyesha hakitabiriki kutokana na ujio wa Kiangazi ambacho sasa kimeingia kwa kasi katika maeneo mengi ya wilaya hiyo na kusababisha jua kuwa kali badala ya baridi na mvua za barafu. Aidha, shughuli za kijamii ikiwemo kuongezaka kwa idadi ya watu ambao wanahitaji maeneo zaidi ya makazi na kilimo kwa namna moja au nyingine kumechangia matokeo hayo kutokana na ukweli kwamba ujenzi wa makazi unahitaji ardhi pamoja na rasilimali misitu ili kukamilisha makazi.

Kutokana na kupanuka kwa mji na makazi kumeshawishi ongezeko la mahitaji ya kupata nishati ya uhakika kwa ajili ya kupikia ikiwemo kuni na mkaa yameongezeaka wilayani humo hali ambayo kidogo kidogo inaendelea kuchochea uharibifu wa mazingira hasa katika misitu. Hivyo basi, Katika kukabiliana na changamoto hizo za uharibifu wa mazingira taasisi isiyo ya kiserikali kwa kushirikiana na Halmashauri hiyo ya wilaya wanatekeleza Kampeni hiyo maalum ili kuunga mkono juhudi za serikali za kuhamasisha jamii kupunguza athari hasi kwa kusisitiza matumizi ya Nishati Mbadala kwa kupikia.

Kampeni hiyo ki msingi inalenga kuwaelimisha wananchi wa wilayani humo namna ya kupokea mabadiliko hayo na kutafuta mbadala wa matumizi ya nishati za kuni na mkaa kuanzia ngazi ya kaya ili kusaidia kuwajengea wananchi uwezo zaidi kwa sababu bado wanategemea kuendesha maisha kwa kutumia uwepo wa misitu ya milima ya Usambara. Kupitia kampeni hiyo, wananchi wanaelewesha sera zilizopo, faida na umuhimu wa kutunza mazingira kwa kuhimiza matumizi ya nishati ya mkaa mbadala wa kupikia maarufu kama mkaa tufe (briquettes), tofauti na mazoea yaliyojengeka miongoji mwa jamii ya watanzania ya kutumia kuni na mkaa kupikia.

Ili kuhakikisha kampeni hiyo inafanikiwa na kuenezwa katika maeneo mengi ya mkoa wa Tanga na Tanzania kwa ujumla Wanaharakati hao wa masuala ya Mazingira ambao ni Kampuni ya Environmental Engineering (EEco) Ltd, inaanzisha kiwanda cha kutengeneza kwa wingi Mkaa Tufe mjini humo. Aina hiyo ya nishati itakayozalishwa na kiwanda hicho, haina tofauti na ile inayotengenezwa sasa na baadhi ya vikundi vya wanawake wajasiriamali wadogo walioko wilayani humo, ambao awali walipatiwa teknolojia hiyo na kuanza kuzalisha mkaa tufe kwa matumizi ya kaya katika vijiji wanamoishi. Mkaa tufe uwezo mkubwa wa kuhifadhi mazingira kutokana na kumudu kupunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya kuni na mkaa nyumbani tofauti na hali ya mahitaji ilivyo sasa katika kaya nyingi za wilayani humo na katika makazi yaliyoko mjini.

Mkurugenzi wa kampuni hiyo yenye makazi yake wilayani hapa, John Nshunju, akizungumza kwenye mahojiano maalum hivi karibuni amesema mkaa tufe ni rahisi kwa kuwa unatengenezwa kwa kutumia teknolojia rahisi ya kuchanganya takataka za shambani, majani, karatasi, vumbi la mbao au mpunga na maji kwa kutumia mashine maalumu iitwayo ‘divider’. “Ni aina ya mkaa tofauti na ule ambao tumezoea kuuona, Mkaa Tufe unaundwa katika umbo la vipande vya mviringo vyenye tobo katikati ili kuruhusu hewa kupita kwa urahisi wakati wa kuuchoma, mkaa huu unafaa kutumiwa kwenye jiko la aina yoyote likiwemo la kuni,” anaeleza.

Mkurugenzi huyo anabainisha kuwa kipande kimoja cha mkaa huo, ambacho kwa sasa kinauzwa kwa bei ya Sh 100 kina uwezo wa kumudu kuchemsha chai inayotosha kunywewa na watu watatu kwa wakati mmoja na kudai nishati hiyo licha ya kuboresha mazingira inasaidia kupunguza gharama za fedha kwa ajili ya kununua mkaa kwa matumizi ya kaya kwa siku. “Mkaa tufe pamoja na kutumika kuhifadhi mazingira pia unasaidia kupunguza gharama za kununua mkaa na kuni nyumbani mathalani kwa wastani kwa siku moja hapa Lushoto familia inauwezo wa kutumia mkaa wa kati ya Sh 800 hadi Sh 1,000 kupikia chakula cha familia lakini kwa kutumia vipande vinne tu vya mkaa tufe vinamtosheleza mama kuandaa chai na chakula cha familia ikiwemo kuchemsha maharage yanayoweza kuliwa na watu wanne,” anasema.

Anasema tangu kuanzishwa kwa Kampuni hiyo miaka mitano iliyopita, wamefanikiwa kufundisha na kuwezesha mtaji midogo kwa vikundi vitatu vya wanawake, ambayo kwa kutumia mashine ndogo za mkono sasa wanazalisha na kuuza mkaa tufe kwa jamii zinayowazunguka. Kampuni ya Environmental Engineering (EEco) Ltd inaamini kwamba kupatikana kwa kiwanda hicho Lushoto, kutaongeza uzalishaji mara dufu wa nishati hiyo ili baadaye iweze kufikia wananchi wengi zaidi, kwa sababu malighafi ipo nyingi na inapatikana bure.




Thursday, August 4, 2011

MADAKTARI BINGWA KUFANYA UPASUAJI BURE TANGA

Jopo la madaktari bingwa tisa kutoka Shirika la Interplast la Ujerumani linatarajiwa kuendesha huduma za upasuaji wa kurekebisha sura na maumbile kwa wakazi wa mkoa wa Tanga wenye matatizo hayo.


Huduma hiyo itatolewa bure kwa siku 15 mfululizo kuanzia Julai 31 hadi Agosti 14 mwaka huu kwa kuhusisha madaktari hao watakaoshirikiana na madaktari wengine wa Hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo.


Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Tanga, mratibu wa upasuaji huo, Dk. Wallace Karata alisema utahusisha midomo iliyopasuka, kaa kaa lililopasuka, makovu sugu yanayozuia muonekano na utendaji kazi wa viungo mbalimbali pamoja na uvimbe mwilini.


Dk. Karata alisema, matibabu hayo yatatolewa bure kwa kuwa shirika hilo limegharamia vitu vyote muhimu kwa ajili ya kufanikisha matibabu hayo isipokuwa gharama za usajili wa mgonjwa pamoja na kulazwa.


“Kwa mara ya nne sasa shirika hilo litaleta jopo la madaktari bingwa wa upasuaji wa kurekebisha viungo mbali
mbali hapa mkoani kwetu Tanga, tunaomba wananchi wajitokeze kwa wingi tena mwaka huu kwa kuwa matibabu yatatolewa bure.


“Kila mgonjwa atachangia Sh 1,000 ya kusajili kadi pale hospitali ya Bombo,” alisema na kuongeza kuwa kwa wagonjwa watakaofanyiwa upasuaji mkubwa, watalazimika kuendelea kupata matibabu chini ya uangalizi wa madaktari.


Tangu kuanza kutolewa kwa matibabu hayo kwenye Mkoa wa Tanga, mwaka 2008 hadi mwaka jana tayari wagonjwa 119 wamefanyiwa upasuaji wa kurekebisha maumbile yao huku wengi wao wakiwa ni watu wazima.


Na Anna Makange, Tanga

AUAWA KWA KUUA WATOTO WAWILI KWA SHOKA

MKAZI wa kijiji cha Misima, Rashidi Maglasi (35), ameuawa na wananchi akituhumiwa kuwaua watoto wawili kwa kuwakata kwa shoka vichwani na kuwajeruhi wazazi wao.


Tukio hilo lilitokea hivi karibuni baada ya Maglasi kuwaua Ridhiwan Bakari (6) aliyekuwa na baba yake Bakari Mokiwa (53) ambao walikuwa wakitokea hospitali kwa ajili ya matibabu ya mtoto huyo. Katika tukio hilo, muuaji huyo alimjeruhi baba wa mtoto huyo.


Habari zaidi zinasema kwamba baada ya tukio hilo, muuaji huyo alikimbia umbali mrefu kidogo ndipo alipokutana na Mwajiha Mwalimu akiwa na mtoto wake Gumbo Mukwagu (4) ambapo aliendeleza mashambulizi hayo na kumuua mtoto na kisha kumjeruhi mama yake.


Baada ya tukio hilo, Mwalimu alipiga kelele za kuomba msaada ndipo wananchi walipotokea na kuanza kumshambulia muuaji huyo hadi kufa. Akithibitisha tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constatine Masawe, alisema huenda muuaji alikua na matatizo ya akili, jambo ambalo bado halijapatiwa uthibitisho.


Hata hivyo wazazi wa watoto hao wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Handeni wakiendelea na matibabu na polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
Auawa kwa kuua watoto wawili kwa shoka.

Na Bertha Mwambela, Handeni, Tanga