BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Saturday, October 31, 2009

BANANA ZORRO JUKWAA MOJA NA WAHAPA HAPA!!

MwanamuzikiI wa muziki wa kizazi kipya Banana Zoro anatarajia kushiriki kwenye tamasha kubwa la uzinduzi wa albamu ya Wahapahapa inayotoa elimu juu ya kuwaepusha vijana na ngono zembe litakalofanyika Novemba 6, jijini Mbeya.

Akizungumza na waandishi wa habari, Afisa kutoka wizara ya Afya anayeshughulikia masuala ya Habari na Ukimwi, Benard Fimbo alisema kuwa lengo la tamasha hilo ni kutoa elimu kwa vijana juu ya kujiepusha na ngono ambazo zinaweza kuwasababishia kupata maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
Fimbo alisema kuwa katika miaka ya karibuni kwa kiasi kikubwa wasanii, wanahabari na mashirika binafsi yanayojihusisha na mapambano dhidi ya Ukimwi wamesaidia kupunguza maambuki ya ugonjwa huo tofauti na ilivyokuwa katika miaka ya nyuma.

Kwa upande wake mkurugenzi wa waandaaji wa tamasha hilo Deo Mwanansabi alisema kuwa mbali ya Banana kutoa burudani kwenye tamasha hilo pia kutakuwa na wanamuziki wengine wa hapa nchini.

Aliwataja wanamuziki hao kuwa ni Enika, bendi kongwe ya muziki wa dansi ya Mlimani Park na bendi ya Wahapahapa.

Tembelea Anko Mo



No comments:

Post a Comment