BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, August 30, 2011

ANKO MO BLOGSPOT INAKUTAKIA EID MUBARAK NJEMA

Anko Mo Blogspot inawatakia waislam wote Eid Mubark njema. Ni muda mrefu hatukuwa pamoja japokuwa mlikuwa mkipata habari za hapa na pale, yote hiyo ilitokana na Mwezi Mtukufu wa ramadhan. Libeneke linaendelea.

Saturday, August 27, 2011

Friday, August 26, 2011

KING MAJUTO KUTOKA TANGA!

MSANII mkongwe wa vichekesho Nchini Amri Athumani 'King Majuto'amesema kuwa tangu ameanza kuigiza hajawahi kufikiria kuacha na wala hana mpango huo ingawa umri wake ni mkubwa.Msanii huyo ambae pamoja na umri wake mkubwa ana uwezo wa kuigiza nafasi zote ukitaka awe kijana nakua na ukitaka awe mzee anakua.


Alisema anawashangaa wanaofikiria kwamba ataacha leo au kesho kuigiza wamesahau kuwa hiyo ni kazi yake."Nawashangaa wanadhani nitaacha kuigiza leo au kesho eti umri wangu mkubwa mbona kwenye mashindano mbali mbali nawafunika"alisema Majuto.

Alifafanua kuwa pamoja na kuwafunika kwenye mashindano mbali mbali amekuwa halipwi fedha anazoahidiwa akishinda hivyo hataki tena kuitwa kwenye hayo mashindano uchwara.

"Nilishinda kwenyevshindano lililoandaliwa na Global Publishers lakini mpaka leo sijapewa zawadi yangu, wanaandaa mashindano bila kujiandaa matokeo yake kila nikishinda hawanipi changu hivyo sitaki tena na wakiniita siendi na ninawakumbusha mimi hii ndio kazi yangu kama alivyo Polisi .daktari ,mwalimu sasa kwani nini wanaidharau"alihoji Majuto.


Majuto alisema pamoja na misukosuko yote hiyo kupitia sanaa ya vichekesho amefanikiwa kujenga nyumba ya kuishi na anamiliki magari mawili.


Wednesday, August 24, 2011

MPIGIE KURA ZUBEDA SEIF

Mpigie Kura Miss Tanga, Zubeda Seif ili aweze kuibuka kidedea katika mashindano ya Miss Tanzania 2011. Kupiga kura andika neno 'mrembo' kisha acha nafasi unaandika namba 11 halafu unatuma kwenda namba 15550. Anza kumpigia kura sasa, onyesha uzalendo. Tanga inaweza!

Saturday, August 20, 2011

SIMBA NDANI YA MKWAKWANI LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA

Klabu Ya Simba Ya Jijini Dar Es Salaam, Itautumia Uwanja Wa Mkwakwani Kuchezea Michezo Yake Ya Ligi Kuu Ya Vodacom Inayotarajia Kuanza Augosti 20 Mwaka Huu, Kufuatia Uwanja Wa Taifa Ambao Ulipanga Kutumia Michezo Yake Kufungwa Na Serikali Baada Ya Kuharibika Kwa Michezo Ya Ligi Ya Kagame.


Kwa Mujibu Wa Habari Kutoka Kwa Mwenyekiti Wa Matawi Ya Simba Mkoani Tanga Mbwana Msumari Ni Kwamba Simba Itautumia Uwanja Wa Mkwakwani Kwa Vile Wanachama Wa Klabu Hiyo Wa Mjini Tanga Wameomba Hivyo Klabu Hiyo Kukubali.


Msumari Ambaye Pia Ni Meneja Wa Uwanja Wa Mkwakwani Alisema Kuwa Amewasiliana Na Mwenyekiti Wa Klabu Hiyo Ismail Aden Rage Kwa Njia Ya Simu Asubuhi Akiwa Dodoma Amemwakikishia Kwamba Klabu Hiyo Itatumia Uwanja Wake.


"Amenihakikishia Kabisa Kwamba Watatumia Uwanja Wa Mkwakwani Badala Ya Arusha Ambako Walisema Walipokuwa Kwenye Tamasha La Simba Day Hawakupata Mapato Ya Kutosha Hivyo Kuona Ni Vema Wakahama Uwanja Huo Na Kuutumia Uwanja Wetu," Alisema Msumari Na Kuongeza Kwamba Katika Tamasha Hilo Simba Walipata Milioni 25 Tu.


Kama Itakuwa Hivyo, Mashabiki Wa Tanga Wataweza Kupata Uhondo Mkubwa Hasa Timu Hiyo Ikija Kupambana Na Mtani Wake Yanga Ambaye Juzi Wamempa Kipacho Cha Mabao 2-0, Tusubiri Tuone Na Blogu Yako Hii Italifuatilia Kwa Karibu Suala Hili Ili Liweze Kukujuza.

Friday, August 19, 2011

JENGO LA WATU WENYE VVU NA UKIMWI LAZINDULIWA BOMBO TANGA

Mganga Mkuu Wa Mkoa Wa Tanga Dkt Ally Uledi Akisoma Risala Katika Ufunguzi Wa Jengo La Kliniki Ya Matunzo Na Matibabu Ya Watu Wenye Vvu Na Ukimwi Katika Hospitali Ya Bombo Mkoani Tanga.



Baadhi Ya Watu Mbalimbali Waliofika Kwenye Uzinduzi Huo Wa Kliniki Hiyo Ya Wagonjwa Wa Vvu Na Ukimwi Wakiwemo Waandishi Wa Habari Ambapo Kushoto Ni Lulu George Wa Nipashe Na Anyefuata Ni Fatma Matulanga Wa Tbc.

Mwakilishi Wa Shirika La Kimaraekani Cdc Dkt Stefan Wiktor Akitoa Salamu Kutoka Kwa Watu Wa Marekani Ambao Wamefadhili Mradi Huo Wa Ujenzi Wa Jengo Hilo Katika Hospitali Hiyo Aliteinama Ni Waziri Wa Fya Dkt Hadji Mponda Na Pembeni Yake Ni Katibu Tawala Wa Mkoa Wa Tanga Bw. Benedictor Ole Kuyan.


Meya Wa Jiji La Tanga Bw. Omari Guledi Akihitimisha Uzinduzi Huo Kwa Kueleza Kwamba Ili Kuondoa Mrundikano Wa Wagonjwa Kaika Hospitali Hiyo Ya Bombo, Halmashauri Ya Jiji La Tanga Wapo Mbioni Kujenga Hospitali Ya Wilaya Eneo La Masiwani.



Picha zote na Mashaka Mhando

Tuesday, August 16, 2011

COASTAL UNION KUKUTANA JUMAPILI



KLABU ya soka ya Coastal Union ya Tanga Agosti 13 inatarajia kufanya mkutano mkuu kwa ajili ya kukusanya na kuzungumza na wanachama kupanga mikakati itakayoifanya timu hiyo kung’ara kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Hemed Aurora alisema pamoja na mambo mengine madhumuni ya mkutano huo ni kuzungumza na wanachama ili kupanga mikakati ya kuhakikisha timu yao hiyo inafanya vizuri kwenye Ligi Kuu.


(Gari ya Coastal Union)


Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2011/2012 inatarajiwa kuanza Agosti 20 katika viwanja mbalimbali nchini ambapo Coastal Union watashuka dimbani kucheza na Mtibwa Sugar

Saturday, August 13, 2011

CRDB YAWASAIDIA WAKULIMA WA KILIMO CHA MPUNGA KOROGWE

Afisa wa benki ya crdb la mkoani tanga akiangalia moja ya mashamba ya mpunga wilayani korogwe ambayo benki hiyo imekuwa ikisaidia kilimo cha umwagiliaji kuwainua wakulima.



Mfereji wa maji yanayokwenda kwenye mashamba ya mpunga ambao umekarabatiwa kwa mamilioni ya fedha kwa ajili ya kuwasaidia wakulima wa mpunga wilayani korogwe kulikofanywa na benki hiyo ya crdb


COASTAL UNION YAITUMIA SALAM MTIBWA

KLABU ya Coastal Union imesema kuwa inatarajiwa kufanya vizuri katika mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu kati yao na Mtibwa Sugar ya Manungu Turiani katika mchezo unaotarajiwa kufanyika katika uwanja wa Mkwakwani agosti 20 mwaka huu.


Akizungumza na blog hii ,Mwenyekiti wa Klabu hiyo,Hemed Aurora amesema maandalizi ya mchezo huo hivi sasa yanaendelea vizuri ambapo timu hiyo inafanya mazoezi yake katika uwanja wa chuo cha Shinzu Mombasa chini ya kocha wao,Hafidhi Badru.

Aidha aliongeza kuwa uongozi wa Klabu hiyo unamshukuru mkuu wa mkoa wa Tanga,Said Kalembo ,mkuu wa wilaya ya Tanga pamoja na wabunge wa mkoa wa Tanga kwa kuwa msatri wa mbele kujitolea kuweza kuisaidia timu hiyo na kuhaidi kutowaangisha katika michezo mbalimbali ya ligi kuu msimu huu.

Aurora aliwataka wakazi wa mkoa wa Tanga pamoja na wadau wengine waliopo hapa nchini kujitokeza ili kuweza kuisadia timu hiyo ili iweze kufanya vizuri katika michuano ya ligi kuu na kuweza kurudisha heshima ya mkoa wa Tanga ambayo ilikuwa imepotea muda mrefu na hivi sasa imerudi tena.

Tuesday, August 9, 2011

MKAA TUFE- NISHATI MBADA ILIYOANZA KUTUMIKA LUSHOTO


MIONGONI mwa suala yanayotishia uhai wa viumbe na mimea duniani hivi sasa ni suala la mabadiliko ya tabia nchi na hali ya hewa kwa ujumla. Mabadiliko hayo chanzo chake kimetokana na uharibifu wa mazingira asilia unaoendelezwa na binadamu wakati anapojishughulisha ili kutafuta maendeleo pasipo kuzingatia kanuni za uasilia. Matokeo ya jumla ya shughuli hizo ni kuongezeka kwa joto duniani linalosababishwa na kasi ya uzalishaji wa gesi ya ukaa katika anga na kuathiri uhai wa Binadamu, viumbe hai wengine na mimea pia.

Athari kubwa itokanayo na mabadiliko ya Hali ya Hewa ni kupanda kwa kiwango cha joto duniani ambako husababisha mabadiliko katika nchi na kuleta matukio yenye athari hasi kwa binadamu kiuchumi na kijamii. Athari mbalimbali zimeendelea kuonekana katika maeneo tofauti tofauti duniani ikiwemo hapa Tanzania na kuanza kufifisha matumaini ya kiuchumi ya wananchi wengi katika maeneo mbalimbali hasa ikizingatiwa kwamba wengi kati yao wanategemea sana shughuli za kilimo na uvuvi kupata kipato.

Pamoja na mambo mengine kimsingi zimepunguza kasi ya utekelezaji wa shughuli muhimu za kiuchumi ambazo katika maeneo mengi zimekuwa zikitegemea uwepo wa bahari, mito na maziwa, mvua za uhakika pamoja na misitu. Matokeo ya mabadiliko hayo yamevuta hisia tofauti kwa taifa na wanaharakati mbalimbali wa mazingira kuanza kujaribu kuhamasisha jamii kupunguza shughuli hasi za kiuchumi na kijamii kwa mazingira kama mbinu ya kupunguza kasi ya vitendo vinavyochochea.

Kutokana na uzito wa matokeo hayo Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga, kwa kushirikiana na wanaharakati wa masuala ya mazingira imeanzisha kampeni maalumu ya kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kama njia ya kukabili tatizo. Lushoto ndiyo wilaya pekee katika mkoa wa Tanga iliyokuwa ikiongoza kwa kuwa na msimu mrefu wa baridi kwa mwaka, ikilinganishwa na maeneo mengine ya wilaya saba zilizosalia ambazo kwa pamoja zinaunda mkoa huo. Wenyeji wa wilaya hiyo wanabainisha kwamba ilikuwa ni jambo la kawaida kwa Mvua ya Barafu kunyesha kwenye maeneo mengi ya wilaya hiyo.

Hapakuwepo na msimu wa joto kutokana na uwepo wa misitu minene, iliyokuwa imefunika Tao la Milima ya Usambara Magharibi. Wanasema ni katika miaka ya hivi karibuni ndipo waliposhangaa kuona hali ikianza kubadilika na kushuhudia ukame unavyokausha mazao katika baadhi ya mashamba, kuanza kwa msimu wa joto ambao awali haukuwepo kabisa sambamba na idadi kubwa ya wananchi kuugua ugonjwa hatari wa Malaria unaoenezwa na Mbu ambao wanapenda kuishi zaidi kwenye maeneo yanye joto kali.

Wanasema hayo yote ni matokeo ya wananchi kujihusisha na shughuli za kijamii na kiuchumi kama vile uchomaji ovyo misitu, ukataji wa miti kwa ajili ya kuni, kuchoma mkaa, mbao na magogo, kilimo katika vyanzo vya maji pamoja na uchimbaji wa madini shughuli ambazo licha ya kuwaongezea kipato, sasa zimewatumbukia nyongo na kuanza kuwataabisha. Tegemeo kubwa la wakazi wa wilaya ya Lushoto ni kilimo cha matunda, mboga mboga na biashara ambavyo tayari vimeanza kuathiriwa na mabadiliko hayo ya tabianchi.

Majira ya mwaka yanabadilika kiasi kwamba ratiba ya mvua haieleweki, hasa kwa vile wakati na kiasi cha mvua za masika na vuli kunyesha hakitabiriki kutokana na ujio wa Kiangazi ambacho sasa kimeingia kwa kasi katika maeneo mengi ya wilaya hiyo na kusababisha jua kuwa kali badala ya baridi na mvua za barafu. Aidha, shughuli za kijamii ikiwemo kuongezaka kwa idadi ya watu ambao wanahitaji maeneo zaidi ya makazi na kilimo kwa namna moja au nyingine kumechangia matokeo hayo kutokana na ukweli kwamba ujenzi wa makazi unahitaji ardhi pamoja na rasilimali misitu ili kukamilisha makazi.

Kutokana na kupanuka kwa mji na makazi kumeshawishi ongezeko la mahitaji ya kupata nishati ya uhakika kwa ajili ya kupikia ikiwemo kuni na mkaa yameongezeaka wilayani humo hali ambayo kidogo kidogo inaendelea kuchochea uharibifu wa mazingira hasa katika misitu. Hivyo basi, Katika kukabiliana na changamoto hizo za uharibifu wa mazingira taasisi isiyo ya kiserikali kwa kushirikiana na Halmashauri hiyo ya wilaya wanatekeleza Kampeni hiyo maalum ili kuunga mkono juhudi za serikali za kuhamasisha jamii kupunguza athari hasi kwa kusisitiza matumizi ya Nishati Mbadala kwa kupikia.

Kampeni hiyo ki msingi inalenga kuwaelimisha wananchi wa wilayani humo namna ya kupokea mabadiliko hayo na kutafuta mbadala wa matumizi ya nishati za kuni na mkaa kuanzia ngazi ya kaya ili kusaidia kuwajengea wananchi uwezo zaidi kwa sababu bado wanategemea kuendesha maisha kwa kutumia uwepo wa misitu ya milima ya Usambara. Kupitia kampeni hiyo, wananchi wanaelewesha sera zilizopo, faida na umuhimu wa kutunza mazingira kwa kuhimiza matumizi ya nishati ya mkaa mbadala wa kupikia maarufu kama mkaa tufe (briquettes), tofauti na mazoea yaliyojengeka miongoji mwa jamii ya watanzania ya kutumia kuni na mkaa kupikia.

Ili kuhakikisha kampeni hiyo inafanikiwa na kuenezwa katika maeneo mengi ya mkoa wa Tanga na Tanzania kwa ujumla Wanaharakati hao wa masuala ya Mazingira ambao ni Kampuni ya Environmental Engineering (EEco) Ltd, inaanzisha kiwanda cha kutengeneza kwa wingi Mkaa Tufe mjini humo. Aina hiyo ya nishati itakayozalishwa na kiwanda hicho, haina tofauti na ile inayotengenezwa sasa na baadhi ya vikundi vya wanawake wajasiriamali wadogo walioko wilayani humo, ambao awali walipatiwa teknolojia hiyo na kuanza kuzalisha mkaa tufe kwa matumizi ya kaya katika vijiji wanamoishi. Mkaa tufe uwezo mkubwa wa kuhifadhi mazingira kutokana na kumudu kupunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya kuni na mkaa nyumbani tofauti na hali ya mahitaji ilivyo sasa katika kaya nyingi za wilayani humo na katika makazi yaliyoko mjini.

Mkurugenzi wa kampuni hiyo yenye makazi yake wilayani hapa, John Nshunju, akizungumza kwenye mahojiano maalum hivi karibuni amesema mkaa tufe ni rahisi kwa kuwa unatengenezwa kwa kutumia teknolojia rahisi ya kuchanganya takataka za shambani, majani, karatasi, vumbi la mbao au mpunga na maji kwa kutumia mashine maalumu iitwayo ‘divider’. “Ni aina ya mkaa tofauti na ule ambao tumezoea kuuona, Mkaa Tufe unaundwa katika umbo la vipande vya mviringo vyenye tobo katikati ili kuruhusu hewa kupita kwa urahisi wakati wa kuuchoma, mkaa huu unafaa kutumiwa kwenye jiko la aina yoyote likiwemo la kuni,” anaeleza.

Mkurugenzi huyo anabainisha kuwa kipande kimoja cha mkaa huo, ambacho kwa sasa kinauzwa kwa bei ya Sh 100 kina uwezo wa kumudu kuchemsha chai inayotosha kunywewa na watu watatu kwa wakati mmoja na kudai nishati hiyo licha ya kuboresha mazingira inasaidia kupunguza gharama za fedha kwa ajili ya kununua mkaa kwa matumizi ya kaya kwa siku. “Mkaa tufe pamoja na kutumika kuhifadhi mazingira pia unasaidia kupunguza gharama za kununua mkaa na kuni nyumbani mathalani kwa wastani kwa siku moja hapa Lushoto familia inauwezo wa kutumia mkaa wa kati ya Sh 800 hadi Sh 1,000 kupikia chakula cha familia lakini kwa kutumia vipande vinne tu vya mkaa tufe vinamtosheleza mama kuandaa chai na chakula cha familia ikiwemo kuchemsha maharage yanayoweza kuliwa na watu wanne,” anasema.

Anasema tangu kuanzishwa kwa Kampuni hiyo miaka mitano iliyopita, wamefanikiwa kufundisha na kuwezesha mtaji midogo kwa vikundi vitatu vya wanawake, ambayo kwa kutumia mashine ndogo za mkono sasa wanazalisha na kuuza mkaa tufe kwa jamii zinayowazunguka. Kampuni ya Environmental Engineering (EEco) Ltd inaamini kwamba kupatikana kwa kiwanda hicho Lushoto, kutaongeza uzalishaji mara dufu wa nishati hiyo ili baadaye iweze kufikia wananchi wengi zaidi, kwa sababu malighafi ipo nyingi na inapatikana bure.




Thursday, August 4, 2011

MADAKTARI BINGWA KUFANYA UPASUAJI BURE TANGA

Jopo la madaktari bingwa tisa kutoka Shirika la Interplast la Ujerumani linatarajiwa kuendesha huduma za upasuaji wa kurekebisha sura na maumbile kwa wakazi wa mkoa wa Tanga wenye matatizo hayo.


Huduma hiyo itatolewa bure kwa siku 15 mfululizo kuanzia Julai 31 hadi Agosti 14 mwaka huu kwa kuhusisha madaktari hao watakaoshirikiana na madaktari wengine wa Hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo.


Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Tanga, mratibu wa upasuaji huo, Dk. Wallace Karata alisema utahusisha midomo iliyopasuka, kaa kaa lililopasuka, makovu sugu yanayozuia muonekano na utendaji kazi wa viungo mbalimbali pamoja na uvimbe mwilini.


Dk. Karata alisema, matibabu hayo yatatolewa bure kwa kuwa shirika hilo limegharamia vitu vyote muhimu kwa ajili ya kufanikisha matibabu hayo isipokuwa gharama za usajili wa mgonjwa pamoja na kulazwa.


“Kwa mara ya nne sasa shirika hilo litaleta jopo la madaktari bingwa wa upasuaji wa kurekebisha viungo mbali
mbali hapa mkoani kwetu Tanga, tunaomba wananchi wajitokeze kwa wingi tena mwaka huu kwa kuwa matibabu yatatolewa bure.


“Kila mgonjwa atachangia Sh 1,000 ya kusajili kadi pale hospitali ya Bombo,” alisema na kuongeza kuwa kwa wagonjwa watakaofanyiwa upasuaji mkubwa, watalazimika kuendelea kupata matibabu chini ya uangalizi wa madaktari.


Tangu kuanza kutolewa kwa matibabu hayo kwenye Mkoa wa Tanga, mwaka 2008 hadi mwaka jana tayari wagonjwa 119 wamefanyiwa upasuaji wa kurekebisha maumbile yao huku wengi wao wakiwa ni watu wazima.


Na Anna Makange, Tanga

AUAWA KWA KUUA WATOTO WAWILI KWA SHOKA

MKAZI wa kijiji cha Misima, Rashidi Maglasi (35), ameuawa na wananchi akituhumiwa kuwaua watoto wawili kwa kuwakata kwa shoka vichwani na kuwajeruhi wazazi wao.


Tukio hilo lilitokea hivi karibuni baada ya Maglasi kuwaua Ridhiwan Bakari (6) aliyekuwa na baba yake Bakari Mokiwa (53) ambao walikuwa wakitokea hospitali kwa ajili ya matibabu ya mtoto huyo. Katika tukio hilo, muuaji huyo alimjeruhi baba wa mtoto huyo.


Habari zaidi zinasema kwamba baada ya tukio hilo, muuaji huyo alikimbia umbali mrefu kidogo ndipo alipokutana na Mwajiha Mwalimu akiwa na mtoto wake Gumbo Mukwagu (4) ambapo aliendeleza mashambulizi hayo na kumuua mtoto na kisha kumjeruhi mama yake.


Baada ya tukio hilo, Mwalimu alipiga kelele za kuomba msaada ndipo wananchi walipotokea na kuanza kumshambulia muuaji huyo hadi kufa. Akithibitisha tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constatine Masawe, alisema huenda muuaji alikua na matatizo ya akili, jambo ambalo bado halijapatiwa uthibitisho.


Hata hivyo wazazi wa watoto hao wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Handeni wakiendelea na matibabu na polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
Auawa kwa kuua watoto wawili kwa shoka.

Na Bertha Mwambela, Handeni, Tanga

Wednesday, August 3, 2011

COASTAL UNION USO KWA USO NA MTIBWA SUGAR LIGI KUU


Timu ya Coastal Union ya Tanga iliyopanda daraja msimu huu itakutana na Mtibwa Sugar kwenye raundi ya kwanza ya mechi za ligi kuu kunako uwanja wao wa nyumbani wa Mkwakwani. Mechi nyingine za raundi ya kwanza zitakuwa kati ya Kagera Sugar na Ruvu Shooting (Kaitaba, Bukoba), Polisi Dodoma na African Lyon (Jamhuri, Dodoma) na Azam na Moro United (Chamazi, Dar es Salaam).

Raundi ya kwanza itamalizika Agosti 21 mwaka huu kwa mechi kati ya JKT Oljoro na Simba kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha na Yanga dhidi ya JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mzunguko wa kwanza (first leg) wa ligi hiyo utamalizika Novemba 5 mwaka huu wakati mzunguko wa pili (second leg) utamalizika Aprili Mosi mwakani ambapo jumla ya mechi 175 zitachezwa.

Pambano la watani wa jadi kati ya Yanga na Simba litafanyika Oktoba 29 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mechi ya mzunguko wa pili ambapo Simba itakuwa mwenyeji itafanyika Aprili Mosi mwakani kwenye uwanja huo huo.

NGORONGORO HEROES YAALIKWA COSAFA
Timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) imealikwa kushiriki michuano ya umri huo ya Shirikisho la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwaka Afrika (COSAFA) itakayofanyika kuanzia Desemba 1-10 jijini Gaborone, Botswana.

Wachezaji wanaotakiwa kushiriki michuano hiyo ni wale waliozaliwa baada ya Januari 1, 1992. Timu zinatakiwa kuthibitisha ushiriki wao kufikia Agosti 17 mwaka huu na ratiba itapangwa Agosti 24 mwaka huu jijini Gaborone. COSAFA itachangia sehemu ya nauli ya timu shiriki kwenda kwenye mashindano hayo.

Ngorongoro Heroes inayofundishwa na Kim Poulsen akisaidiwa na Adolf Rishard hivi sasa inafanya mazoezi ya wiki moja kila mwezi.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Tuesday, August 2, 2011

FAIDA YA FUTARI YA TENDE NA MAJI


Assalam alaykoum,

Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) ametufundisha namna ya kufturu na vyenye faida katika miongoni mwa futari.
Kufuturu ni kitu cha kwanza kinachofungua kinywa cha mfungaji mara baada ya kumaliza muda wa kufunga katika siku husika. Kifungua kinywa hiki cha mwanzo ndio huitwa futari.
Nabii wa karne hii ya sayansi na teknolojia ametuhusia sana Waislaam tunapokuwa tumefunga, ni vyema kufturu kwa tende au maji.


Mafundisho haya ya Mtume Muhammas (S.A.W) yamekuwa kinyume kabisa na namna waislaam wengi wanavyofungua saumu zao.
Watu wengi wanapofungua saum zao hukimbilia kula vyakula vya nafaka kama vile uji, juice, tambi, katlesi n.k. Pamoja na kufuturu vitu hivo vizito katika tumbo, huwa mfuturuji wa vyakula vingi mwisho hushindwa kuhema uzuri.Kuhusiana na kula Mtume Muhammad ametuhusia sana tumbo tuligawe sehemu tatu kuu nazo ni:-MajiChakulaHewa.
Utaratibu huu wakulipa nafasi tumbo kwa chakula, maji na hewa unasaidia sana katika mfumo wa usagaji wa chakula.Tende na maji ni vitu vilivyotajwa sana kwa matumisi ya mfungaji wa saum na mzazi pia.


"Basi akachukua mimba yake akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali kisha uchungu ukampelekea katika shina la mtende, akawa anazaa huku anasema laiti ningelikufa kabla ya haya na ningelikuwa niliyesahaulika kabisa, mara ikafika sauti chini kutoka chini yake ikamuambia usihuzunike Maryaam hakika Mola wako amejaalia kijito cha maji chini yako. Na litikise shina la mtende kwako litaangusha tende nzuri zilizoiva basi ule, unywe na liulie jicho lako furahi na pumua moyo wako." (QUR-AAN 19:22-26)
Kutokana na mafundisho hayo ya Quraan inaonesha tumbo la mtu aliyezaa linahitaji tende au maji kama ilivyo mtu mwenye kufunga.


Jambo la kujiuliza hekima ipi Mtume ameitumia katika kutufundisha kula tende na maji na sio kula vyakula vizito.Vyakula vya nafaka kama vile mbaazi,viazi,maandazi n.k ni vyakula vizito husababisha maumivu katika tumbo.
Hali hii hutokana na ukweli kuwa katika ukuta wa tumbo la chakula na hata katika utumbo mwembamba kuna maji mazito mfano wake kama ute wa yai la kuku, maji hayo yanasaidia aina mbali mbali za acid zisifike katika ngozi ya tumbo na kufanya michubuko ambayo yanaweza kuleta ugonjwa wa vidonda vya tumbo.Kuta za tumbo zinapokutana na acid husababisha eneo hilo kutepeta na kulifanya liwe laini.


FAIDA YA TENDE NA MAJI: katika tende na maji kuna madini mengi yanayoambatana na sukari na hewa ya oxygen. Vitu vinapofika katika eneo hili vinasaidia kupunguza nguvu ya gas, gas ambayo ikizidi hatima yake huleta matatizo na magonjwa.
Kwahio Inshallah ftari yetu ya mwanzo iwe ni tende kwa maji kisha utafuatilisha machopochopo mengine ambayo machoopochopo hayo yasiwe yakushibisha kiasi ambacho mtu ukashindwa hata kuswali taraweh.


KUTOKUFUNGA MWEZI WA RAMADHANI

Kufunga Ramadhani ni nguzo ya nne katika nguzo tano za Kiislamu na kutokufunga Ramadhani bila udhuru wowote ule wa kisheria ni moja ya madhambi makubwa sabini. Mwenyezi Mungu S.W.T. kautukuza sana mwezi wa Ramadhani kuliko miezi yote mingine kwani imeteremshwa Qurani katika mwezi huu mtukufu na pia kajaalia kuwepo katika mwezi huu usiku wa Lailatul-Qadri usiku wa heshima, usiku ulio bora kuliko miezu elfu.


Kufunga katika mwezi huu mtukufu ni faridha wajibu kwa aliyetimiza masharti yake, kama ilivyokuwa faridha wajibu kwa wale waliokuwa kabla yetu. Na yule atakaeacha kufunga siku moja tu bila sababu yoyote ile ya kisheria kama vile ugonjwa au safari, basi atakuwa amefanya madhambi makubwa. Na akifa katika hali hiyo basi atakuwa amefanya dhambi kubwa na adhabu yake ni kubwa nayo ni Moto wa Jahannam. Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil Baqarah aya ya 183 na ya 184, "?يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمْ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِنْ قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ * أَيَّامًا مَعْدُودَاتٍ فَمَنْ كَانَ مِنْكُمْ مَرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِنْ أَيَّامٍ أُخَرَ¦?


Maana yake, "Enyi mlioamini! Mmelazimishwa kufunga (saumu) kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumchaMungu. Siku chache (kufunga huko), basi atakaekuwa mgonjwa miongoni mwenu au katika safari (akafungua) basi (atimize) hesabu katika siku nyingine."Na pia Hadithi iliyopokelewa na Ibn `Umar R.A.A. na kutolewa na L-Bukhari na Muslim, Mtume S.A.W. kasema, ""بُنِيَ الإسْلامُ عَلَى خَمْسٍ : شَهَادَةِ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَأَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللَّهِ وَإِقَامِ الصَّلاةِ وَإِيتَاءِ الزَّكَاةِ وَصَوْمِ رَمَضَانَ وَحَجِّ الْبَيْتِ."Maana yake, "Umejengwa Uislamu kwa nguzo tano, (nguzo ya kwanza):


Hapana mungu mwenye kupasa kuabudiwa ila Allah, na hakika Muhammad S.A.W. ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na (nguzo ya pili): Kusimamisha Sala, na (nguzo ya tatu): Kutoa Zaka, na (nguzo ya nne): Kufunga (mwezi wa) Ramadhani na (nguzo ya tano): Kuhiji (nyumba ya Mwenyezi Mungu kwa yule mwenye uwezo)."Sahaba Ibn Abbaas R.A.A. kasema, ""عُرَى الإِسْلامِ وقواعد الدين ثلاث : شَهَادَةِ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ ، والصَّلاةُ ، وَصَوْمِ رَمَضَانَ."Maana yake, "Uislamu pamoja na kanuni za dini zimefungamana na mambo matatu: Shahada ya kuwa hapana apasae kuabudiwa (kwa haki) ila ALLAH na Sala na kufunga mwezi wa Ramadhani."

Monday, August 1, 2011

ANKO MO BLOGSPOT INAKUTAKIA MFUNGO MWEMA WA RAMADHANI

Anko Mo Blogspot inakutakia mfungo mwema wa Ramadhan.