BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Saturday, October 31, 2009

BANANA ZORRO JUKWAA MOJA NA WAHAPA HAPA!!

MwanamuzikiI wa muziki wa kizazi kipya Banana Zoro anatarajia kushiriki kwenye tamasha kubwa la uzinduzi wa albamu ya Wahapahapa inayotoa elimu juu ya kuwaepusha vijana na ngono zembe litakalofanyika Novemba 6, jijini Mbeya.

Akizungumza na waandishi wa habari, Afisa kutoka wizara ya Afya anayeshughulikia masuala ya Habari na Ukimwi, Benard Fimbo alisema kuwa lengo la tamasha hilo ni kutoa elimu kwa vijana juu ya kujiepusha na ngono ambazo zinaweza kuwasababishia kupata maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
Fimbo alisema kuwa katika miaka ya karibuni kwa kiasi kikubwa wasanii, wanahabari na mashirika binafsi yanayojihusisha na mapambano dhidi ya Ukimwi wamesaidia kupunguza maambuki ya ugonjwa huo tofauti na ilivyokuwa katika miaka ya nyuma.

Kwa upande wake mkurugenzi wa waandaaji wa tamasha hilo Deo Mwanansabi alisema kuwa mbali ya Banana kutoa burudani kwenye tamasha hilo pia kutakuwa na wanamuziki wengine wa hapa nchini.

Aliwataja wanamuziki hao kuwa ni Enika, bendi kongwe ya muziki wa dansi ya Mlimani Park na bendi ya Wahapahapa.

Tembelea Anko Mo



Sunday, October 25, 2009

PAMOJA NA MVUA- FIESTA ONE LOVE TANGA (MKWAKWANI) NI NOMAAAA!!

The Heavy Weight Mc, Profesa Jay akikamua kwa kwenda mbele kunako uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga kwenye Fiesta One Love iliyofanyika usiku wa kuamkia leo.

Mwanachemba, ndio kama hivyo tena kwenye kona Shaaaa!! Pamoja na tupo High kama KLM na kukusha kama CNN- alisababisha vya kutosha uwanja wa Mkwakwani.

Kutoka Ilala La Familia hadi Tanga Town, Chi! Chi! Chi! Chi! Chi! Chidi Benz akiwa na Chiku kwenye Fiesta One kwenye uwanja wa Mkwakwani- ilikuwa ni nomaa wadau.

Maunda akibembeleza kimtindo

Hizi ndio shangwe za Fiesta One Love jijini Tanga, Tanzania. Tazama nyomi la watu wakipata burudani kuhakikisha macho yanapata nafasi ya kuona kile kilicholetwa na Clouds Fm.

Maunda Zorro akikamua jukwaani kwa hisia kali





Saturday, October 24, 2009

FIESTA ONE LOVE LEO JIJINI TANGA- MVUA NIAJEEE BANA!!!!


Sikukuu ya wasanii Tanzania maarufu kama Fiesta safari hii ikiwa ni ONE LOVE- inashuka leo jijini Tanga huku kila kona ya mji ukiwa na hamu ya kutaka kupata raha hizo.
Katika hali isiyo ya kawaida, jiji la Tanga asubuhi ya leo hadi kufikia saa nane mchana kumekuwa na mvua kubwa jambo lilloonekana kuwakatisha tamaa wapenda burudani.
Hata hivyo shangwe zinasubiriwa kwa hamu, kwani waswahili husema Maji Ukishayavulia Nguo Ni Sharti Uyaoge!!!
Anko Mo Blogspot itajivinjari kunako uwanja wa Mkwakwani kushuhudia show hiyo na kukuletea picha za ukweli kwenye kurasa hii.

Friday, October 23, 2009

MAPANGO YA AMBONI MKOANI TANGA- KIVUTIO CHA UTALII

Mapango ya Amboni yanayopatikana mkoani Tanga, Tanzania kama yanavyoonekana katika picha. Kwa juu sehemu ya kufikia kwa watalii wanaokwenda kutazama mapango hayo.

Watu wakiingia kutazama mapango ya Amboni.

Hapa ni sehemu ya pili ya mapango hayo maarufu mkoani Tanga.

Sehemu ya kuingilia kwenye mapango ya Amboni, ambyo ni sehemu ya kihistoria inayotembelewa na watalii wengi.




Saturday, October 17, 2009

PANGANI YAPEWA HADHI KUWA MJI WA KIHISTORIA NA UTAMADUNI DUNIANI

SHIRIKA la Makumbusho Duniani la World Monuments Fund (WMF) limeutambua na kuupa heshima mji wa Pangani kuwa mmoja wa miji mikongwe ya kihistoria na urithi wa Utamaduni duniani.

Mkurugenzi wa shirika la Uzima kwa Sanaa (UZIKWASA) la mjini Pangani, Dkt. Vera Pieroth alisema mjini huo wa kihistoria umetajwa kuwa ni miongoni mwa miji 93 ya urithi wa Utamaduni iliyopo katika nchi 47 duniani zinazotambuliwa na shirika hilo.

Vera alisema kuwa uamuzi wa kutunuku mji huo heshima hiyo umetangazwa hivi karibuni na Rais wa WMF, Bonnie Burnham, jijini New York, Marekani ambapo mji wa Pangani umekuwa kati ya maeneo manne katika bara la Afrika ambayo imepewa hadhi na WMF.

“Kuteuliwa kwa mji wa Pangani ni faraja kubwa kwa watu wa hapa na shirika letu la UZIKWASA. Tangu mwaka 2007 shirika letu kwa kushirikia na Halmashauri ya Wilaya ya Pangani na Kamati za kijamii tumekuwa kutangaza vivutio vya kihistoria vya mji hapa na tunafurahi sasa juhudi za pamoja ambazo zimeleta matunda mazuri,” alisema.
Miaka miwili iliyopita UZIKWASA kwa kushirikiana na Idara ya mambo ya Kale iliendesha kongamano la kujadili jinsi ya kuhifadhi na kutanga Mali kale na urithi wa Utamaduni wa Pangani, lililofadhiliwa na Ubalozi wa Ujerumani na Wizara ya Maliasili na Utalii, na baadaye kufanyika utafiti wa kubainisha maeneo ya urithi wa utamaduni na historia yaliyopo katika Wilaya ya Pangani.

“Utafiti ulitusaibia kubainisha mambo mbalimbali, wananchi wengi walishiriki katika kutaja maeneo muhimu, kuibua vitu vya kizamani, kutoa picha na michoro, vyombo na mambo mengine mbalimbali ya kihitoria ambayo tuliyaweka kumbukumbu ambazo baada ya kupata baraka za Wilaya tulituma WMF na hatimaye tumepata heshima hii,” anasema.

Kwa kutambuliwa na shirika la WMF lililoanzishwa mwaka 1965 kwa lengo la kuhifadhi, kutunza na kuendeleza maeneo ya makumbusho ya urithi wa Utamaduni na mali kale, mji wa Pangani sasa unatangazwa na kutambuliwa rasmi kuwa ni sehemu ya Utalii wa kihistoria na kiutamaduni Duniani.

Friday, October 16, 2009

ANKO MO BLOGSPOT KUANDAA MISS PANGANI 2010


Kamati ya maandalizi ya Kumtafuta Miss Pangani 2010 imekutana leo katika ukumbi wa hoteli ya Koleprento uliopo Jijini tanga kwa ajili ya kujadili juu ya Mashindano hayo.
Muandaaji wa MissPangani , Mohammed Hammie kupitia kampuni ya Anko Mo Blogspot inayofanya shughulisha na maswala ya habari kwa njia ya Internet jijini Tanga- aliliambia gazeti hili kuwa maandalizi ya mashindano hayo yataendelea kufanyika mara kwa mara ili kufanikisha zoezi hilo ambalo litashirikisha warembo nane.

Kitongoji cha Miss Pangani ni kipya katika mchakato wa kusaka warembo mkoani hapa, ambapo kimeahidi kuleta mabadiliko katika sanaa ya urembo nchini Tanzania.

Vitongoji vyengine vilivyopewa dhamana ya kutoa warembo kwa ajili ya kumsaka Miss Tanga na hatimae Miss Tanzania ni pamoja kitongoji cha Ngamiani,Usagara,Chumbageni,College,Tanga city centre,Korogwe, na Lushoto
Hata hivyo Bw Mohammed amesema kuwa, kwa kuwa wilaya ya Pangani ni sehemu ya utalii mkoani Tanga. Hivyo kampuni yake imeona kuna haja kuchukua nafasi hiyo kutanga utalii wilayani humo kwa ajili ya kutoa fursa kwa wananchi wake kutambua thamani ya eneo lao.

Mashindano ya urembo yameonekana kukuwa kwa kasi mkoani Tanga lakini takribani miaka miwili kumekuwa na ukosefu wa kushika nafasi za juu kunako mashindano ya taifa ya miss Tanzania.

Hivi karibuni mrembo Glory Chuwa kutokea mkoani hapa amejikuta akishika nafasi za chini katika mtanange huo uliofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mbele ya kamati kuu ya Miss Pangani, Bw Mohammed ameongeza kuwa katika shindano hilo washiriki watakaofanya vizuri kuanzia nafasi ya kwanza hadi ya Tatu watapata tiketi ya kuungana na Washiriki wengine katika Kinyanganyiro cha Kumsaka Miss Tanga ambaye atapata nafasi ya kwenda kuuwakilisha mkoa katika mashindano ya taifa ambapo kilele chake kimemalizika hivi juzi na Miriam Gerlad kutokea Mwanza kuibuka kidedea.
Aidha katika shindano hilo ambalo litawashirikisha washiriki (8)mshindi wa wa kwanza atajinyakulia kitita cha Tsh 400,000 -Mshindi wa pili 250,000, na Mshindi wa tatu 150,000. Mshindi wa 4 na 5 watajinyakulia tsh 100,000 na Washindi wengine wa 6 na 8 tsh 50,000 kila mmoja.

Na Oscar Assenga, Tanga.

Wednesday, October 14, 2009

TANGA- MHHH!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! MKONO MTUPU HAULAMBWI!!

MKOA wa Mwanza umezidi kung'ara kupitia sanaa mchini baada ya mshiriki kutoka mkoani humo, Pascal Cassian kuibuka mshindi katika shindano la kusaka vipaji vya waimbaji chipukizi maarufu kama Bongo Star Search ambalo fainali zake zilifikia tamati jana usiku kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.


Kabla ya ushindi huo, tayari Mwanza ilikuwa imetwaa mara mbili mfululizo taji la urembo maarufu kama 'Miss Tanzania 2009' baada mwanadada Miriam Gerald kuibuka mshind.
Kutokana na ushindi huo, Cassian aliweza kutia kibindoni fedha taslimu sh25 milioni kutoka kwa waandaaji wa shindano Kampuni ya Benchmark Production .

Mbali na zawadi hiyo kutoka kwa waandaaji, mshindi huyo pia alikabidhiwa sh1,500,000 baada ya kuibuka mtunzi bora wa wimbo wa ukimwi sambamba na kitita kingine cha Sh500,000 kutoka duka la mavazi la Mariedo Botique ambalo pia lilidhamini shindano hilo.

Washindi wa mashindano hayo ni pamoja na Peter Msechu kutoka Kigoma, ambaye alishika nafasi ya pili- Kelvin Mbati nafasi ya tatu na Jackosn George kutokea Tanga. Mshiriki pekee wa kike Beatrice William alishika nafasi ya tano huku akipata zawadi ya mavazi kutoka Mariedo kama kifutio jasho.



Jackosn George- TANGA
Mkoa wa Tanga ulishindwa kung'ara kwenye mashindano ya Miss Tanzania yaliyofanyika mwaka huu, huku mshiriki wake Glory Chuwa akirudi nyumbani mikono mitupu. Jamani---- watanga mpooooo!!

Wednesday, October 7, 2009

HONGERA LADY JAY DEE- WEWE NDIO MKALI WA VIJIMAMBO VYA TANGA!!

Katika shindano la NANI MKALi lisilo la rasmi lililokuwa likiendeshwa na blog hii, likiwa linawapambanisha wanadada wanamuziki kutokea nchini Tanzania ambao ni Keisher, Kylnn, Jay dee na Nakaaya limefikia tamati leo na mwanadada Lady Jay Dee ameibuka kuwa mshindi.

Kura zilizopigwa na wadau wa blog hii ni 36, ambapoo Kylnn alipata kura 3 akiwa na asilimia 8 akifuatiwa na Nakaaya aliyetoka na kura 6 huku Keisher akishika nafasi ya tatu kwa kuwa na kura 9. Lady Jay Dee ndie ameibuka kidedea kwa kupata kura 20.

Jamani- mpambano huu haukuwa rasmi, ilikuwa ni katika kuwafanya wadau wa blog hii wapate chachu ya chakusema kupitia VIJIMAMBO VYA TANGA!! Kila la heri wajamaeni





Tuesday, October 6, 2009

HII NDIO PANGANI (PAN TOWN)- KARIBUNI SANA WAGENI

Jiwe hili la kumbukumbu pia- liliwekwa na wajerumani July 23 mwaka 1916. Lipo Pangani karibu na kivuko


Hili jiwe liliwekwa hapa miaka kumi baada ya Tanzania kupata uhuru wake kutoka kwa mkolini


Hii Lodge inapatikana Pangani- ipo barabara inayoelekea Halmashauri

Kituo cha utalii wilayani Pangani, Tanga kama kinavyoonekana katika picha


Moja kati ya majengo ambayo yanafanya mji wa Pangani kuwa kivutio kikubwa cha watalii duniani

Jengo jengine ambalo lipo katikati ya mji wa Pangani- watalii wengi huja kutazama majengo haya ya kihistoria

Hapa ni karibu na barabara ya Jamhuri, baadhi ya boti zikiwa zimepaki ufukweni

Anko Mo akiongea na simu wakati akiwa wilayani Pangani kikazi- Pangani ni mji mtulivu, huku ukipambwa na upepo mwanana wa bahari

Boti za kuvulia samaki zikiwa zimepaki ufukweni- sikuwa najua kama Pangani ipo karibu sana na Zanzibar!!! Watu huenda na kurudi

Boti na makumbi ya nazi baharini- Pangani husifika kwa kutoa nazi pia. Kuna mashamba ya minazi sana

Hapa panaitwa STOP OVER, moja ya bar maarufu wilayani Pangani ambayo watalii wengi hufika kwa ajili ya kula na kunywa!! Hapa ndipo nilipokuwa natoa menyu ya Pizza wadau

Pangani kwa majengo ya kihistoria usipimie- tazama jengo jengine hapa

Hapa panaitwa PANGADECO- klabu ya kujirusha siku za wikiend. Ipo baharini kabisaaaaa

Sio zote!!! Hii ni moja tu ya Beach zinazopatikana Pangani

Ukitaka kuamini Pangani inasifika kwa nazi tazama hiki kifuu- kipo baharini

Hii ndio anga ya Pangani wadau- KARIBUNI PANGANI







Monday, October 5, 2009

MR. EBBO AZUNGUMZIA KUHUSU BODA BODA


Msanii, ambaye pia ni prodicer maarufu hapa Tanga, Tanzania anayemiliki studio ya Motika Mr.Ebbo. Ametolewa kwenye tovuti ya BONGO CELEBRITY akizungumzia kuhusu boda boda.
Zaidi tembelea www.bongocelebrity.com

MFAHAMU ELIZABETH- MWAKILISHI PEKEE WA BIG BROTHER KUTOKA TANZANIA


Age- 22 Country- Tanzania Hometow-n Dar Es Salaam Occupation- TV Presenter / Actress
Biography Elizabeth has one sister, two brothers and she's a Miss Tanzania Top 10 finalist. She says the best part of her country to visit is Mount Kilimanjaro and the best thing about Tanzanians is their kind and positive nature. Elizabeth is a big Man United and Chicago Bulls fan and rates sleeping late and waking up too early as her bad habits. She loves dancing, needle work, cooking, watching TV and traveling - she has also lived in Hungary

FIESTA 2009 ONE LOVE- INAKUJA TANGA OKTOBA 24


Shangwe za FIESTA 2009 ONE LOVE zinakuja Tanga tarehe 24 Oktoba, siku ya Jumamosi. Wadau wa burudani kaeni tayari


Tamasha la fiesta safari hii linadhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Ltd huku kauli mbiu ya tamasha hilo ambalo hukutanisha maelfu ya watu kuwa ni One Love


Saturday, October 3, 2009

MIRIAM GERALD MISS TANZANIA 2009- KUTOKEA MWANZA KWA MARA YA PILI!!

Miriam Gerald pichani kutoka jiji la Mwanza ndiye Vodacom Miss Tanzania 2009 na pia ndiye Redds miss photogernic. Hongera sana dada Miriam kwa ushindi huo mnono ambao kiukweli ulionekana unastahili.
Washisriki wa shindano la Vodacom miss Tanzania 2009 wakiwa wamepozi na vazi la ufukweni usiku wa kuamkia leo

Wanyange wa Miss Tanzania 2009 wakipita kwa madaha kwa style ya Cat Walk

Miriam Gerald Miss Tanzania 2009!!