BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, September 7, 2011

KISIMA CHA MAJI CHAZINDULIWA LUSHOTO

Na Oscar Assenga,Lushoto.
MRADI wa Kisima cha maji katika kituo cha Afya Kangangai uliofadhiliwa na kikundi cha urafiki wa ujerumani na Tanzania (Deustsch Tanzanischer freundeskreis DTF)umezinduliwa juzi wilayani Lushoto.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo,Daktari Mfawidhi wa kituo hicho,Bakari Mavura alisema mradi huo ulianza mwaka 2008 kutokana na kuwepo kwa tatizo la maji katika kata ya Mwangoi tarafa ya Mlalo ambapo waliamua kukaa chini na kuanza kubuni mradi huo wakishirikiana na kamati ya afya ya kituo hicho.Mavura alisema baada ya kubuni mradi huo waliweza kuishirikisha jamii na kuweza kupata marafiki wa kikundi cha wajerumani na walipotoa mawazo na uweza kuyafanyia kazi.


Katika mradi huo shilingi milioni 16.2 zimetumika kati ya hizo shilingi milioni kumi laki mbili zimepatikana kutoka kwa kikundi cha urafiki na halmashauri ya wilaya ya Lushoto imechangia shilingi milioni sita.


Mavura alielaza maji hayo yatakuwa ni kwajili ya kituo hicho pamoja na watumishi wanaofanya kazi ambapo zaidi ya watumishi 10 pamoja na wananchi 22,000 watanufaika mradi huo pamoja na wagonjwa ambao watakwenda kupata matibabu kwenye kituo hicho cha afya cha Kangagai. "Wananchi wanapaswa kukitunza vizuri kisima hicho ili kuweza kuondokana na tatizo la maji "alisema Mavura.


Aidha aliongeza kuwa wanatarajiwa kuishirikisha jamii katika utunzji wa kisima ili kiweze kuwa endelevu.Alieleza kuwa licha ya kukamilika kwa kisima hicho wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa shillingi Millioni moja na laki nane kwa ajili ya kumalizia ufungaji wa mfumo wa maji safi na maji taka kwenye majengo ya kituo chicho.Mwisho.

No comments:

Post a Comment