BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, January 4, 2011

HISTORIA YA KANISA KUU, PAROKIA YA MT ANTONI WA PADUA, CHUMBAGENI TANGA 1893

Kanisa la Chumbageni lilianzishwa mwaka 1893. Kanisa hili lilijengwa wakati mmoja na bandari ya Tanga. Kipindi hiki mji wa Tanga ulikuwa mdogo sana na wakazi wake walikuwa wachache, hivyo Parokia hii iliwatosha watu wa mji wa Tanga.

Parokia ya Mtakatifu Anthony wa Padua, Chumbageni ilianzishwa na Mapadre wa Shirika la Roho Mtakatifu. Ilikuwa ni moja ya sehemu za Vikarieti ya Kilimanjaro. Jinsi muda ulivyoenda, na bidii ya Wamisionari, wakristu waliongezeka. Hawa ni baadhi ya Mapadre waliofanya kazi katika Parokia hii kipindi hicho: Pd. Francis Kennedy, Pd. James Cannolly, na Pd. O’Kane.

Wamisionari walifungua vigango mbalimbali kandokando ya barabara kuu za Tanga-Mombasa, Tanga-Pangani na Tanga-Moshi. Vilevile waliwahudumia wafungwa ambao walikuwa wamehukumiwa kunyongwa katika Gereza kuu la Maweni Tanga. Mheshimiwa Pd. Madden wakati fulani alihudumia wafungwa ishirini na tatu. Miaka ya 1960, Pd. Gerald Smith aliendeleza vigango vingine, navyo ni Mtakatifu Karoli Lwanga-Majani Mapana, Mtakatifu Josef Kagwa-Amboni, Mtakatifu Mathias Mulumba-Usagara, Mtakatifu Petro Saruji na Mtakatifu Gerald Pongwe. Vigango vingine ni Chote, Kisimatui, Kange, Kakindu, Mkembe na Jaribu Tena.

Mwaka 1948 Tanga pamoja na bandari yake ilifanywa kuwa Mkoa maalumu kwa viwanda vya Mkonge. Tukio hili liliifanya Tanga kukua na kufahamika zaidi, hata hivyo watu waliongezeka zaidi kwa ajili ya kufanyakazi katika mashamba ya mkonge na viwandani. Mwaka wa 1952 mji wa Tanga peke yake ulikuwa na wakazi waafrika wapatao 4,635, waarabu 1,029, waeshia 5,779 na wazungu 558.

Mwishoni mwa miaka ya sitini Pd. Gerard Smith ambaye pia kwa miaka 20 alikuwa paroko wa Mt. Antoni wa Padua alihakikisha kuwa vigango vya Mt. Antoni vinakuwa. Alijenga makanisa mbalimbali kama vile Mt. Charles Lwanga, Majani Mapana; Mt. Yosefu Kagwa, Amboni; Mt.. Mathias Mulumba, Usagara, kisha Mt. Peters Saruji Pongwe. Mwaka 1985 Pd. Smith alihamia na kuwa paroko Parokia ya Mt. Peter, Saruji. Akiwa paroko wa Mt. Petro Saruji Pongwe alijenga makanisa katika vigango vifuatavyo Mt. Gerard, Pongwe; Chote, Kisimatui, Kange, Kakindu, Mkembe and Jaribu Tena.Pia alijenga shule ya awali na nyumba ya masista Pongwe, Saruji, Majani Mapana Usagara and Kisimatui.

Pia alijenga Hostel ya wasichana katika parokia ya Mt. Anthony wa Padua, Chumbageni. Hostel hii daima imekuwa msaada mkubwa kwa wasichana wanaosoma elimu ya sekondari na vyuo Tanga mjni. Pia alijenga Go-down, kubwa Chumbageni ambalo linatumika hadi sasa.

Pd. Smith pia alikuwa ni Wakili wa Askofu wakati wa Mhashamu Askoufu Maurus Komba. Alipohamia parokia ya Mt. Petro Saruji Pongwe, Pd.. Martin Maganga akawa paroko mpya wa parokia ya Mt. Anton wa Padua, Chumbageni Tanga.

Pd. Gerard Smith alifariki mwaka 2001 na kuzikwa huko parokia Gare. Pd. Firmat Tarimo akawa paroko mpya katika parokia ya Mt. Petro Saruji Pongwe.

No comments:

Post a Comment