BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Saturday, August 20, 2011

SIMBA NDANI YA MKWAKWANI LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA

Klabu Ya Simba Ya Jijini Dar Es Salaam, Itautumia Uwanja Wa Mkwakwani Kuchezea Michezo Yake Ya Ligi Kuu Ya Vodacom Inayotarajia Kuanza Augosti 20 Mwaka Huu, Kufuatia Uwanja Wa Taifa Ambao Ulipanga Kutumia Michezo Yake Kufungwa Na Serikali Baada Ya Kuharibika Kwa Michezo Ya Ligi Ya Kagame.


Kwa Mujibu Wa Habari Kutoka Kwa Mwenyekiti Wa Matawi Ya Simba Mkoani Tanga Mbwana Msumari Ni Kwamba Simba Itautumia Uwanja Wa Mkwakwani Kwa Vile Wanachama Wa Klabu Hiyo Wa Mjini Tanga Wameomba Hivyo Klabu Hiyo Kukubali.


Msumari Ambaye Pia Ni Meneja Wa Uwanja Wa Mkwakwani Alisema Kuwa Amewasiliana Na Mwenyekiti Wa Klabu Hiyo Ismail Aden Rage Kwa Njia Ya Simu Asubuhi Akiwa Dodoma Amemwakikishia Kwamba Klabu Hiyo Itatumia Uwanja Wake.


"Amenihakikishia Kabisa Kwamba Watatumia Uwanja Wa Mkwakwani Badala Ya Arusha Ambako Walisema Walipokuwa Kwenye Tamasha La Simba Day Hawakupata Mapato Ya Kutosha Hivyo Kuona Ni Vema Wakahama Uwanja Huo Na Kuutumia Uwanja Wetu," Alisema Msumari Na Kuongeza Kwamba Katika Tamasha Hilo Simba Walipata Milioni 25 Tu.


Kama Itakuwa Hivyo, Mashabiki Wa Tanga Wataweza Kupata Uhondo Mkubwa Hasa Timu Hiyo Ikija Kupambana Na Mtani Wake Yanga Ambaye Juzi Wamempa Kipacho Cha Mabao 2-0, Tusubiri Tuone Na Blogu Yako Hii Italifuatilia Kwa Karibu Suala Hili Ili Liweze Kukujuza.

No comments:

Post a Comment