
Kwa Mujibu Wa Habari Kutoka Kwa Mwenyekiti Wa Matawi Ya Simba Mkoani Tanga Mbwana Msumari Ni Kwamba Simba Itautumia Uwanja Wa Mkwakwani Kwa Vile Wanachama Wa Klabu Hiyo Wa Mjini Tanga Wameomba Hivyo Klabu Hiyo Kukubali.
Msumari Ambaye Pia Ni Meneja Wa Uwanja Wa Mkwakwani Alisema Kuwa Amewasiliana Na Mwenyekiti Wa Klabu Hiyo Ismail Aden Rage Kwa Njia Ya Simu Asubuhi Akiwa Dodoma Amemwakikishia Kwamba Klabu Hiyo Itatumia Uwanja Wake.
"Amenihakikishia Kabisa Kwamba Watatumia Uwanja Wa Mkwakwani Badala Ya Arusha Ambako Walisema Walipokuwa Kwenye Tamasha La Simba Day Hawakupata Mapato Ya Kutosha Hivyo Kuona Ni Vema Wakahama Uwanja Huo Na Kuutumia Uwanja Wetu," Alisema Msumari Na Kuongeza Kwamba Katika Tamasha Hilo Simba Walipata Milioni 25 Tu.
Kama Itakuwa Hivyo, Mashabiki Wa Tanga Wataweza Kupata Uhondo Mkubwa Hasa Timu Hiyo Ikija Kupambana Na Mtani Wake Yanga Ambaye Juzi Wamempa Kipacho Cha Mabao 2-0, Tusubiri Tuone Na Blogu Yako Hii Italifuatilia Kwa Karibu Suala Hili Ili Liweze Kukujuza.
No comments:
Post a Comment