BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Saturday, August 13, 2011

COASTAL UNION YAITUMIA SALAM MTIBWA

KLABU ya Coastal Union imesema kuwa inatarajiwa kufanya vizuri katika mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu kati yao na Mtibwa Sugar ya Manungu Turiani katika mchezo unaotarajiwa kufanyika katika uwanja wa Mkwakwani agosti 20 mwaka huu.


Akizungumza na blog hii ,Mwenyekiti wa Klabu hiyo,Hemed Aurora amesema maandalizi ya mchezo huo hivi sasa yanaendelea vizuri ambapo timu hiyo inafanya mazoezi yake katika uwanja wa chuo cha Shinzu Mombasa chini ya kocha wao,Hafidhi Badru.

Aidha aliongeza kuwa uongozi wa Klabu hiyo unamshukuru mkuu wa mkoa wa Tanga,Said Kalembo ,mkuu wa wilaya ya Tanga pamoja na wabunge wa mkoa wa Tanga kwa kuwa msatri wa mbele kujitolea kuweza kuisaidia timu hiyo na kuhaidi kutowaangisha katika michezo mbalimbali ya ligi kuu msimu huu.

Aurora aliwataka wakazi wa mkoa wa Tanga pamoja na wadau wengine waliopo hapa nchini kujitokeza ili kuweza kuisadia timu hiyo ili iweze kufanya vizuri katika michuano ya ligi kuu na kuweza kurudisha heshima ya mkoa wa Tanga ambayo ilikuwa imepotea muda mrefu na hivi sasa imerudi tena.

2 comments:

  1. jitahidi ku update blog! habari zina miezi mitatu. unachosha wasomaji anko mo vp?

    ReplyDelete
  2. Very nice.
    http://www.urdukeeper.com/funny-sms

    ReplyDelete