BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, April 28, 2009

ABDUL AIBUKA KIDEDEA MAISHA PLUS!!

Mshiriki wa Maisha Plus Abdul, akikikabidhiwa pesa halali za Kitanzania shilinngi Million Kumi Taslimu kutoka kwa mdau aliyepewa jukumu la kutoa zawadi hiyo kunako usiku wa kuamkia jana wakati shindano hilo lilipofika tamati.

Katika siku hiyo ya mwisho washiriki kumi waliobakia walianza kutolewa kwa uchache wa kura walizokuwa wakipigiwa na watazamaji wa kituo cha televisheni cha TBC1. Washiriki walioingia kumi bora ni Boniface, Maulid, Upendo, Steve, Teddy, Charles, Moshy, Hamis (Kingunge), Modesta na Abdul. Baadaye wakatolewa Modesta aliyepata kura 620, Boniface (1,260) na Teddy (2,666). Wakafuata Kingunge (3,006), Moshi (3,828), Maulid (4,251) na Steve (5,700).


Ndipo wakabakia Upendo, Charles na Abdul. Akatolewa Upendo. Kazi ikabaki sasa kwa Abdul na Charles, marafiki wawili wakubwa katika kijiji. Na kama wengi walivyotabiri, Abdul aliondoka na Milioni 10 kwa kumbwaga Charles na wanakijiji wengine kwa kuwa na kura nyingi zaidi.


Washiriki hao walioingia kumi bora leo hii wanatembelea mbuga za wanyama Mikumi kwa ahadi waliyopewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwanguna, alipotembelea kijiji cha Maisha Plus wiki iliyopita.






No comments:

Post a Comment