BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, April 8, 2009

HUYU NDIE MKALI WA HIP HOP TANZANIA

Jina lake ni Albert Mangwea. Kwa mashabiki wa muziki wa kizazi kipya ukimuita Ngwea watakuelewa zaidi. Hivi majuzi alijishindia tuzo ya Kili Music Award kama Best Hip Hop Artist in Tanzania akiwashinda wakali wengine kama Fid Q, Chid Benz, Mwana FA na Witness.

Ngwea mwenyewe hakuwepo ukumbini wakati wa kutolewa kwa tuzo hizo na badala yake tuzo yake ilipokelewa na Meneja wake Tippo Athuman ambaye pia ndio mmiliki wa maduka ya Zizzou Fashions. Yawezekana Ngwea hakutokea kutokana na kubanwa na masomo pale Chuo cha Sanaa Bagamoyo ambako amekwenda kujifunza mengi katika sanaa.

Sasa wengi mmeshamsikia Ngwea. Ametoka mbali mpaka kufikia hapo alipo! Lakini wengine wamejiuliza,kwanini kashinda? Kwa wale mlionitumia swali hilo jibu langu ni fupi;sijui.Lakini naweza kuhisi.Mwaka huu zipo nyimbo kadhaa za Ngwea ambazo zimetamba na kujikita vizuri katika vichwa vya watu.Miongoni mwa nyimbo hizo ni ule wa Nipe Deal ambao ulitengenezwa katika style kutoka “Bondeni”. Kama hujausikia basi leo tunakupa nafasi hiyo.





No comments:

Post a Comment