
Ngwea mwenyewe hakuwepo ukumbini wakati wa kutolewa kwa tuzo hizo na badala yake tuzo yake ilipokelewa na Meneja wake Tippo Athuman ambaye pia ndio mmiliki wa maduka ya Zizzou Fashions. Yawezekana Ngwea hakutokea kutokana na kubanwa na masomo pale Chuo cha Sanaa Bagamoyo ambako amekwenda kujifunza mengi katika sanaa.
Sasa wengi mmeshamsikia Ngwea. Ametoka mbali mpaka kufikia hapo alipo! Lakini wengine wamejiuliza,kwanini kashinda? Kwa wale mlionitumia swali hilo jibu langu ni fupi;sijui.Lakini naweza kuhisi.Mwaka huu zipo nyimbo kadhaa za Ngwea ambazo zimetamba na kujikita vizuri katika vichwa vya watu.Miongoni mwa nyimbo hizo ni ule wa Nipe Deal ambao ulitengenezwa katika style kutoka “Bondeni”. Kama hujausikia basi leo tunakupa nafasi hiyo.
No comments:
Post a Comment