BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, April 24, 2009

BONGO STAR SEARCH DAR NI JUMAMOSI NA JUMAPILI.

Mkurugenzi wa Benchmark waandaaji wa Bongo Star Seach Ritah Paulsen (Pichani) akizungumza na wanahabari katika mako makuu ya Vodacom jengo la PPF Tower wakati alipoongea na wanahabari kuelezea juu ya shindano la BSS linalotarajiwa kufanyika jumamosi na jumapili mkoani Dar es alaam kulia ni Nector Foya meneja mawasiliano Vodacom.
Shindano la kutafuta wawakilishi wa mkoa wa Dar es alaam katika shindano la BSS 2009 litafanyika kuanzia jumamosi mpaka jumapili wiki hii katika ukumbi wa New World Cinema ambapo zaidi ya washiriki wapatao 2000 wanatarajia kujitokeza ambapo mshindi wa mwaka huu anatarajiwa kuondoka na zaidi ya milioni 15 ambazo mshindi wa mwaka jana alijishindia.
Kampuni ya simu za mkononi Vodacom ni wadhamini wa shindano hilo linaloratibiwa na kampuni ya Benchmark Production ambapo zaidi ya vijana 8000 wameshiriki katika mchujo huo mikoani kote ambako shindano hilo limefanyika na vijana 35 wameingia raundi ya pili ya shindano hilo vijana walishinda mikoani na mikoa yao ni kama ifuatavyo
.....Dodoma ni: Mwapwani Yahaya, Waziri Salum, Kamwitani Malili, Sarafina Mshindo na Joma Malick.
Mwanza ni Beatrice Wiliam, Haji Ramadhani, Monica Amon na Paschal Casian Tabora ni: Leah Julius, Rajabu Miraji na Kayombe Mrisho
Mtwara ni: Jamilah Yusuf, Josephat Obedi, Nicolaus Samuel na Ally Mtambo Mbeya ni: Ndigwabo Ahazi, Anitha Jackson, Issa Ahmed na Mosses Mwaifele
Arusha ni: Brandy Francis Amani Lisu, Sarah Mbwambo na Frola Ezekiel
Tanga ni: Jumanne Charles, Njele Juma, Jackson George na Marck Kauli
Kigoma ni: Peter J Msechu na Kauke Adam na mwisho ni Zanzibar ambako wamepatikana Mohamed Omary, Yusuph Mina, Aboubakar Pishak na Kelvin Stephen wasindi hawa wataungana wa watakaopatikana kutoka mkoa wa Dar es alaam na kuingia mzunguko wa pili wa mchujo huo.

No comments:

Post a Comment