BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, April 20, 2009

MAISHA PLUS MAANA YAKE NINI..?


Waswahili wanasema Njaa kipimo cha akili, Kila kukicha watu wanazidi kubuni namna ya kukabiriana na maisha ya kila siku, na hii imekuwa changamoto kwani maisha ya kutegemea kuajiriwa kwa sasa hakuna na kila mmoja anatakiwa kuwaza jinsi gani atajiajiri. Changamoto hii ndio matunda ya vitu kama Maisha Plus.



Maisha Plus ni nini?Ni shindano la uhalisia ( Reality Show) ambayo halijawahi kufanyika barani Afrika, ni shindalo linalo ‘reflect’maisha halisi ya Mtanzania hasa vijana. Shindano hili lilianza kuonyeshwa kupitia kituo cha TBC1 March 1,2009, Mchakato wa kuwatafuta washiriki 18 ulianza Novemba mwaka 2008 katika kanda nane za Tanzania bara na Visiwani.



Lengo la Maisha Plus ni nini?Kuwawezesha vijana kujitambuaKuwapa ujuzi kwa kuwafundisha vitu mbalimbali kupitia semina na mafunzo mbalimbali wanayopewa.Kuendeleza vipaji vyaoKuwapa mtazamo chanya wa maisha watazamaji na washiriki.Kubadilishana utamaduniKuburudisha watazamaji. Malengo ya badae ya Maisha PlusMwezi wa saba season II ya shindano hili itaanza na safari hii usaili utafanyika katika mikoa yote ya Tanzania.



Season III ya shindano hili itajumuisha nchi zote za Afrika Mashariki ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi n.k. Waandaaji wa shindano hili ni kampuni ya dmb Inc inayomilikiwa na Masoud Kipanya, Fransis Bonda na David Sevuri. Kipindi hutengenezwa na kampuni ya True Vision Production.



Regards

Julieth Kulangwa Media

Media Coordinator
0717 551355

No comments:

Post a Comment