BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, April 28, 2009

FEROOZ KULETA SOKONI SAUTI NA VYOMBO MAY 4


Msanii wa muziki wa kizazi kipya a.k.a Bongo Fleva Ferooz Mrisho anatarajia kuingiza albamu yake mpya sokoni iitwayo sauti na vyombo may 4,Albamu hiyo iliyozinduliwa kwa kishindo ndani ya ukumbi wa diamond jubilee ina jumla ya nyimbo kumi

Ferooz ameiambia Jiachie leo kuwa albamu hiyo itasambazwa na kampuni ya usambazaji hapa jijini ya GMC,na kuwa albamu hiyo itapatikana kila sehemu ikiwemo na mikoani,hivyo wapenzi wa muziki wa kizazi kipya wajitokeze kwa wingi kuinunua albamu hiyo yenye kila aina ya ladha.
Albamu hiyo imerekodiwa na prodyuza P-Funk a.k.a Majani ndani ya Bongo Records,aidha amezitaja nyimbo zilizomo ndani ya albam hiyo kuwa ni sauti na vyombo, Kwa Kupaa, Mr.Policeman ambayo inatamba kwa sasa kwenye vituo vingi vya redio, Receiption na nyinginezo.

Katika albamu hiyo amewashirikisha wasanii kibao akiwemo Matonya, Maunda Zorro, Durry Sykes pamoja na Chid Benz ili kuifanya iwe bomba na yenye ladha mchanhanyiko.

No comments:

Post a Comment