BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Sunday, April 5, 2009

UNTOUCHABLE DJ'S- KITOVU CHA BURUDANI TANZANIA

Mshkaji anaitwa William J Lisingu, ni muanzilishi wa Untouchable Dj's ambayo kwa hivi karibuni imekuwa ikija juu sana kwenye anga za burudani ukizingatia ubunifu aliokuwa nao jamaa pamoja na ujuzi.

Untouchable kwa ujumla ilianzia jijini Tanga, takribani miaka miwili iliyopita wakati William akiwa na redio Mwambao fm. Ni ngumu kuelezea wazo la ujio wake wa Untouchable alikolipata, lakini kwa undani zaidi utagundua juu ya hisia kali za muziki ambazo jamaa anazo.


Wakati anapiga story na Blog hii, Will kamwe huwezi kumdhania kwamba anaweza kufanya mambo makubwa kama ambavyo tayari ameyafanya hadi sasa kupitia Untouchable.

Tayari Untouchable umemuwezesha kuwa na mradi wa fulana ambazo unawakilisha nembo ( LOGO ) za Untouchable. Awali wakati naziona fulana zake kwa mmoja wa watangazai mahiri wa Mwambao fm Bra-A, nilivutiwa sana.

Nikaona kuna haja ya kuwaletea kitu kizuri wadau wangu wote ambao wanashiriki kwa pamoja kuhakikisha Blog hii inapiga hatua. Kiukweli, ukizungumzia Dj's ambao wanafanya vizuri jijini Tanga na hata Tanzania kwa ujumla- basi hutasita kutaja Untouchable Dj's ambao kiongozi wake ni William J Lusingu. Kama ulipata bahati ya kutazama video ya wimbo wa Angie ambao alimshirikisha Chid Benz, ngoma inaitwa WEWE- Utakubali kwa ninachosema hapa
.
Big sana kaka and keep it up!!!!




No comments:

Post a Comment