BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, July 13, 2010

BENEDICT KAGUO, OSCAR ASSENGA WAPEWA TUZO.

MWANDISHI wa gazeti la Majira Mtangazaji wa Radio Mwambao Fm ya jijini Tanga, Benedict Kaguo 'Father K' kulia akipokea tuzo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Five Brothers Entertainment Nassor Makau ikiwa ni kuthamini mchango wake katika kufanikisha Mashindano ya Miss Tanga yaliyoandaliwa na Kampuni hiyo.

Hafla hiyo fupi iliyofanyika juzi kwenye makao makuu ya Kampuni hiyo yaliyopo Ring street hapa jijini Tanga. Shindano la kumsaka mnyange wa Miss Tanga yalifikia tamati kwenye hoteli ya Tanga Beach Resort ambapo Anna Kiwambo aliibuka kidedea.

Mwandishi wa habari wa gazeti la Bingwa na mtangazaji wa Mwambao Fm Radio Oscar Assenga akikabidhiwa cheti cha ushiriki na kufanikisha mashindano ya Miss Tanga 2010 kutoka kwa Mkurugenzi wa Five Brothers Entertainment Nassor Makao ofisini kwake kwenye hafla hiyo ilifanyika na kuhudhiriwa na watu wachache

Mkurugenzi wa Kampuni ya Five Brothers Entertainment Nassor Makau akimkabidhi cheti cha ushiriki Mwaandaaji wa Miss Usagara 2010 Asia Msangi katika makao makuu ya Kampuni hiyo Mtaa wa Ring jijini Tanga.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Five Brothers Entertainment Nassor Makau katikati akijadiliana jambo na waandishi mahiri wa sanaa ya urembo Benedict Kaguo kushoto na Oscar Assenga Mwandishi wa New Habari Co-operation wachapishaji wa gazeti la Bingwa nje ya ofisi ya kampuni hiyo mtaa wa Ring jijini Tanga.

No comments:

Post a Comment