BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, July 21, 2010

BREAKING NEWS!!!!!! WAGOSI WA KAYA WATEMANA!!

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya hapa nchini kutoka katika kundi la Wagosi wa Kaya lenye makazi yake jijini hapa John Simba "Dr.John"amesema kuwa kundi hilo limekufa kutokana na msanii mwenzie Fredy Maliki "Mkoloni"Kujiingiza katika masuala ya Kisiasa hapa nchini kwa kujiunga katika chama cha chadema.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi,Dr.John alisema kuwa kwa sasa kila kitu ambacho kitakuwa kinafanyika katika kundi hilo ikiwa ni pamoja na kutoa nyimbo na kuimba itakuwa ni kama maagizo ya Chama cha Chadema.

Dr.John alisema kuwa kwa sasa hivi anaangalia mambo mengine ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kuwainua wasanii chipukizi katika mkoa wa Tanga ikiwemo mwanae mwenyewe Josephine "Phine".

Aidha alisema kuwa mikakati yake kwa sasa ni kufanya kazi peke yake kama solo artist kwa kushirikiana na wasanii mbalimbali kutoka hapa nchini. "Ule urafiki uliokuwepo kati ya mkoloni na mimi upo pale pale lakini sio kwenye kazi "alisema Dr.John.

Aidha alitoa wito kwa wasanii chipukizi wa mziki wa kizazi kuangalia muziki na mambo mengine na sio wang"ang"anie kwenye muziku kueleza kuwa kwa sasa wanatakiwa kuandika mashairi ambayo yana ujumbe kwenye jamii na sio mapenzi.

No comments:

Post a Comment