BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, July 26, 2010

'NO FEATURING KWA SASA'- Q CHILLAH!

Msanii kutokea mkoani Tanga Aboubakar Shaban Katwila a.k.a Q Chillah ambaye anafanya vizuri kunako anga za muziki wa bongo flava hapa nchini, amsema kuwa hivi sasa hataki tena kusikia habari za kushirikishwa (Featuring) katika ngoma za wasanii wengine. Chillah aliongeza kwamba ameamua kufiikia uwamuzi huo kwa sababu yupo tait na ujio wake mpya baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu.
"Hivi sasa nipo kwenye mishemishe za kwenda levo nyengine, sihitaji kushirikishwa na msanii yeyote yule kwani nimeshawasaidia sana, kilichopo mble yangu muda huu ni kuangalia jinsi ya kuupeleka muziki wangu mbali" alisema Chillah.

Akiwa ametoka chimbo n ngoma yake ya 'Saba Mara Sabini' ambayo inafanya vizuri kila kukicha kunako redio tofauti tofauti nchini....msanii huyo pia hakusita kutaja jina la albamu yake mpya ambayo ni "A SING OF MATURENESS" kwa kuwa albamu hiyo imeshakamilika na kinachofuata ni video za ngoma kadhaa kabla ya kuwapelekea mahabiki wake.

No comments:

Post a Comment