BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, July 16, 2010

TOVUTI YA MKOA WA TANGA HADI LINI...!????

Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa umekuwa katika michango mbalimbali ya kukuza matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEKNOHAMA) katika ngazi ya mkoa na halmashauri za wilaya kwa lengo la kujenga serikali mtandao (e-government). Kuimarika kwa matumizi haya ya (TEKNOHAMA) kutasaidia sana kurahisisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi katika shughuli mbalimbali za kila siku kati ya serikali (mkoa), halmashauri za wilaya na wadau wengine.

Moja ya vitu ilivyoshughulikia ni uanzishwaji wa Tovuti za Mikoa kwa Mikoa yote ya Tanzania bara. Ambapo tovuti hizi zimezinduliwa rasmi na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda tarehe 19 Februari 2009 halfla hiyo imefanyika Ofisi za Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro

Wasi wasi wangu ni kwamba hadi sasa mkoa wa Tanga hauna tovuti tangu waziri mkuu Mizengo Pinda atangaze nia yake hiyo Februari 2009. Pichani mkoa wa Morogoro ukiwa tayari umepatiwa tovuti yake....humo kuna kila kitu kinachohusu mkoa huo. Sisi Tanga hadi lini..>>????

Pichani tovuti ya mkoa wa Kagera, tovuti ya mkoa wa Tabora na tovuti ya mkoa wa Dar es salaam. Tunaomba mkuu wa mkoa wa Tanga Saidi Kalembo ulitazame hili. Mkoa wako hadi sasa haujapata tovuti.

No comments:

Post a Comment