BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, November 26, 2009

MIRIAM AANZA VIZURI MISS WORLD HUKO AFRIKA KUSINI


Miss Tanzania 2009, Miriam Gerald ambaye yupo Afrika Kusini katika kuliwakilisha Taifa kwenye mashindano makubwa kabisa ya Miss World usiku wa jana alifanikiwa kuingia Fainali ya vazi la ufukweni baada ya kuingia kwenye 40 bora katika hatua za awali za mashindano hayo makubwa, fainali ambazo zinataraji kufanyika usiku wa leo.

Kwa mujibu wa kanuni za mashindano ya dunia, mrembo atakayefanikiwa kuibuka mshindi katika taji hilo la mavazi ya ufukweni anakuwa tayari amepata tiketi ya kuingia katika hatua ya 20 Bora ya shindano kubwa la kumtafuta malkia wa dunia.

Mkurugenzi wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga, alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa, Miriam amepata nafasi hiyo ambayo imeshuhudia warembo wengine 80 wakichujwa.

Lundenga alisema kuwa hiyo ni moja ya mafanikio kwa mwakilishi huyo wa nchi kwa sababu ameonekana kuwa ni bora katika vazi hilo.

Alisema pia wanaomba Miriam aendelee kufanya vizuri leo na kupata nafasi ya kuingia hatua ya 20 Bora ya fainali ya mashindano hayo ambayo imepangwa kufanyika Desemba 12 katika jiji la Johannesburg.

Alisema kuwa warembo wote wanaoshinda katika mataji madogo madogo, wanaingia moja kwa moja kwenye hatua hiyo ya 20 Bora ambayo inakuwa rahisi zaidi kushinda taji la Miss World.

Mrembo mwingine aliyeingia katika hatua ya 20 Bora ya mashindano hayo ni kutoka Japan ambaye aliibuka kidedea katika taji la michezo. Mrembo huyo ambaye aliwahi kushiriki katika michuano ya Olimpiki, aliwashinda wenzake katika mbio fupi.

Warembo hao pia walishindana katika kupiga penati.


No comments:

Post a Comment