BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Saturday, November 28, 2009

DAZ NUNDAZ KURUDI TENA KWENYE RAMANI YA BONGO FLAVA!!

Kama unalikumbuka ni kundi lililowahi kutamba sana miaka ya 90 ambalo lilikuwa likiundwa na wasanii nyota wa muziki wa kizazi kipya wawili Ferouz na Daz Baba ambao ndio walichangia kwa kiasi kikubwa kundi hilo kujipatia umaarufu wametangaza rasmi kumaliza tofauti zao.
Wakizungumza kwa pamoja, wasanii hao walidai kuwa kwa sasa wako tayari kufanya kazi pamoja na hata kulirejesha upya kundi lao la Daznundaz.

“Unajua tofauti zetu zilikuwa ndogo tu, ingawa vyombo vya habari vilichangia sana kuzikuza,hivi sasa tuko pamoja na mimi niko tayari kufanyakazi na mshkaji Daz Baba,” alieleza Ferouz, ambaye anaonekana kufulia kinoma kimuziki na kimaisha tofauti na alipokuwa na kundi la Daz nundaz.

“Mimi na msanii mwenzangu Larumba ambaye tulikuwa pamoja tulianzisha kundi letu la Tanzaniano , lakini hili halituzuii kukaa pamoja na Ferouz na washkaji wetu wengine ili kulirejesha kundi letu la Daznundaz. Ferouz ni mtu wangu na niko tayari kufanya naye kazi,” alisema Daz Mwalimu .
Kundi la Daznundaz lilisambaratika siku chache baada ya baadhi ya wasanii wake wakiongozwa na Ferouz kumtimua kundini msanii mwenzao Dazbaba kwa madai kuwa alikuwa akitumia dawa za kulevya ‘teja.’

Kundi hilo lilipata kutamba na nyimbo zake kali kama vile; Maji ya shingo, Kamanda, Barua, Jahaz la Daz na nyingine





No comments:

Post a Comment