
Wakizungumza kwa pamoja, wasanii hao walidai kuwa kwa sasa wako tayari kufanya kazi pamoja na hata kulirejesha upya kundi lao la Daznundaz.

“Mimi na msanii mwenzangu Larumba ambaye tulikuwa pamoja tulianzisha kundi letu la Tanzaniano , lakini hili halituzuii kukaa pamoja na Ferouz na washkaji wetu wengine ili kulirejesha kundi letu la Daznundaz. Ferouz ni mtu wangu na niko tayari kufanya naye kazi,” alisema Daz Mwalimu .

Kundi hilo lilipata kutamba na nyimbo zake kali kama vile; Maji ya shingo, Kamanda, Barua, Jahaz la Daz na nyingine
No comments:
Post a Comment