BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, November 11, 2009

MR PRESIDENT YA ROMA MPANGO MZIMA REDIONI!!


Msanii kutoka jijini Tanga, Tanzania ROMA ama Rymes Of Magic Attraction ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la MR PRESIDENT. Roma ambaye alishawahi kutamba na ngoma ya TANZANIA iliyovuma karibu kila nchi na Afrika Mashariki kwa ujumla amekuja na ujio mpya uliowaacha midomo wazi mashabiki wa muziki wa bongo flava.

Akizungumza na Blog hii, msanii huyo amesema kuwa ngoma ya MR PRESIDENT ilimchukua muda hadi kuifanikisha toka alipotangaza kwani alishafanya kazi producer Duke wa M- Lab Record na ngoma kukamilika. Lakini hata hivyo msanii huyo aliahirisha kui'riliz ngoma hiyo na kuamua kufanya kazi na J Marder wa Tongwe Record iliyopo Masaki jijini Dar Es Salaam.


Roma akipiga story na Anko Mo, alitabanaisha kuwa alichonga na J Marder na kupenda kufanya nae kazi ya MR PRESIDENT- kama moja ya hatua ya kusonga mbele katika maendeleo ya muziki wa bongo flava nchini Tanzania.

Mkali huyo wa Hip Hop kutokea Tanga, Tanzania ameongeza kuwa hadi sasa yupo Tongwe Record chini ya mmiliki wake J Marder na tayari kuna ngoma nyengine anazitayarisha kwa ajili ya kutoka na albamu hapo baadae.


Roma amewataja baadhi ya wasanii ambao anatarajia kuwapa shavu kwenye ngoma zake mpya ni pamoja na Izzo B na Nick Wa Pili ambazo ataziachia very soon.

Mchizi wangu wa ukweli alimalizia kuwa, bado yupo na YUDDI ambaye ni Mixing Producer wake aliyefanya ngoma ya TANZANIA. Mnoma alizitaja baadhi ya redio ambazo hadi sasa zinagonga ngoma yake kuwa ni Mwambao Fm ya Tanga, Breez Fm, Clouds Fm, Times Fm, E.A Radio, Coconut Fm, Magic Fm pia imefika Mtwara, tabora na karibu nchini nzima.


Dizaini mnoma kama amebanwa na skuli, bt amesema kuwa yupo mbioni katika mpango mzima wa albamu punde tu atapokuwa free.

No comments:

Post a Comment