Msanii kutokea mkoani Tanga Aboubakar Shaban Katwila a.k.a Q Chillah ambaye anafanya vizuri kunako anga za muziki wa bongo flava hapa nchini, amsema kuwa hivi sasa hataki tena kusikia habari za kushirikishwa (Featuring) katika ngoma za wasanii wengine. Chillah aliongeza kwamba ameamua kufiikia uwamuzi huo kwa sababu yupo tait na ujio wake mpya baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu.
Akiwa ametoka chimbo n ngoma yake ya 'Saba Mara Sabini' ambayo inafanya vizuri kila kukicha kunako redio tofauti tofauti nchini....msanii huyo pia hakusita kutaja jina la albamu yake mpya ambayo ni "A SING OF MATURENESS" kwa kuwa albamu hiyo imeshakamilika na kinachofuata ni video za ngoma kadhaa kabla ya kuwapelekea mahabiki wake.










































