
Siku hii ilichaguliwa rasmi mwaka 1988 wakati wa Mkutano wa Dunia wa Mawaziri wa Afya Kuhusu Mpango wa Kuzuia Ukimwi. Kuanzia hapo siku hii imekuwa ikikumbukwa rasmi na serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, na wanaharakati.
Toka mwaka 1988 hadi 2004, Siku ya Ukimwi Duniani ilikuwa ikiratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Ukimwi (UNAIDS). Mwaka 2005 UNAIDS ililipa shirika lisilo la kiserikali la Kampeni ya Ukimwi Duniani (the World AIDS Campaign) wajibu wa kuratibu siku hii.
Kila mwaka siku hii hukumbukwa kwa ujumbe maalum. Ujumbe wa mwaka 2005 ni Zuia Ukimwi: Timiza Ahadi. Ujumbe huu utatumika hadi mwaka huu wa 2010. KAPIME UJUE AFYA YAKO EWE MDAU MTANZANIA, EWE MDAU WA 'VIJIMAMBO VYA TANGA'!
No comments:
Post a Comment