BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, December 21, 2010

PANGANI YATAJWA KUWA MOJA YA KIVUTIO CHA UTALII DUNIANI!

SHIRIKA la Makumbusho Duniani la World Monuments Fund (WMF) limeutambua na kuupa heshima mji wa Pangani kuwa mmoja wa miji mikongwe ya kihistoria na urithi wa Utamaduni duniani.

Mkurugenzi wa shirika la Uzima kwa Sanaa (UZIKWASA) la mjini Pangani, Dkt. Vera Pieroth alisema mjini huo wa kihistoria umetajwa kuwa ni miongoni mwa miji 93 ya urithi wa Utamaduni iliyopo katika nchi 47 duniani zinazotambuliwa na shirika hilo.

Vera alisema kuwa uamuzi wa kutunuku mji huo heshima hiyo umetangazwa hivi karibuni na Rais wa WMF, Bonnie Burnham, jijini New York, Marekani ambapo mji wa Pangani umekuwa kati ya maeneo manne katika bara la Afrika ambayo imepewa hadhi na WMF.

“Kuteuliwa kwa mji wa Pangani ni faraja kubwa kwa watu wa hapa na shirika letu la UZIKWASA. Tangu mwaka 2007 shirika letu kwa kushirikia na Halmashauri ya Wilaya ya Pangani na Kamati za kijamii tumekuwa kutangaza vivutio vya kihistoria vya mji hapa na tunafurahi sasa juhudi za pamoja ambazo zimeleta matunda mazuri,” alisema.

Miaka miwili iliyopita UZIKWASA kwa kushirikiana na Idara ya mambo ya Kale iliendesha kongamano la kujadili jinsi ya kuhifadhi na kutanga Mali kale na urithi wa Utamaduni wa Pangani, lililofadhiliwa na Ubalozi wa Ujerumani na Wizara ya Maliasili na Utalii, na baadaye kufanyika utafiti wa kubainisha maeneo ya urithi wa utamaduni na historia yaliyopo katika Wilaya ya Pangani.

“Utafiti ulitusaibia kubainisha mambo mbalimbali, wananchi wengi walishiriki katika kutaja maeneo muhimu, kuibua vitu vya kizamani, kutoa picha na michoro, vyombo na mambo mengine mbalimbali ya kihitoria ambayo tuliyaweka kumbukumbu ambazo baada ya kupata baraka za Wilaya tulituma WMF na hatimaye tumepata heshima hii,” anasema.

Kwa kutambuliwa na shirika la WMF lililoanzishwa mwaka 1965 kwa lengo la kuhifadhi, kutunza na kuendeleza maeneo ya makumbusho ya urithi wa Utamaduni na mali kale, mji wa Pangani sasa unatangazwa na kutambuliwa rasmi kuwa ni sehemu ya Utalii wa kihistoria na kiutamaduni Duniani.

No comments:

Post a Comment