BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, December 23, 2009

AY ATOA SOMO LA FUNGA MWAKA!!!


Nyota wa hip hop nchini AY amewapa somo kuwa mwaka 2010 utakuwa na maana kubwa katika muziki wa kizazi kipya kama wasanii wa hapa nchini wataamka na kusaka mafanikio nje ya mipaka.

"Wasanii wengi hapa nchini wanaonekana kuridhika kushindana wenyewe kwa wenyewe humu nchini," alisema AY

Haya si maendeleo, ni sawa na mtu anayekaa ndani mwake na kuona kuwa TV ya nchi 14 aliyonayo ni kubwa ya kutosha na makochi aliyonayo ni mazuri kabisa... anaona hivyo kwasababu hajatoka nje kuona changamoto tofauti.


Ndio maana nasema wasanii nchini tusiridhike kufanya shoo hapa Dar es salaam ama kusafiri kufanya shoo za Kigoma, na Arusha tu.
"Hii inatudumaza kimawazo kwasababu mawazo yetu mengi yanafanana. Tujaribu kutoka nje. Tujaribu kusonga mbele tusikubali kuishia shule ya msingi. Tuwe na mawazo ya kusoma sekondari hadi vyuo vikuu.


No comments:

Post a Comment