BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, December 9, 2009

KILA LA KHERI VICTORIA MARTINE- WATANGA WOTE WAPO PAMOJA NA WEWE

Aliyekuwa mnyange Miss Tanga 2007, Victoria Martine amekuwa ni mmoja kati ya warembo wawili watakaoiwakilisha Tanzania kunako mashindano ya urembo ya Afrika Mashariki kwa mwaka huu, yanayotarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa ya tarehe 18.

Victoria Martine (20) na Juliet William (19) walichaguliwa kufuatia mchakato uliochukua takribani miezi mitatu huku ukiendeshwa na kamati maalum iliyochaguliwa na waandaaji wa Miss East Africa ambapo kamati hiyo ilikutana na warembo zaidi ya 150 kutoka sehemu mbalimbali Nchini ili kupata wawakilishi wawili wanaofaa kuiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo ya urembo.



Victoria Martine, ni mrembo maarufu hapa Nchini ambae anajishughulisha na mambo ya mitindo, na pia amewahi kushinda tuzo ya reds fashion ambassador kwa mwaka 2007 Juliet William, yeye ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo cha USIU cha jijini Nairobi, na pia ni mshindi wa tatu wa mashindano ya Miss Tanzania kwa mwaka huu.



Warembo wote wana viwango vinavyofaa kushiriki katika mashindano hayo makubwa katika ukanda huu wa Africa.Mashindano ya Miss East Africa 2009ambayo yanasubiliwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa mambo ya urembo barani Afrika yatafanyika tarehe 18 mwezi huu katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam, na yatawashirikisha warembo kutoka Nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Ethiopia, Mauritius, Eritrea, na wenyeji Tanzania.



Mashindano hayo yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Limited ya Jijini Dar es salaam, na kudhaminiwa na Kunduchi Beach Hotel & Resort, EATV, CMC Automobile, na AKO Catering Services.







No comments:

Post a Comment