BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Sunday, December 20, 2009

SIO ISHU KUWA'DIS WALIOKUTOA- ASEMA AFANDE SELE

Mfalme wa Rhymes nchini, Seleman Msindi (Afande Sele) amewataka wasanii wanaochipukia na kukubalika wasijisahau na badala yeke warudishe fadhila kwa waliochangia mafanikio yao.

Afande aliyachana hayo huku kusisitiza kuwa ni upuuzi wa hali ya juu kwa msanii kuwaimba vibaya maprodyuza huku wakifahamu fika kwamba wahusika hawawezi kujibu. Kama hiyo haitoshi, Afande Sele amebainisha kwamba usanii huo unarudisha nyuma muziki wa kizai kipya.

"Tunatakiwa kuachana na ugomvi na kumkimbia shetani ili mambo yetu yawe mazuri," anasema afande. Anasema awali wasani walikuwa na tabia ya kuimba wapenzi wao kwa kuwataja majina lakini baada ya kukemea, tabia hiyo imekoma.


"Kinachotakiwa ni kuangalia matatizo yanayoigharimu nchi na kuyaibua katika tungo ili kusaidia maendeleo. "Najua wasanii wa Bongo hawataki kuambiwa ukweli ingawa ndivyo ilivyo, mfano ukimwambia msanii fulani anaimba kama fulani, hapo litatokea bifu wakati unatakiwa kukubali uhalisia.

(Huyu ni Afande Sele jamani)
Mfano mimi nafanana na Sugu katika uimbaji kwa kuwa ndipo nilipotokea siwezi kukataa,"alisema msanii huyo anayeuwakilisha vyema mkoa wake wa Morogoro na ambaye yupo katika hatua za mwisho kuachia track mpya itakayoitwa 'Kingdom', ambayo imegongwa studio za Bongo Records.





No comments:

Post a Comment