BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, December 15, 2009

UNAWAJUA GREAT THINKERS WALIOTAMBA KUNAKO FASIHI ANDISHI NCHINI TANZANIA..??


(HAMMIE RAJAB)

Wadau wa blog na wale wapenda kusoma vitabu vya GREAT THINKERS ambao wameweka historia katika kutumia fasihi andishi nchini Tanzania. Kama kuna mtu anaweza kunisaidia kupata mtiririko wa vitabu hivi tafadhali awasiliane na mimi kwani ni HAZINA ILIYOJIFICHA.

Nimeona kuna haja ya kuwa na libraly ya vitabu hivi ili kutunza na kuenzi utamaduni wa mali zetu kupitia wahasisi hawa ambao hawatasahaulika/japokuwa wengine wapo mbele ya haki na wengine bado wangali hai.

Sitasahau kipindi kile upo darasani mwalimu anafundisha, mzee umeinamia kwa chini unaperuzi SANDA YA JAMBAZI- Maliki Mbowe alivyolitingisha jiji la Morogoro!!! Yeyote aliye na copy ya moja ya vitabu hivi
atakuwa amenisaidia sana...........

(FARAJI KATALAMBULA)

Ila mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Eddie Ganzel mahari pema peponi kwa alifanikiwa KUMSAKA HAYAWANI, moja kati ya watu ambao nilikuwa napenda sana vitabu vyao.
Pia Nilipokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kifo cha mwandishi maarufu, Ben Mtobwa ama 'Joram Kiango'. Taifa lilipoteza kinara mwingine wa kutumia fasihi andishi kufichua masuala mazito yaliyoigubika jamii yetu.

Alitumia ipasavyo'mtutu wa kalamu' kufichua uzandiki na ufisadi katika jamii. Lakini upeo wa mwanadamu una kikomo.

(BEN MTOBWA)
Nawasihi tumpe mtunzi huyu 'ZAWADI YA USHINDI' kwa kusoma kwa undani vitabu vyake ili tutambue ni nini hasa amejaribu kutufunulia 'NYUMA YA MAPAZIA' ya jamii yetu iliyozingirwa na 'MALAIKA WA SHETANI' na
mafisadi wenye 'ROHO YA PAKA' wanaomsulubisha 'MHARIRI MSALABANI' na kudiriki kusema 'NAJISIKIA KUUA TENA' kupitia mikataba mibovu wanayoisaini 'DAR-ES-SALAAM USIKU' pasipo kumwambia mwekezaji uchwara 'PESA ZAKO ZINANUKA' na tena bila kuogopa 'SALAMU KUTOKA KUZIMU' au kilio chetu cha 'TUTARUDI NA ROHO ZETU?' Buriani Ben Mtobwa!

Nitayakumbuka sana haya majina: Hammie Rajab, Ben Mtobwa, Eristablus Elvis Musiba, Eddie Ganzel, Bawji, Sam Kitogo, Faraji Katalambula, Agolo Andulu, Kajubi Mukajanga, Beka Mfaume...na wengine wengi- hakika hawa ni GREAT THINKERS!!!

Hata hivyo vitabu ninavyovihitaji ni:
Kamlete akibisha mlipiue> Sanda ya Jambazi> Ama zake ama zangu> somo kaniponza> Najuta kuolewa> Tamu ya Haramu> Rest In Peace Dear Mother> Simu ya kifo> Lawalawa Tabora> Kikosi cha Kisasi> Kufa na Kupona> Hofu> Njama> Uchu> Mzizi wa Mbuyu> Malaika wa Shetani> Tutarudi na Roho zetu> Salam toka Kuzimu> Dar-es-Salaam Usiku> Najisikia Kuua Tena> Roho mkononi> Awe hai au amekufa namtaka> Nimekoma ukuwadi na shogayo hasidi> Kikomo> mikononi mwa nunda> Willy Gamba vyoote> Joram Kiango vyoote>

Tusaidiane kutunza hazina hii wadau




No comments:

Post a Comment