BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, December 18, 2009

K-LYINN ATOA SINGO MPYA YA "I' M NOT A FLIRT"

Miss Tanzania 2000 Jacqueline Ntuyabaliwe, ametambulisha wimbo wake mpya wa “I’m Not a Flirt”. Mrembo wa Milenia Jacq, maarufu pia kwa jina lake la jukwaani la K-Lyinn, amesema jana kuwa wimbo huo ni kwa ajili ya albam yake mpya ambayo itatoka mwaka 2010.

“Hii ni single ya kwanza,” alisema muimbaji huyo wa Bongofleva. “Nimesharekodi baadhi ya nyimbo na huu ni mwanzo tu.”
Muimbaji huyo amesema wimbo huo umerekodiwa katika studio ya B.Hitz ya prodyuza bora wa mwaka jana wa tuzo za Kili Hermy B na unamfafanulia mpenzi wake kwamba yeye ni mtulivu katika mahusiano yao.

Unamaanisha kwamba niko kwenye mahusiano, mimi si mhangaikaji wa kimapenzi,” alisema mwanadada huyo. “Namweleza huyo mtu wangu kwamba asihisi kwamba mimi si mwaminifu katika mapenzi yetu,” alisema K-Lyinn bila ya kufafanua kama anajielezea yeye moja kwa moja.

K-Lyinn alisema wimbo huo ameuimba kwa lugha ya Kiingereza ingawa pia kiswahili kimo. Miongoni mwa mashairi katika wimbo huo yanasema: “Wanaume wananitolea macho lakini mimi ni wako, acha wivu.”

Akizungumzia sababu za kuamua kutumia lugha ya Kiingereza ambayo tungo zake hapa nchini zimekuwa zikikosa mapokezi mazuri kwa mashabiki. alisema “Tunawaimbia watu mbalimbali, hivyo tunapaswa kumgusa kila mmoja na pia tunalenga kujitanua kimataifa”

Muimbaji huyo anasema wakati fulani alipokuwa katika ziara zake za kimuziki nje ya Tanzania, alishaulizwa, “Huwezi kutuimbia kwa lugha tuijuayo?” “Ndio sababu nikaamua kutoka namna hii kivingine,” alisema muimbaji huyo aliyepotea kwa muda kwenye gemu ya muziki.

No comments:

Post a Comment