Mkali wa miondoko ya hip hop nchini, kutoka lebo ya micharazo, Harry Samir a.k.a Mr Blue, amekamilisha taratibu zote za kurudi darasani kwa ajili ya kujifunza umombo.
Habari kutoka pande za Ilala, yaliko maskani ya dogo huyo ‘tozi’ anayesumbua katika game la muziki wa Bongo fleva na kibao chake cha ‘Tupo pamoja’ zinasema kuwa, ameamua kuingia darasani kujifunza kiingereza na lugha nyingine kibao za kimataifa, ili kujiweka sawa kwa ajili ya kuupeleka muziki wake kwenye ‘levo’ za kimataifa.

BIG UP KWA KUAMUA KURUDI SCONGA MDOGO WETU
ReplyDelete