BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, December 17, 2009

BLUE KURUDI TENA SHULE KWA AJILI YA KUJIFUNZA KIMOMBO


Mkali wa miondoko ya hip hop nchini, kutoka lebo ya micharazo, Harry Samir a.k.a Mr Blue, amekamilisha taratibu zote za kurudi darasani kwa ajili ya kujifunza umombo.


Habari kutoka pande za Ilala, yaliko maskani ya dogo huyo ‘tozi’ anayesumbua katika game la muziki wa Bongo fleva na kibao chake cha ‘Tupo pamoja’ zinasema kuwa, ameamua kuingia darasani kujifunza kiingereza na lugha nyingine kibao za kimataifa, ili kujiweka sawa kwa ajili ya kuupeleka muziki wake kwenye ‘levo’ za kimataifa.

Mchizi huyo alikiri kuamua kurudi ‘skonga’ na akazidi kumwaga ‘data’ kuwa ameamua kufanya hivyo baada ya kubaini kuwa muziki wake haufiki katika anga za kimataifa kutokana na kushindwa kuimba kwa lugha zinazoeleweka kimataifa. “Nguzo muhimu ya kufika huko ni kujaribu kuimba kwa lugha za kimataifa ambazo zinaeleweka nje ya mipaka ya Tanzania,” alitonya Blue

1 comment:

  1. BIG UP KWA KUAMUA KURUDI SCONGA MDOGO WETU

    ReplyDelete