TID alisema kuwa, imekuwa ni ngumu kwa mtu au kikundi cha watu fulani kuzisaidia bendi zilizoanzishwa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya kama vile Top Band, Machozi Band ya Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ B-Band’ ya Banana Zorro na Bush Band ya Lucas Mkenda ‘Mr.Nice’ badala yake wanazikumbatia za wakuja.“Tunadharaulika sana, bendi zetu zinaonekana ni za wahuni.
Wadhamini wanaona bora wazisaidie bendi za wakongo kuliko zetu. Ukienda kuomba udhamini wanapiga chenga, lakini akienda mkongo anashobokewa kinoma,” alisema T.I.D.
No comments:
Post a Comment