BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Saturday, December 5, 2009

TUNADHARAULIKA SANA NA BENDI ZETU- ASEMA TOP IN DAR

Kiongozi wa TOP Band, Khaleed Mohamed ‘T.I.D’ ameibuka na kuwashutumu vikali wadhamini wanaoshobokea kudhamini bendi za muziki zinazoundwa na wasanii wa kigeni hasa wakongo kuliko zile za wazawa.
TID alisema kuwa, imekuwa ni ngumu kwa mtu au kikundi cha watu fulani kuzisaidia bendi zilizoanzishwa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya kama vile Top Band, Machozi Band ya Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ B-Band’ ya Banana Zorro na Bush Band ya Lucas Mkenda ‘Mr.Nice’ badala yake wanazikumbatia za wakuja.“Tunadharaulika sana, bendi zetu zinaonekana ni za wahuni.

Wadhamini wanaona bora wazisaidie bendi za wakongo kuliko zetu. Ukienda kuomba udhamini wanapiga chenga, lakini akienda mkongo anashobokewa kinoma,” alisema T.I.D.

No comments:

Post a Comment