BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, March 10, 2011

MAZOEZI YA MISS TANGA CITY CENTRAL MOTO!

Warembo wa kitongoji cha Miss Tanga City Central wakiwa katika mazoezi kunako klabu Pweza iliyopo chuda relini. Kitongoji hicho ambacho ndio kimefungua pazia la mazoezi jijini hapa, kimejitapa kutoa mshindi kwa mwaka huu. Mbio za mashindano ya kumsaka mnyange wa Miss Tanga 2011 zimeanza hivi karibuni huku taji hilo likishikiwa na Anna Kiwambo ambaye ni Miss Tanga 210. Miss Tanga 2011 inaandaliwa na kampuni ya New Face Entertainment.

Mwalimu wa kitongoji cha Miss Tanga City Central bibie Mariam Bandawe.

Kitongoji cha Miss Tanga City 2011 kinaandaliwa na kampuni ya Green Apple Entertainment chini ya bibie Aisha Salim mwenye nywele ndefu pichani- akiwa na mwalimu wa dansi kwa warembo bibie Amina. Miss Tanga City inaletwa kwenu kwa udhamini wa Aurora Security, Madam Hair Dressing Saloon, J Pal, Amani Spares, na Anko Mo Blogspot....

No comments:

Post a Comment