BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, April 15, 2011

FILAMU YA FUKWE YAANIKA HISTORIA YA TANGA

BIASHARA ya utumwa katika Pwani ya Tanzania Bara , ilikuwa na faida kidogo. Biashara hiyo ililetwa na Waarabu ambao waliwashawishi wenyeji kwa zawadi ndogo na kujikuta wameingia katika kazi ya kukamata watumwa na kuwauza kwa Waarabu hao. Wananchi wa Bara na Pwani, walikuwa ni wenye nidhamu na heshima kulingana na mila na desturi za kila kabila.

Kama kawaida yao, ukarimu huo uliwagharimu wema bali mahasidi waliotaka rasilimali watu yaani watumwa. Moja ya mikoa ya Tanzania iliyoathiriwa na mfumo wa biashara ya utumwa ni Tanga. Hali hiyo ilitokana na kuingia kwa desturi na utamaduni, ambao baadhi ya vizazi vya koo zilizokuwa zinashirikiana na wafanyabiashara hao waliziiga.

Idadi kubwa ya wakazi wa sasa wa pwani ya mkoa wa Tanga, si wenyeji wa asili ya maeneo hayo, bali ni kizazi cha watumwa waliouzwa kutoka Tanzania Bara, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Zambia, Zimbabwe, Rwanda na Burundi, Msumbiji na Malawi. Historia inaeleza kuwa watumwa walipokamatwa walitembezwa maelfu ya kilometa, wakipelekwa katika vituo mbalimbali vya kukusanyia vilivyotapakaa pwani ya Tanzania Bara, kuanzia Tanga, Pwani, Lindi na Mtwara.

Katika mikoa hiyo minne, Tanga ndiyo uliongoza kwa kuwa na vituo vingi zaidi. Uchunguzi wa mwaka mmoja na nusu uliofanywa kwa ushirikiano wa serikali na Mradi wa Uandishi na Utengenezaji wa Filamu za Historia ya Taifa iliyoitwa Fukwe za Dhahabu, uliondeshwa kati ya Februari 2009 na Septemba 2010 mkoani Tanga, unaonesha kwamba, mkoa wote ulikuwa na zaidi ya vituo arobaini na mbili...............

Kusoma zaidi BONYEZA HAPA



Makala hii imeandikwa na Anna Makange, Tanga.

No comments:

Post a Comment