BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, April 26, 2011

PILI HASHIM NDIO MISS TANGA CITY CENTRAL 2011

Hatimae mnyange wa kitongoji cha Miss Tanga City Central amepatikana huku shindano hilo likiacha historia kubwa. Mwanadada Pili Hashim ndie aliyabahatika kuvaa taji hilo ambalo hapo kabla lilikuwa likishikiliwa na Anna Kiwambo mrembo wa kitongoji hicho kwa mwaka jana. Nafasi ya pili ilichukuliwa na Mishi Juma huku nafasi ya tatu ikienda kwa Salha Ibrahim. Kitongoji ca Miss Tanga City Central kiliandaliwa na kampuni ya Green Apple Entertainment kwa udhamini mkubwa wa Madam Hair Dressing Saloon, Mwanakodo, Sarah Issa, Arbab MB pamoja na Anko Mo Blogspot. Warembo wanne wamebahatika kuingia kunako kambi ya Miss Tanga 2011 ambapo kwa mwaka huu inaandaliwa na kampuni ya New Face Entertainment na itafanyika tarehe 11/06/2011 pale Mkonge Hotel. Kabla ya hapo Miss Tanga ilikuwa ikiandaliwa na kampuni ya Five Brothers Entertainment.

Judith Kitogo ndie alikuwa mnyange wa Miss Talent 2011. Hata hivyo ndie aliyechukua nafasi ya nne na kubahatika pia kuindia kunako ambi ya Miss Tanga

Maximilan Luhanga ndie mkurugenzi wa kampuni ya New Face Entertainement yenye dhamana ya kuandaa Miss Tanga 2011. Hapa akimtangaza mnyange wa Miss Tanga City Central.

Pili Hashim na Mishi Juma ndio walibahatika kuingia fainali. Na hapa ilikuwa presha inapanda, presha inashuka mpaka alipotangazwa mshindi.

Top Five ya Miss Tanga City Central 2011....Pili Hashim (4), Rukia Shemdoe (1), Salha Ibrahim (3), Judith Kitogo (2) na Mishi Juma mwenye namba (5).....

Anaitwa Anna Kiwambo, ndie aliyekuwa anarudisha taji baada ya muda wake kumalizika. Anna Kiwambo pia ndie Miss Tanga 2010.

Mdhamini mkuu Jayesh Ranjiti maarufu kama J Pal akitoa burudani baada ya kuzungumza na watu waliohudhuria. Ilikuwa burudani tupu!!!

Kundi la Town Boys wakitoa burudani

Majaji wakijadili jambo na bibie Aisha ambaye ndie aliyeandaa shindano hilo kutoka kampuni ya Green Apple

Majaji wakiwa makini wakifuatilia warembo.

Warembo wa Miss Central wakipita na vazi la ufukweni.

Wakifungua show......

No comments:

Post a Comment