BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, April 6, 2011

NOEL NI MSHIRIKI WA SHINDANO LA RUKA JUU KUTOKA TANGA


Jina: Noel Joseph Mbelwa

Umri: Miaka 26

Biashara: Muuzaji wa Vinywaji Laini vya Jumla

Namba ya ushiriki: 01




Noel anatoa huduma ya kuuza vinywaji laini kwa bei ya jumla katika eneo la Saruji mkoani Tanga. Baada ya kumaliza elimu ya msingi Noel alijaribu kutafuta elimu zaidi ikashindikana, kutokana na hali ngumu akaamua kuingia kwenye soko la ajira, nayo ikawa taabu.

Hatimaye alipofika Dar es salaam 2006/7 rafiki yake mmoja alimuunganishia kibarua katika kampuni ya SBC, watengenezaji wa vinywaji vya Pepsi. Ndipo Noel akaanza kazi ya kupakia na kupakua soda. Baada ya muda Noel na wenzake walipunguzwa kazi, akaenda Tanga katika hekaheka za kutafuta ajira.

Noel ni mshiriki wa shindano la kumsaka mjasilia mali linaloitwa RUKA JUU chini ya Femina HIP....BONYEZA HAPA upate kujua mengi kuhusu shindano hilo


No comments:

Post a Comment