BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, April 6, 2011

MFAHAMU SAUMU MSHIRIKI WA RUKA JUU KUTOKA TANGA


Jina: Saumu Pongwe Liku

Umri: Miaka 29

Biashara: Duka la Vipodozi

Namba ya ushiriki: 02


Saumu anapatikana mitaa ya Kwaminchi mjini Tanga. Hapo ndipo lilipo duka lake la vipodozi, na mwendo kidogo kutoka hapo lipo duka lake lingine anakouza mavazi ya vijana wa kike na wa kiume. Baada ya kumaliza kidato cha nne Saumu aliamua kutafuta ajira. Aliajiriwa mara mbili lakini katika ajira hizo hakujiona akipata maendeleo.

Akaanza kujiwekea akiba ili ikimridhisha ajiajiri mwenyewe. Ilipofika hiyo siku akaacha kazi, wakati huo akiwa mwajiri wa kituo kimoja cha kuuza mafuta alikokuwa amefanya kazi kwa miaka minne. Akaanzisha biashara ya kuuza nguo kwa kukopesha. Biashara hii haikuwa rahisi kwani alijikuta akigombana na wateja kutokana na usumbufu wakati wa kulipa.

Saumu ni mshiriki wa shindano la kumsaka mjasilia mali linaloitwa RUKA JUU chini ya Femina HIP....
BONYEZA HAPA upate kujua mengi kuhusu shindano hilo


No comments:

Post a Comment