BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, April 6, 2011

RAJAB NAE NI MSHIRIKI WA SHINDANO LA RUKA JUU KUTOKA KILINDI TANGA


Jina: Rajab Mnyamisi Mgongwe

Umri: Miaka 28

Biashara: Mzalishaji na msambazaji umeme

Namba ya ushiriki: 05





Ukifika kijiji cha Gombero wilayani Kilindi, Tanga, ukauliza kumuona Rajab, utaulizwa “yule wa umeme?” ingawa kuna Rajab wengi mitaa ile. Kijana huyu ni mzalishaji na msambazaji umeme pekee eneo hilo tangu 2008. Rajab pia ni mkulima na mfugaji na aliianza biashara yake hii ya kutoa huduma ya umeme kwa mtaji wa kilo kumi tu za mbegu ya maharage alizopanda shambani mwake.

Alipovuna Rajab alipata kilo 40 ambazo alipanda tena na kupata magunia manne ambayo baadhi alihifadhi kama akiba ya chakula na mengine mbegu kwa msimu uliofuata. Alipopanda tena akavuna magunia 10 na ndiyo aliyoyauza na kupata fedha za kwenda kununulia mashine ya kuzalisha umeme.

Rajab ni mshiriki wa shindano la kumsaka mjasilia mali linaloitwa RUKA JUU chini ya Femina HIP....BONYEZA HAPA upate kujua mengi kuhusu shindano hilo

No comments:

Post a Comment