BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, May 12, 2010

JIDE AIBUKA KIDEDEA POLL YA ANKO MO BLOGSPOT!!

Katika shindano lisilo rasmi la kumsaka mkali wa bongo flava nchini Tanzania kwa upande wa wanawake lililokuwa likiendeshwa na Blog hii, hatimae limefikia mwisho huku Lady Jay Dee akiibuka kidedea kwa kupata kura takribani 45 ambazo ni sawa na asilimia 50.53.

Mshindi wa pili katika mchakato huo ni Keisher ambaye amepata kura 17 ambazo ni sawa na asilimia 17.89. Ray C ameshika narasi ya tatu kwa kura 16, huku K-ylln akishika nafasi ya nne kwa kura 16 na Best akishika mkia kwa kura 3.

Kura zote hizo zilipigwa na wadau wa VIJIMAMBO VYA TANGA kupitia Blog hii. Shukrani wote mliojitokeza na kuwapigia kura wasanii manowapenda kupitia Poll iliyokuwa hapo pembeni.

Nimewaletea changamoto nyengine ya kuchagua MKALI WA HIP HOP TANZANIA. Mpigie kura msanii unayedhani ni mkali zaidi ya wote kwa upande wa wanaume. Poll ipo hapo kulia!!

No comments:

Post a Comment