BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, May 10, 2010

NITADAI CHANGU HADI KIAMA- SUMA LEE

Msanii kutoka Tanga Suma lee juzi alifanya mahojiano na kituo cha redio cha East Africa -Katika mahojiano hayo Suma aliulizwa kuhusiana na wimbo wake unaoitwa Driving Crazy aliomshirikisha Quick Rocka mbona hajaufanyia video na nimkali sana.

Jamaa akafunguka na kuelezea ukweli wote ya kwamba alikuwa hana hela na alipomfuata Adamu wa Visul Lab alimwambia anataka video na Adamu akamwambia ni shs laki 9, so Suma yeye akamwambia anatanguliza laki mbili halafu anampa tena laki 3 ndio waanze kushoot itakapoisha atammalizia laki 5 zake.

Cha ajabu anachosema Suma Lee baada yakumpa hiyo hela akawa anamcheki jamaa hapokei simu yake wala nini lakini akimtumia msg za dini hata kama imemfikia nusu Adamu anamjibu tuma tena imekuja nusu lakini swala la kushoot jamaa analipotezea.

Alipoulizwa sasa vipi hiyo hela utamsamehe au inakuwaje..? jamaa alijibu
"hiyo hela nitaidai mpaka kiama, laki mbili nyingi ndugu yangu lazima ataitoa tu"

Mwishoni akasema video hiyo atampatia rafiki yake Kallage ili aifanye na isipotee hivi hivi, kuhusu swala la album Suma alisema album inakaribia kuisha na itakuwa na nyimbo 10 na jina la album itaitwa HESABU ZA MAPENZI, na mtu mzima Marco Chali kutoka MJ Rec ndio ataisimamia kila kitu mpaka iwe sawa kuingia sokoni.

No comments:

Post a Comment