BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, May 20, 2010

TIP TOP INATAFUTA WAREMBO KWA AJILI YA VIDEO YAO MPYA!!

Kundi maarufu Tanzania kwenye anga za muziki wa bongo flava Tip Top Connection linatarajia kufanya video wa wimbo wao mpya unaitwa 'Bado Tunapanda' uliotengenezwa pale Mj Record chini ya producer Markochali.

Akizungumza na VIJIMAMBO VYA TANGA meneja wa kundi hilo Babu Tale amesema kuwa ili kukamilika kwa video hiyo anahitaji warembo watakaopamba katika baadhi ya matukio.

Tale ameongeza kuwa, video hiyo itafanyika siku ya jumapili pale Kunduchi Beach na warembo watapata nafasi ya ku'shine kunako video hiyo itakayotengenezwa na gwiji la kutengeneza video bora nchini Tanzania Adam Juma.

'Bado Tunapanda' umetiwa sauti na wasanii wote wakubwa wa kundi la Tip Top ikiwa ni pamoja na Keisher, Kassim, Tunda Man, na Madee.

Je wewe ni mrembo na unahisi unaweza kuuza sura kwenye video za wasanii wakubwa!!!?? piga namba hii 0652116576

No comments:

Post a Comment