BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, May 6, 2010

NAVAA VIMINI KUONGEZA MVUTO- JIDE

Anaitwa Jide, Lady Jaydee au 'Manka' kama anavyopenda ajulikane siku hizi..ameweka bayana kwamba anapendelea zaidi kuvaa vimini ili kuongeza mvuto na kusisimua mashabiki wake anapokuwa jukwaani.

Lakini hakuishia hapo msanii huyo ameliambia gazeti moja maarufu la nchini Kenya kuwa hapendi kurudia nguo kwa vile anawaogopa mapaparazi.

"Napenda kuvaa nguo fupi kwenye maonyesho na viatu virefu. Nywele zangu pia nazibadili kwa mitindo tofauti kila siku," alisisitiza msanii huyo anayemiliki Machozi Band inayotamba Dar es Salaam.

"Kinachonifanya nionekana tofauti na wasanii wenzangu ni kwamba ninajituma sana na ninapenda sana kutengeneza nywele zangu, ni nadra sana kunikuta kwenye staili moja ya nywele wiki mbili nzima."

"Kujirefusha huwa navaa viatu virefu wakati ninapokuwa jukwaani na magauni au sketi fupi ili miguu ionekane mirefu. Napenda sana staili za mitaa."

No comments:

Post a Comment