BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, May 13, 2010

'VISA NA MIKASA NDANI YA TIP TOP'- TALE

Akiwa kiongozi wa kundi la Tip Top Connection kwa muda wa miaka 12, tangu alipoanza kuunda kundi hilo mwaka 1998 akiwa na Madee, Babu Tale amevunja ukimya na kuamua kuelezea visa na mikasa alivyokutana navyo akiwa kama kiongozi wa kundi hilo.

Hili lilitokana na tetesi zilizoenea kwamba kiongozi huyo ana mpango wa kumrudisha Mb Dog ndani ya kundi hilo soon, hivyo nilimtafuta kiongozi huyo ili aweze kuelezea mkakati wake.

Khamis Shabani Taletale a.k.a Babu Tale anaanza kwa kusema nieleza kwamba taarifa hizo ni za kweli na hivi sasa yupo katika maandalizi ya kumrudisha msanii huyo ikiwa atakuwa tayari kuungana na kundi hilo tena kwa mara ya pili.

Hata hivyo Tale alipoulizwa kuhusiana na maamuzi ya wasanii wengi kuchomoka ndani ya kundi hilo na kila mmoja kuelezea sababu iliyomfanya atoke, licha ya sababu zao kufanana lakini Babu Tale alieleza kuwa sababu hizo si za msingi.

Mb Dog, alitangaza kudhulumiwa
"Sina ubaya wala matatizo na Mb Dog kwani aliondoka ndani ya kundi bila kukwaruzana, lakini kilichonisikitisha nilimsikia katika mahojiano na vyombo vya habari akielezea kuwa uongozi wa kundi ulikuwa haumtendei haki.

Tale alielezea kuwa kurudi kwa Mb Dog kutakuwa na mabadiliko ambayo yatakuwapo ndani ya kundi na itategemea namna msanii mwenyewe atakavyokubaliana na uongozi wa kundi.

Hata hivyo alieleza kuwa kuna wasanii wengi sana ambao hivi sasa wanatumia mgongo wa Mb Dog bila mwenyewe kujua, hivyo iwapo atasimama chini ya mwamba imara ataweza kurudi upya na kwa kasi kubwa kwenye game.

Spark, 'Nipe ripoti' ya Tundaman
"Msanii huyu alikuja kwangu mikono nyuma lakini siamini katika kile ambacho amenifanyia katika kipindi cha mwisho, mimi sio Mungu lakini sidhani kama nitampokea tena ndani ya kundi langu.

"Nilimsaidia kwa kiasi kikubwa sana mpaka alipoweza kufika alipofika, lakini baadaye alianza kuwa na utovu wa nidhamu hali iliyosababisha tumkanye mara kwa mara nikiwa na Abdi Bonge (mwekezaji katika kundi) lakini haikusaidia.

Tale anasema, kutokana na tatizo la Spark kutokupata shoo baada ya kutoa singo yake 'Usiniache' Bonge alishauri watoe albamu ya pamoja na Tundaman ili waweze kunyanyuana.


Z' Anto, nilimkuza kisanii nashangaa alinikashfu
"Kwa madai yake alisema kwamba mkataba wa kazi kati yake na Tip Top umeisha, kitu ambacho hakikuwa sahihi" Ninasikitika sana kwani katika wasanii ambao wamekuzwa vipaji vyao wakiwa Tip Top huyu ni mmojawapo, kwani hakuwa na kitu chochote".

"Lakini mpaka anaondoka kwetu alikuwa amejijenga na kutembelea gari, iliniuma sana kwani sikutegemea kama siku moja angeweza kufanya aliyoyafanya" anasema Tale na kuongeza kuwa kati yake na Z Anto hawakuwahi kugombana.

Licha ya matatizo yaliyotokea, Tale anasema kuwa msanii huyo hivi sasa amejitokeza na kuwasiliana na Bonge kwa njia ya simu akihitaji kurudi tena upya ndani ya kundi hilo.


PNC alikana msaada wangu
"PNC alifika toka Mwanza akiwa hana la kufanya, katika kipindi hicho chote alikuwa chini ya Mully B ambaye alikuwa akimsaidia sana kutokana na kipaji alichokuwa nacho.

"Baada ya kutaka kumsaidia niligundua kwamba hana pa kuishi hivyo niliamua kuishi naye katika nyumba yangu na nilikuwa nikilala naye kitanda kimoja mpaka pale nilipohitaji kuoa ndipo nilipomhamisha na aliendelea kuishi chumba kimoja na mdogo wangu.

"Lakini tabia zake zilianza kubadilika na baadaye nikaja kumsikia katika kipindi kimoja cha mahojiano akijieleza kwamba ameamua kujitoa Tip Top maana hakuna msaada wowote anaoupata na hajawahi kusaidiwa na mimi, niliumia sana.

Pingu ana majungu, mnafiki
"Kwa kweli nitasema kwamba Pingu ndiye aliyemshawishi Z Anto atoke ndani ya kundi, naye bila kufikiri akafuatana naye lakini hawakufika mbali wakabwagana.

"Baada ya kutoka alianza kuongea majungu mengi tu hii ilidhihirisha kwamba Pingu hakuwa mtu mzuri katika kundi kwani alikuwa unafiki.

Babu Tale anasema kwamba walikwenda Nairobi Kenya kwa ajili ya kurekodi Video na Juakali, kwa pesa zake lakini baada ya kutoka kwa wasanii hao walianza kumdai video hiyo ndipo yeye alivyoamua kuifuta.


Tale anasema kuwa licha ya yote waliyoyafanya mpaka sasa hakuna msanii ambaye alitoka nje ya kundi na bado anafanya vizuri, wengi wamerudi nyuma. Pia alisisitiza kwamba msanii kusimamiwa ni tofauti na akijisimamia yeye mwenyewe.

"Katika kundi tunafanya kazi kama 'Brothers' (ndugu) hivyo inakuwa rahisi wao kunizoea hivyo wanapofikia maamuzi mazito wanashindwa kunishirikisha.

Tale ni baba wa mtoto mmoja aitwaye Tale Junior huku akiwa na mkewe ambaye amekiri kumpenda kuliko mwanamke mwingine yeyote. Pia ni mdogo wa mwekezaji wa kundi hilo Abdi Bonge ambaye kwa hivi sasa amejiweka pembeni na kundi hilo na kuendelea na mambo yake mengine.

Kundi hilo hivi sasa lina vinara watano ambao bado wanakubalika katika ulimwengu wa muziki wa kizazi kipya kama Keisha, Tundaman, Madee, Cassim na Deso licha ya kuwepo wasanii wengine chipukizi.

No comments:

Post a Comment