BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Sunday, May 30, 2010

WITNESS JUSTINE NDIO MISS NGAMIANI 2010!!

Mnyange wa Miss Ngamiani 2010 Witness Justine akiwa katika uso wa furaha punde tu baada ya kutangazwa mshindi wa kitongoji chicho. Mshindi wa pili alikuwa Asha Thabit huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Tabu Mrisho. Kitongoji cha Miss Ngamiani 2010 kiliandaliwa na kituo cha redio Breeze Fm kilichopo jijini Tanga.

Ilikuwa mashamsham baada ya Witness kutangazwa kuwa mshindi, mashabiki wake walishindwa kujizuia.

Mapaparazi nao hawakuwa nyuma.

Nilipenda hii- Baba na Mama Witeness walikuja kumpa pongezi mtoto wao.

Baba akionyesha 'dole' ishara kwamba mwanangu ndio kiboko yao!!

Oooohh baba! baaaba baba, babaaaaaa! Baba huyo, babaaaaa babaaaaa huyo babaaaa, baba huyo babaaaaaaaaaa!! Safi sana baba

Mkurugenzi wa 5 Brothers Entertainment Nasoro Makau akiwa juu ya stage, tayari kumtangaza mshidni wa Miss Ngamiani. 5 Brothers ndio inandaa Miss Tanga 2010, ambayo itafanyika tarehe 19/06/2010 kunako hoteli ya Tanga Beach Resort.

Alipotaja mshindi wa tano, wanne na watatu! Wakabakia hawa....ilikuwa presha inapanda na kushuka!!

Hapa ilikuwa presha juuuuuuuuuu!!!

Hii ndio ilikuwa Tano Bora ya Miss Ngamiani 2010.

Burudani kibao zilikuwepo...ngoma za asili hiyo!

Jamaa alipoiga bonge la show!

Mtangazaji wa redio Breeze Fm anaitwa Fabby- ndio alikuwa Mc wa shughuli nzima.

Kundi la TMC ambalo linazidi kupanda chati jijini Tanga likitoa burudani...jamani, hawa jamaa wanaimba ile mbaya! sikiliza wimbo wao wa 'Tuna Bang Zaidi Yao' hapo juu palipoandikwa SIKILIZA TANGA FLAVA HAPA!

Man Sasha wa kundi la TMC akiwa kazini.

Dogo pamoja na Dokta Leader wote wa TMC....

Yassir 'Yeyo' akiwa na Dj wa Breeze Fm Dj Bob Nass

Lunza, Amina ambaye alikuwa mwalimu wa warembo pamoja na Fabi- nyhuma ya stage wakiweka mambo sawa.

Hawa ndio walimu wa warembo....mwalimu Lunza pamoja na mwalimu Amina. Amina pia ndio mwalimu wa warembo wa Miss Pangani 2010 ambayo inaandaliwa na Anko Mo Blogspot. Miss Pangani itafanyika siku ya ijumaa ya terehe 4 kwenye ukumbi wa Safari Lodge Annex.

Amina katika pozzz!!!

Warembo wakiwa katika vazi la asili ambalo walifanyia show ya ufunguzi.

Mdau pamoja na Dj Bob Nass.

Palikuwa hapatoshi...watu wakifuatilia mchakato. Ilifanyika katika uwanja wa Mkwakwani VIP.

Raha Tupu!!!!

No comments:

Post a Comment