BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, May 10, 2010

'PASTOR'- NGOMA MPYA YA ROMA!!

Mkali wa Hip Hop kutokea Tanga City Rymes Of Magic Attractio ama ROMA, ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Pastor. Ngoma hiyo ambayo ameitengeneza pale Tongwa Record, imebeba maneno ya kiroho yenye kuletea upako na kurudisha wokovu kwa waliopotea na Roma mwenye ndio Pastor!!

Wimbo unaanza hivi- "I am the pastor of this church, i am the pastor of this churh......Fanya ishara ya msalaba upokee haya maubiri, mimi ni mteule ninawaletea injili, nina ushuhuda wa kiroho bwana yu aja msubiri, natangaza UPAKO na habari za mnara wa Babeli"

Kama vipi unaweza kuusikiliza hapo juu palipoandikwa SIKILIZA TANGA FLAVA HAPA! Tayari Roma anatamba na ngoma zake kama Salute, Tanzania pamoja na Mr President ambayo hadi sasa bado inafanya vizuri karibu kila redio nchini Tanzania.

Roma pia ametajwa kwenye Teen Extra Award category ya 15. Lyricist Of The Year ambapo anachuana na wasanii wengine kama Fid Q, Niki Wa Pili, Ngwea, Joh Makini, Jay Moh na G Nako. I know Tanga tunaweza na ROMA ndie msanii pekee anayestahili kuwa Lyricist wa mwaka kutokana na tungo za ukweli zinazopatikana kwenye ngoma zake zote!

Unachotakiwa kufanya ni kufungua hii website http://www.nipe5.com Utakapoifungua angalia mkono wako wa kushoto kuna sehemu imeandikwa Teen Extra Award hapo utabonyeza kwa ajili ya kuona washiriki wote halafu utaingia kipengele cha 15. Lyricist Of The Year na hapo utabonyeza jina la ROMA.

Au kuingia moja kwa moja kwenye hiyo web site na kumpigia kura Roma Bonyeza Hapa

No comments:

Post a Comment