BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, May 18, 2010

NGOMA MPYA YA TIZZLE- KUTOKA TANGA MPAKA LONDON!!

(Tizzle na Damuz)

Msanii kutokea jijini Tanga anayejulikana kwa jina la Tizzle ambaye hivi sasa anaishi nchini Uingereza kuonako jiji la London, amechia ngoma yake mpya inayoitwa 'Nameless' aliyomshirikisha Damuz.

Akiongea na Blog hii moja kwa moja kutokea Uingereza, Tizzle amesema kuwa ngoma hiyo ameifanya pale studio za East London kwenye studio moja inaitwa Mzuka Entertainment Rec chini ya producer Josh.

Tizzle aliongeza kuwa, anaamini ngoma hiyo itamuweka pazuri kunako ramani ya Bongo Flava na duniani kwa ujumla kwa kuwa ina kiwango cha kimataifa. Sikiliza wimbo huo hapo juu palipoandikwa SIKILIZA TANGA FLAVA HAPA! Song: NamelesS, Artist: Tizzle feat Damuz

Msanii huyo ambaye kabla ya kwenda Uingereza alikuwa anaishi pale Majani Mapana na baadae kuhamia Bara Bara ya 15, kwa sasa yupo anajipanga kutoka na ngoma nyingine ya 'Hisia Zangu' ambayo atawashirikisha washkaji zake damuz, josh pamoja na danny.

Mpango wa albamu unakuja na ataipa jina punde tu itakapokamilika.



No comments:

Post a Comment